Jumatano, 15 Aprili 2026

MIVIRINGO TATU AJILI YA KUWAFANYA WANAFUNZI

 













Jambo kwa wote, naitwa Dean Davis, na tazama ''ongezeka'', ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa katika vijiji.

Kutangaza injili kupitiya njia ya miviringo tatu ni namna muhimu ya kugawanya Habari njema ya Yesu na kualika kila mtu amkubali Kristo kuwa Mfalme wa maisha yake. Umejifunza kusimulia hadisi kubwa ya Mungu kwa kuchora njia hii, kila miviringo kwa kila kipindi. Endelea kujifunza, endelea kuchora na uendelee kutangaza Habari njema ! Unajuwa kama unaweza kutumikisha njia ya miviringo tatu kama chombo kwa kufanya wanafunzi ? Inawezekana !

Shabaa yetu, kama wapandaji wa makanisa, ilionyeshwa vizuri na Mtume Paulo. Alisema kumuhusu Yesu : "Ni yeye tunaye mushuhudia, akionya na kufundisha kila mtu kwa hekima yote, ili kumuonyesha kila mtu aliye kamili ndani ya Kristo.'' miviringo tatu inaweza kukusaidia kumleta mtu kwa Kristo. Inaweza pia kukusaidia kutambuwa ao kujuwa mahali alipo mwamini katika

njia yake kuelekea ukomavu kamili katika Kristo. Tazama namna ya kufanya : mbele ya yote, onyesha njia ya miviringo tatu kwa mwamini. Baadaye, ukianzia mviringo uliyo juu upande wa kuume, uliza : ni kwa namna gani umegunduwa kama ulimwengu tunamoishi umevunjika ? Namna gani unajaribu kukwepa haya mateso mbele ya kukutana na Kristo ? Sikia kwa makini. Uliza maswali ya ziada, onyesha hali ya utulivu, ya huruma na umupe moyo. Kisha, onyesha mkuki uliyo kati ya mviringo wa dunia iliyo vunjika na mviringo wa Kristo.

Uliza rafiki yako : "ni wakati gani uliacha uasi wako ili kunyenyekea na kuomba Kristo awe Bwana na Mfalme wako ?'

Ongea na mwamini kuhusu toba na imani yake. Baada ya hayo, hakikisha kwamba Yesu ni yeye Mfalme wa maisha ya rafiki yako. 

Kwa mwisho, onyesha mtu huyo anayezunguukwa na nukta zenue mwanga. Taswira hii inawakilisha mtu aliyepata amani na imani. Uliza sasa rafiki yako :"je ! Unamrudilia Mungu? Unaishi maisha mapya ambayo Yesu alitowa kwa ajili yako msalabani ?" Kwa kila wakati, anapopatwa na tatizo, unaweza kumsaidia rafiki yako kuelekea ukomavu wake kama mwanafunzi. Pengine bado kabisa haja omba msamaha. Pengine bado hajamkubali Yesu kama Mfalme. Pengine hajahisi nguvu za Roho Mtakatifu ili kuishi maisha yaliyo badilishwa ndani ya Mungu. Kwa kutumikisha mtindo wa miviringo tatu wakati wa mazungumuzo na mtu anayejiita Mkristo, unaweza kutambuwa ni wapi alipo kuhusu njia ya ukomavu ya ukristo. Sasa, utajuwa namna gani ya kumsaidia kukomaa akiwa kama mwanafunzi.

Ilikuwa "ongezeka", na mimi ni Dean Davis, nawaalila kutumikisha miviringo tatu ajili ya kutangaza injili ET mafundisho ya wanafunzi.

MIVIRINGO TATU AJILI YA KUTANGAZA INJILI

 













Jambo, na karibu kwenye ''ongezeka'', ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa katika vijiji.

Mimi ni Brad Snowden. Wakati ninapo gunduwa kitu kizuri, napenda kuigawanya, na ikiwa najuwa kwamba hiki chombo kiko rahisi kwa matumizi muhimu, siwezi kujizuwia kuigawanya.

Leo, tutagunduwa chombo cha kutamanika ajili ya kutangaza Habari njema ya Yesu-Kristo. Mungu anatupa namna ya kugawanya hii habari njema pamoja na wale bado hawajasikia kuhusu upendo wake. Chombo ambacho tutagunduwa leo ni kile cha miviringo tatu. Ni chombo chenye nguvu kwa kutangaza injili ya Yesu-Kristo kwa watu wote. Miviringo tatu ni taswira rahisi inayoshindikiza ushuhuda wako kuhusu Yesu-Kristo. Kuko vipendele sita rahisi kwa  kugawanya hiyo ushuhuda, na miviringo tatu zinaweza kuchorwa kwenye karatasi wala chini kwenye udongo. Nani asiye tamani taswira nzuri? Ndiyo lengo kabisa ya chombo hicho. Tunaweza sasa kuongea kuhusu mpango wa Mungu, kwa namna alivyo umba dunia, na vile tunavyoishi ndani ya dunia iliyovunjika na dhambi. Kwa kutumikisha miviringo tatu,  unaweza kugawanya hadisi yote, kuanza uumbaji hadi kwenye msalaba. Hii inatupa chombo rahisi ambacho kinaweza kutumikishwa na watu wote.

Kwa kuchora miviringo na kwakuielewesha,  maelezo yanakuwa rahisi. Hii inatupa pia fursa ya kuwauliza moja kwa moja kama wako tayari kupokea Yesu-Kristo. Chombo hiki kina nguvu tena ni cha muhimu, na ubora wake zaidi ni vile hakiitaji kukariri maandiko. Kama ukikariri maandiko inakuwa bora zaidi, na unaweza kuigawanya. Nafurahia uumbaji wa Bwana anaye turuhusu kugawanya upendo wake kwa wote.

Anatupa vyombo vinavyo rahisisha ugawaji.

Wakati tunataka kutayarisha shamba kwa upandaji, hatuwezi kwenda bila vyombo vyetu, na baadaye tunastahili kuvitumikisha kwa kupanda mbegu. Inaenda sambamba na chombo cha miviringo tatu ambacho Mungu ametupatiya. Tunapashwa kujizoweza kwa kuvitumikisha, na zaidi mutakavyo vitumikisha kwa nguvu zenu kwa kutangaza injili, zaidi itakuwa rahisi. Ninajuwa kama Mungu atawatumikisha, na hiyo itakuwa na nguvu kwa Ufalme. Tazama neno la kutiya moyo kwa wasimamizi wa upandaji wa makanisa katika vijiji.

Ni kwa wanani utagawanya nao leo?

Mungu awabariki !

SIMULIA HADISI YA MUNGU

 











   Jambo kwa wote, mimi ni Dean Davis, na tazama ''ongezeka'', ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa katika vijiji.

Moja ya ujuzi wa muhimu kwa msimamizi wa upandaji wa makanisa ni uwezo wa kusimulia hadisi ya Mungu kwa uwazi, kwa ufupi na kwa kushawishi. Biblia inatuhadisia hadisi kubwa. Lakini Biblia ni kubwa. Siyo Kitabu kimoja, lakini ni mchanganyiko wa vitabu 66 tofauti ambavyo vinaambatana vyote kuelekea Yesu, Mwokozi wa ulimwengu. Hivo basi, wakati tunapotangaza injili, tunapo fundisha, tunapo omba, ao kushauri, tunastahili kuchunga moyoni hadisi kubwa  na kuirejelea mara kwa mara.

Kwa mda wa myezi tatu ya mpango mpya wa upandaji wa makanisa katika vijiji, wasimamizi wa upandaji wa makanisa wanajifunza kusimulia hadisi ya Mungu mnamo dakika 10 ao chini ya mda huo. Bali, ili kuweza kufupisha kiini cha neno la Mungu kwa hadisi ya dakika 10, inastahili kuifahamu vizuri. Kwa kweli, inastahili kujuwa hadisi ya kila kitabu cha Biblia na kuelewa Mada zake maalum, kama vile upendo, utakaso na dhambi, kujitolea na wokovu, ukombozi na msamaha, pamoja na neema na imani. Lakini usivunjike moyo kama haujuwe vizuri vitabu vyote vya Biblia wala kama hauelewi vizuri Mada zake maalum. Anza kusimulia hadisi kubwa ya Mungu ukifuata mtindo wa miviringo tatu. Daima ongeza ufahamu wako kuhusu hadisi hii. Soma ao usikie Biblia katika lugha yako ya asili. Anza kusoma Mwanzo na umalize na Ufunuo. Usiogope kama hauelewi vipendele vyote. zingatia tu  mada maalum za Biblia.

Kwa kuendelea kwako kusoma, Mada hizi zitajirudilia bila kukoma : upendo na msamaha, utakaso na dhambi, kujitowa na wokovu, ukombozi na msamaha, pamoja na neema na imani.

Zaidi unavyojuwa watu muhimu na Mada za muhimu za Biblia, zaidi utatayarishwa kusimulia hadisi ya Mungu kwa ufupi na kwa ukubalifu.

Inastahili kujuwa kila kifungu cha Biblia ili kutangaza hadisi ya Mungu kwa misheni ya injili wala mafundisho kwa wanafunzi ?

Apana. Lakini zaidi unavyoelewa, vizuri zaidi utaweza kusimulia hadisi ya Mungu na kuikabili sawasawa na maitaji ya wasikilizaji . Stafano, moja ya watu wa Mungu walio na ushawishi zaidi, aliishi pamoja naye. Hadisi yake inasimuliwa katika kitabu cha Matendo ya Mitume, sura ya 7. Stafano alijuwa hadisi ya Mungu. Alipoalikwa, alijuwa kuisimulia kwa ufupi na kuweka mojamoja kwenye vitendo. Hata kama wasikilizaji wake hawakuitikia vizuri, ushuhuda wake uliashiria mabadiliko katika historia ya kanisa.

Utukufu wa Mungu ulijitukuza wakati Stefano alisimulia hadisi yake kwa ujasiri. Sasa, usivunjike moyo na uendelee na utafiti wako ili kujuwa hadisi ya Mungu, kwa kuelewa Mada maalum na kujuwa kuisimulia. Kama hauna Biblia ya sauti katika lugha yako ya asili, jielekeze kwenye mtandao wa Google Play store ili uweze kupokea (télécharger l'application Bible) na hapo utapokea Biblia za sauti katika ma mia za lugha za nyumbani.

Ilikuwa ''ongezeka'', na mimi Dean Davis, nawauliza ni pamoja na wanani utagawanya nao leo neno hili la kutiya moyo ?

Maendeleo ya Uongozi - Baazi ya tabia za ziada za kutafuta kwa viongozi wanaojitokeza

 












Mimi ni Chuck Rapp na ongezeka, ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wasimamizi na wapandaji wa makanisa katika vijiji.

Mada yetu katika mwaka huu wa 2026 ni maendeleo ya Uongozi. Katika vipindi vyangu viwili vya nyuma, niliongea kuhusu tabia mbali mbali ambazo nazitafuta kwa viongozi wanaokuja. Kwa mtazamo wangu, cha muhimu ni utambulisho mkubwa unao shikamana na Yesu-Kristo pamoja na unyenyekevu. Turu ya mwisho niligusia

umuhimu wa historia na ujuzi wa mtu.

Leo, natarajia kugawanya mawazo mamoja kuhusu tabia zingine tatu ninazo zitafuta kwa viongozi wanaokuja : mpangilio, hamu ya kufunzwa na kukomaa, usikivu wa kupokea mafundisho.

Nafikiri kwamba munaweza kuona ukamilishano wao.

* Mpangilio unatafsiriwa kama "uwezo wa kuchunguza na kuanzisha vitendo kwa namna ya kibinafsi". Walio  na moyo wa kuongoza hawangojee kuambiwa nini watafanya. Wanatenda. Isipokuwa, kitu cha muhimu ni kwamba wafanye yaliyo "haki", na ndipo hapo uchunguzi unakuwa wa muhimu. Kwa kurudilia podikasti yangu ya nyuma, mtu iko na tabia ya kufanya uchunguzi wa haki na kutenda ipasavyo? Nafikiria watoto wa Isakari katika 1Mambo ya nyakati 12:32. 

"Na wa wana wa Isakari, watu wenye akili za kujua nyakati, kuyajua yawapasayo Israeli wayatende; vichwa vyao walikuwa watu mia mbili na ndugu zao wote walikuwa chini ya amri yao."

* Ya pili, hamu kubwa ya kujifunza na kuendelea ni muhimu kwa maendeleo ya viongozi wanaokuja. Mara nyingi wanasema ''viongozi ni wanafunzi" na ninaamini kama ni kweli kabisa. Wakati ninapochunguza viongozi wanaokuja, ninakuwa mwangalifu kwa wale walio na moyo wa kupenda kujuwa na wanaoitaji kujifunza elimu mpya na kuendeleza ujuzi mpya. Hawasite kutowa nguvu na mda mwafaka ajili ya kuendelea,  katika suala la nguvu na uwezo.

* Kwa kulinganisha moja kwa moja na nukta yangu ya pili, ni muhimu kwamba viongozi wapya wawe wasikivu kwa mafundisho. Mithali 1:5 inatushauri "mwenye hekima asikie na kuongezewa elimu, na mwenye ufahamu ayafikie mashauri yenye njia.'' viongozi vijana wanastahili kuonyesha alama ya unyenyekevu (kama nilivyoizungumzia mwezi uliyopita) kwa kusikiliza na kujifunza, na wanastahili kuwa wenye utambuzi kwa mashauri wanayopokea. Wakati ninapo tazama na kuchunguza viongozi wapya, ninatafuta kutambuwa  washauri wao. Je ! Wako na mwenendo mzuri wa kufuata?

Nitaendeleza mawazo yangu kuhusu tabia za kutafutwa kwa viongozi wanaokuja katika podikasti yangu inayokuja.

Ujumbe huu ni wa kutiya moyo kwa wapandaji na wasimamizi wa makanisa katika vijiji.

Alhamisi, 2 Aprili 2026

NAMNA GANI UTATAMBUWA WATU WA AMANI

 










    Jambo kwa wote, naitwa Dean Davis na tazama ''ongezeka'', ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa katika vijiji.

Moja ya uzoefu wa mafanikio ambayo Mtumishi Mkristo anastahili kuishi ni kutafuta na kupata watu wa amani. Munajuwa kama mtu wa amani ni mwanaume ao mwanamuke, aliyetayarishwa na Mungu kwa kupokea injili na kujibu kwa wajumbe wa injili wakati wanaleta Habari njema. Munajuwa watu wa amani wanaoonyeshwa ndani ya Biblia : Mwanamuke Msamaria kwenye kisima, Kornelio, Lidia, Mlinzi wa gereza kwa Filipo na wengine zaidi. Munajuwa namna gani Mungu alivyotayarisha watu hawa kupokea Habari njema na kuweka mawasiliano kati ya wajumbe wa Habari njema na watu wengine ndani ya miji na vijiji. Mfano wao unafuata mtindo ambao Yesu aliwafundisha wamisionari 72. Mtindo huo wa huduma ulioonyeshwa na Yesu, unapatikana katika Luka 10.1-10.

Sifa kwa Bwana, mtindo huu wa huduma ulioanzishwa na Mwokozi bado ungali nguvu hata leo.

Ninakumbuka wakati nilipokuwa nikisaidia kupanda kanisa pa Quito, inchini Équateur. Nilikuwa nikishiriki katika kusanyiko la maombi, ndipo nilipo pokea wito wa kasisi wa Hospital. Alisema : "kuko bwana moja hapa ambaye ameonekana na ugonjwa wa uvimbe kwenye kifuko cha mkojo. Iko na woga sana. Anapashwa sasa kutoka kwenye Hospital yetu nakujielekeza kwenye hospital ingine.

Unaweza kutuma mtu moja wa kanisa lenu kuongea naye haraka?''

Nilijielekeza mara moja kwenye hospital na nikaojiana na yule bwana pamoja na mke wake.

Alikuwa hakika mwenye woga sana. Alijuwa ugonjwa wake. Nilimwambia kama ni mapenzi ya Mungu kuponya watoto wake, iwe hapa chini wala katika ulimwengu ujao.

Niligunduwa kwamba hakuwa nauhakika wowote wa kuwa mtoto wa Mungu.

Niliwaalika, yeye na mke wake, kuomba ili wampokee Kristo, ndivyo walivyofanya. Baadaye, niliomba kwa ajili ya uponyaji wake. Maisha yake yalibadilishwa na kwa mda mchache, aligawanya Habari njema pamoja na jamaa lake.

Wakati waganga walipomfanyia vipimo, walishangaa kuona uvimbe wake ulipona ! Rafiki yangu huyo alikuwa mtu wa amani.

Alionyesha kuwa hivo kupitiya namna alivyo kubali, wakati nilipompendekeza kuomba. Alihakikisha kama alikuwa mtu wa amani kwa kiu chake cha kujuwa mambo ya Mungu na utashi wake wa kugawanya Habari njema pamoja na wengine.

Tunapata watu wa amani kupitiya maombi. Niliitwa kwa ajili yake wakati nikishiriki kusanyiko la maombi pamoja na wengine wapandaji wa makanisa. Jibu lao kwa ombi la kufanya maombi mara nyingi ni alama ya kiu cha kiroho. Tunapata watu wa amani kwa kugawa injili. Watu wa amani walitayarishwa na Mungu kuwa na kiu ya Habari njema ; wanaonyesha kiu hicho kwa namna wanavyoitikia.

Watu wa amani wanatangaza Habari njema waliyosikia kwa jamaa na rafiki zao.

Wanaonyesha wajumbe wa injili kwa ndugu zao. Wanaunganisha wajumbe wa injili pamoja na rafiki zao, jirani zao na wanamemba wa jamaa zao. Watu wa amani ni chombo ambacho Mungu anatumikisha ili kueneza Habari njema kwa watu wengi. Anafanya hivo sababu hapendi hata moja apotee, bali wote waifikie toba.

Wakati tunapata watu wa amani, tunafurahi sababu tunaona na kuamini kwamba injili inaweza kutawanyishwa haraka!

Naweye Je! Uko na hadisi ao umekutana na kijana, mwanaume ao mwanamuke aliye na kiu ya Mungu ? Uko na hadisi wala umekutana na mtu wa amani aliye kubali uwepo, kwa maombi yako na kwa kutangaza kwako injili ? Kama jibu ni ndiyo, endelea kutafuta na kupata watu wengine wa amani. Kama sivyo, omba Mungu akuongoze kuelekea kwenye watu aliyowatarisha kuwa watu wa amani. Wakati wataweka tumaini lao kwa Kristo, uwafundishe kutii kwa kila agizo la Yesu.

Uwasaidiye kuwaleta watu walio kandokando yao kwa Yesu.

Ilikuwa ''ongezeka'', na mimi Dean Davis. ''nawauliza ni kwa wanani mutagawanya nao leo neno hili la kutiya moyo ?''

SIMULIA HADISI YAKO - MAISHA YAKO MBELE YA KUKUTANA NA KRISTO

 












Jambo ! Karibu kwenye ''ongezeka'', ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo wachungaji, wapandaji wa makanisa na viongozi wa Kikristo.

Mimi ni muhamasishaji wenu Daneille Snowden.

Katika mpango wa mafunzo ya wapandaji wa makanisa ndani ya vijiji vipya, tunafunzwa kutumikisha kibweta cha vyombo vya mpandaji, ambayo inaitwa pia " chombo 4-1-1". Kibweta hiki cha vyombo kinapendekeza swali ine kwenye karatasi moja.

Swali la kwanza ni : "sababu gani ?"

Kwakulijibu, tunagunduwa utambulisho wetu katika Kristo, huku tukifahamu kuwa tuko hai ndani yake, Zaidi ya hayo, utambulisho huo katika Kristo, tunagunduwa pia tuko mawakili, sababu kwa kugawanya upendo wake, tunageuzwa kuchukuwa sura yake (2Wakorintho 5:17-21)

Leo, tunachukuwa swali lingine, ambalo limeulizwa mbali kidogo katika kibweta cha vyombo vya mpandaji : "Nitasema nini ?" Inahusu kugawanya ushuhuda wa sekonde 15 (hadisi yetu) kwa yale aliyoyafanya Yesu kwa ajili yetu.

Wengi miongoni mwetu tunajuwa kama tunaanza mara kwa mara kwa kusema :"ilifikia kwa wakati mwengine ndani ya maisha yangu ... " Tunasimusilia hadisi kutokana na Roho Mtakatifu, hadisi yetu binafsi, hadisi ambayo msomaji  anahisi kushikamana nayo. Ni hadisi ya maisha yetu mbele ya kukutana na Kristo kuwa Bwana na Mwokozi.

Unakumbuka kipindi kile ambacho maisha yako uliyaona kuwa bure, wakati ulijisikia ukiwa bure moyoni mwako ? Gawanya hiyo hadisi !

Ninakumbuka kipindi cha mwanzo wakati nikitangaza injili, nilikuwa nikiingia nyumba kwa nyumba ili kutangaza injili, ao nilikuwa nikiongea na watu barabarani. Nilikuwa na woga sana ! Ijapokuwa, wakati moja kuna mtu ambaye niliongea naye alifikia kuniambia matatizo zake, Roho Mtakatifu alifunguwa roho na moyo wangu ili niweze kugawa TUMAINI iliyotokana na ushuhuda wangu binafsi ! Hadisi yangu ilitokea rohoni, roho iliyobadiiishwa na kuwekwa huru na Yesu-Kristo. Na wakati nilipokuwa nikisimulia hadisi yangu, Neno la Mungu liliinua utaji ili watu hawa waweze kuona hata kujihisi upendo na nguvu za Mungu kwao binafsi.

Simulia hadisi, sema juu ya maisha yako mbele ya kukutana na Kristo ! Inashauriwa kuchukuwa hadisi fupi za sekunde 15 kwenye karatasi.

Uwe tayari ! Maandiki yanatuambia :

"Mwe tayari siku zote kumjibu kila mtu awaulizaye habari za tumaini lililo ndani yenu; lakini kwa upole na kwa hofu." 

(1Petro 3:15)

Ilikuwa ''ongezeka''. Usishite kugawanya podikasti hii.

Tukutane kwenye Facebook, Youtube na kwenye mtandao wetu vcpencouragement.org.

Jumatano, 25 Machi 2026

MIFANO YA KIBIBLIA KUHUSU WATU WA AMANI

 










     Jambo kwa wote, naitwa Dean Davis, na tazama ''ongezeka'' ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa katika vijiji.

Wakati nilipoanza kupanda makanisa katika miaka ya 1980, nilikuwa bado kusikia neno  ''mtu wa amani'', hata na rafiki zangu nao pia. Tulijifunza Luka 10:1-10, pale ambapo Bwana wetu Yesu anafundisha wamitume wake 72 kutafuta watu wa amani.

Lakini, hatukuwai kusisitiza juu ya fundisho kubwa linalohusu kifungu hiki;

Kuko wanaume na wanawake, kwa eneo nyingi, waliyo tayarishwa na Mungu ili wapokee injili na kuwapokea wale wanaotangaza Habari njema. Mutafute hawa wanaume na hawa wanawake. Mukae pamoja nao wakati wote munao tangaza ufalme wa Mungu.

Moja ya hadisi za Biblia zinazovutia zaidi zinazohusu mtu wa amani, ni ile inayohadisia kukutana kwa Yesu na mwanamuke Msamaria kwenye kisima. (Yohana 4:1-43). Yesu alikutana na mwanamuke Msamaria aliyekuwa na sifa mbaya. Lakini alikuwa na kiu ya kumjuwa Mungu. Wakati aliposikia Habari njema, alitangaza habari kwa mji wote. Bwana wetu Yesu alibaki siku mbili pamoja na waamini wa Samaria mbele ya kuendelea na huduma yake Galilaya.

Baada ya ufufuko wa Yesu na ujio wa Roho Mtakatifu kwa wanaume na wanawake waliokusanyika kwenye mzunguuko wa ndani, wamitume walikawia kufanya mafundisho ya kutafuta watu wa amani. Hakika, waliendelesha kanisa lao pa Yerusalemu na wakatangaza Habari njema ya ufalme wa Mungu. Lakini wamitume hawakutafuta watu wa amani inje ya mji. Ilibidi miujiza mingi itendeke ili hiyo ifanyike.

Petro alimpata mtu wa amani aitwaye Kornelio. Hadisi ya kukutana kwao inapatikana katika Matendo ya Mitume, sura 10. Kornelio alikuwa kasisi wa jeshi la kirumi. Kupitiya ujuzi wake, petro hakupenda kabisa kushirikiana na Warumi.

Lakini Mungu alimuelewesha kiwazi katika ndoto kwamba angestahili kwenda kumuona Kornelio. Akampata mtu mwenye sifa njema, aliye na kiu ya kumjuwa Mungu. Kornelio alikusanya majirani na rafiki zake ili wasikie mafundisho ya Petro. Wakati Petro akihadisia hadisi ya Yesu na kueleza unabii wa Agano la kale kumuhusu, Roho Mtakatifu akawashukia hata na kwa wapagni ! Petro akabatiza walio amini na kubaki nao kwa mda wa siku chache.

Mumeona njia ? Mungu anatayarisha watu kupokea injili. Anawapa kiu ya kumjuwa. Waamini wanapokea ujumbe wa Yesu, ujumbe wa mpango kabambi wa Mungu ili kuokowa ulimwengu ulio vunjika. Wakati watu wa amani wanasikia Habari njema, wanaipokea. Wanakuwa na kiu ya kuijuwa zaidi. Hawachungi injili kwa ajili yao wenyewe ; wana alika rafiki zao kuisikiliza. Waamini wanao tangaza Habari njema wanabaki na waamini wapya kwa kujenga imani yao. Kuko watu wa amani ambao Mungu anataka mukutane nao. Kuko watu wanao ishi karibu yenu na wako na kiu ya kumjuwa Mungu. Muwaombee. Muwatafute. Muombe pamoja nao. Mugawe Habari njema pamoja nao. Mubakiye nao. Muwaambiye kuhusu Yesu kwa majirani na rafiki zao.

Ndiyo ! Kuko watu wa amani ambao Mungu anataka mukutane nao.

Ilikuwa ''ongezeka'', na mimi Dean Davis, nawauliza ni pamoja na wanani utagawanya nao leo neno hili la kutiya moyo ?

MIVIRINGO TATU AJILI YA KUWAFANYA WANAFUNZI

  Jambo kwa wote, naitwa Dean Davis, na tazama ''ongezeka'', ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa mak...