Jambo kwa wote, naitwa Dean Davis na tazama ''ongezeka'', ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa katika vijiji.
Tunajuwa kama wazo Z inamaanisha kuanzia Ku mwisho. Tunaelewa pia kuwa ''wazo Z'' inamaana kuwazia kwa upekee kwa mambo ya baadaye ambayo Mungu alitayarishia ulimwengu. Tunawazia hivo ili kujiunga kwa Mungu, kama wafanyakazi pamoja na Kristo, ili kutekeleza mipango yake duniani. Tunajuwa kwamba Mungu hapendi hata moja apotee, bali wote waifikie toba. Mungu ni mvumilivu kwetu. Ndiyo maana bado Yesu hajarudi duniani. Ni kutokana na upendo wa uvumilivu wa Mungu, hukumu ya mwisho haijakuwa (2Petro 3:4-10). Tofauti na hayo, Mungu anaita watu wote, mahali pote, kutubu na kuamini Habari njema (Matendo ya Mitume 17:30-31). Lakini jukumu langu ni nini katika huu mpango? Najuwa kama Mungu iko na mpango kwa ajili ya dunia nzima, sasa ni mpango wake gani kwa mji, mkowa, idara langu, ao Taifa langu ?
Wanafunzi wengi waaminifu, wanao muheshimu Kristo, walijiuliza swali hili la muhimu. Pengine nawe pia. Kaka na dada, naweza kuwaakikishia kuwa, Mungu iko na mpango mkubwa kwa ajili ya ulimwengu, na anaitekeleza polepole Ila kwa uangalifu. Lakini iko na mpango gani kwa eneo ambako naishi ? Rafiki yangu, mpango wa Mungu kwa ajili ya mkowa ambamo unaishi ndani ni ule ule mpango wa Mungu kwa dunia nzima. Mungu anapenda kuwa watu wote wa mkowa wako wasikie na kuelewa habari njema. Anapenda kwamba kila mwanaume na kila mwanamuke, kila kijana na kila binti wa mkowa wako ajuwe Habari njema, atubu na kuweka tumaini lake kwa Kristo. Anapenda kama sote tufahamu neema yake ya wokovu ya mabadiliko ndani ya kanisa.
Ni namna gani sasa tunastahili kuomba? Maombi yetu yatasaidiwa na wazo Z. Tunapashwa kuomba kama vile Kristo alivyo tuamuru: "ufalme wako uje, mapenzi yako yafanyike hapa duniani kama mbinguni.'' (Mathayo 6:10). Tunastahili kuomba ili wapandaji wa makanisa na waamini wa makanisa wapande kanisa katika kila Kijiji cha mkowa. Tunastahili kutembea kwa maombi na kuhimiza waombaji, tukiwasaidia kuchaguwa wazo Z. Tuombe tukichunga moyoni mwetu mpango wa Mungu. Tutatumika namna gani ? Tunapashwa kutumika tukihakikisha kwamba makanisa safi yanajizidisha kwa haraka katika mkowa wetu, ili kwamba mipango ya Mungu itekelezwe duniani, yatekelezwe karibu yetu, miongoni mwa watu wanaosema lugha yetu na wanaoishi kandokando yetu. Ni nani tutamtuma? Tunapashwa kutuma watumishi, wengi katika mkowa wetu hadi mwisho wa dunia. Tunapashwa kutuma watu wanaojuwa roho ya Mungu, watu wenye juhudi kutumika na kuomba kufuatana na wazo Z. Tunapashwa kutuma watumishi waliyo jiandaa kutangaza habari njema ya Yesu, kufanya wanafunzi na kupanda makanisa safi yanayokomaa. Kaka na dada, tuchaguwe wazo Z katika yote tunayotenda, tukiwa na uaminifu kwa Mungu kwa ajili ya utawala wake ujao na ili kwamba mapenzi yake yafanyike duniani kama mbinguni.
Ilikuwa "Ongezeka" na mimi Dean Davis.
Nawauliza : "ni pamoja na wanani utagawanya nao leo neno hili la kutiya moyo ?

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni