Jambo kwa wote, naitwa Dean Davis, na tazama ''ongezeka'' ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa katika vijiji.
Wakati nilipoanza kupanda makanisa katika miaka ya 1980, nilikuwa bado kusikia neno ''mtu wa amani'', hata na rafiki zangu nao pia. Tulijifunza Luka 10:1-10, pale ambapo Bwana wetu Yesu anafundisha wamitume wake 72 kutafuta watu wa amani.
Lakini, hatukuwai kusisitiza juu ya fundisho kubwa linalohusu kifungu hiki;
Kuko wanaume na wanawake, kwa eneo nyingi, waliyo tayarishwa na Mungu ili wapokee injili na kuwapokea wale wanaotangaza Habari njema. Mutafute hawa wanaume na hawa wanawake. Mukae pamoja nao wakati wote munao tangaza ufalme wa Mungu.
Moja ya hadisi za Biblia zinazovutia zaidi zinazohusu mtu wa amani, ni ile inayohadisia kukutana kwa Yesu na mwanamuke Msamaria kwenye kisima. (Yohana 4:1-43). Yesu alikutana na mwanamuke Msamaria aliyekuwa na sifa mbaya. Lakini alikuwa na kiu ya kumjuwa Mungu. Wakati aliposikia Habari njema, alitangaza habari kwa mji wote. Bwana wetu Yesu alibaki siku mbili pamoja na waamini wa Samaria mbele ya kuendelea na huduma yake Galilaya.
Baada ya ufufuko wa Yesu na ujio wa Roho Mtakatifu kwa wanaume na wanawake waliokusanyika kwenye mzunguuko wa ndani, wamitume walikawia kufanya mafundisho ya kutafuta watu wa amani. Hakika, waliendelesha kanisa lao pa Yerusalemu na wakatangaza Habari njema ya ufalme wa Mungu. Lakini wamitume hawakutafuta watu wa amani inje ya mji. Ilibidi miujiza mingi itendeke ili hiyo ifanyike.
Petro alimpata mtu wa amani aitwaye Kornelio. Hadisi ya kukutana kwao inapatikana katika Matendo ya Mitume, sura 10. Kornelio alikuwa kasisi wa jeshi la kirumi. Kupitiya ujuzi wake, petro hakupenda kabisa kushirikiana na Warumi.
Lakini Mungu alimuelewesha kiwazi katika ndoto kwamba angestahili kwenda kumuona Kornelio. Akampata mtu mwenye sifa njema, aliye na kiu ya kumjuwa Mungu. Kornelio alikusanya majirani na rafiki zake ili wasikie mafundisho ya Petro. Wakati Petro akihadisia hadisi ya Yesu na kueleza unabii wa Agano la kale kumuhusu, Roho Mtakatifu akawashukia hata na kwa wapagni ! Petro akabatiza walio amini na kubaki nao kwa mda wa siku chache.
Mumeona njia ? Mungu anatayarisha watu kupokea injili. Anawapa kiu ya kumjuwa. Waamini wanapokea ujumbe wa Yesu, ujumbe wa mpango kabambi wa Mungu ili kuokowa ulimwengu ulio vunjika. Wakati watu wa amani wanasikia Habari njema, wanaipokea. Wanakuwa na kiu ya kuijuwa zaidi. Hawachungi injili kwa ajili yao wenyewe ; wana alika rafiki zao kuisikiliza. Waamini wanao tangaza Habari njema wanabaki na waamini wapya kwa kujenga imani yao. Kuko watu wa amani ambao Mungu anataka mukutane nao. Kuko watu wanao ishi karibu yenu na wako na kiu ya kumjuwa Mungu. Muwaombee. Muwatafute. Muombe pamoja nao. Mugawe Habari njema pamoja nao. Mubakiye nao. Muwaambiye kuhusu Yesu kwa majirani na rafiki zao.
Ndiyo ! Kuko watu wa amani ambao Mungu anataka mukutane nao.
Ilikuwa ''ongezeka'', na mimi Dean Davis, nawauliza ni pamoja na wanani utagawanya nao leo neno hili la kutiya moyo ?










