Jambo kwa wote, naitwa Dean Davis, na tazama ''ongezeka'', ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa katika vijiji.
Kutangaza injili kupitiya njia ya miviringo tatu ni namna muhimu ya kugawanya Habari njema ya Yesu na kualika kila mtu amkubali Kristo kuwa Mfalme wa maisha yake. Umejifunza kusimulia hadisi kubwa ya Mungu kwa kuchora njia hii, kila miviringo kwa kila kipindi. Endelea kujifunza, endelea kuchora na uendelee kutangaza Habari njema ! Unajuwa kama unaweza kutumikisha njia ya miviringo tatu kama chombo kwa kufanya wanafunzi ? Inawezekana !
Shabaa yetu, kama wapandaji wa makanisa, ilionyeshwa vizuri na Mtume Paulo. Alisema kumuhusu Yesu : "Ni yeye tunaye mushuhudia, akionya na kufundisha kila mtu kwa hekima yote, ili kumuonyesha kila mtu aliye kamili ndani ya Kristo.'' miviringo tatu inaweza kukusaidia kumleta mtu kwa Kristo. Inaweza pia kukusaidia kutambuwa ao kujuwa mahali alipo mwamini katika
njia yake kuelekea ukomavu kamili katika Kristo. Tazama namna ya kufanya : mbele ya yote, onyesha njia ya miviringo tatu kwa mwamini. Baadaye, ukianzia mviringo uliyo juu upande wa kuume, uliza : ni kwa namna gani umegunduwa kama ulimwengu tunamoishi umevunjika ? Namna gani unajaribu kukwepa haya mateso mbele ya kukutana na Kristo ? Sikia kwa makini. Uliza maswali ya ziada, onyesha hali ya utulivu, ya huruma na umupe moyo. Kisha, onyesha mkuki uliyo kati ya mviringo wa dunia iliyo vunjika na mviringo wa Kristo.
Uliza rafiki yako : "ni wakati gani uliacha uasi wako ili kunyenyekea na kuomba Kristo awe Bwana na Mfalme wako ?'
Ongea na mwamini kuhusu toba na imani yake. Baada ya hayo, hakikisha kwamba Yesu ni yeye Mfalme wa maisha ya rafiki yako.
Kwa mwisho, onyesha mtu huyo anayezunguukwa na nukta zenue mwanga. Taswira hii inawakilisha mtu aliyepata amani na imani. Uliza sasa rafiki yako :"je ! Unamrudilia Mungu? Unaishi maisha mapya ambayo Yesu alitowa kwa ajili yako msalabani ?" Kwa kila wakati, anapopatwa na tatizo, unaweza kumsaidia rafiki yako kuelekea ukomavu wake kama mwanafunzi. Pengine bado kabisa haja omba msamaha. Pengine bado hajamkubali Yesu kama Mfalme. Pengine hajahisi nguvu za Roho Mtakatifu ili kuishi maisha yaliyo badilishwa ndani ya Mungu. Kwa kutumikisha mtindo wa miviringo tatu wakati wa mazungumuzo na mtu anayejiita Mkristo, unaweza kutambuwa ni wapi alipo kuhusu njia ya ukomavu ya ukristo. Sasa, utajuwa namna gani ya kumsaidia kukomaa akiwa kama mwanafunzi.
Ilikuwa "ongezeka", na mimi ni Dean Davis, nawaalila kutumikisha miviringo tatu ajili ya kutangaza injili ET mafundisho ya wanafunzi.

.jpeg)

.jpeg)




