Jumatano, 4 Machi 2026

WAZO Z MPANGO WA MUNGU JUU YA ULIMWENGU

 










     Jambo kwa wote, naitwa Dean Davis, na tazama "ongezeka", ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa katika vijiji.

Watu wengi walisema :"anza ukifikiria mwisho kichwani." Wajengaji wanaanza na mwisho kichwani mwao wakati wanapojenga nyumba.

Ata mbele ya kuondowa udongo sababu ya kujenga msingi wa nyumba mpya, mjengaji hodari anajuwa urefu na upana bitakuwa namna gani.

Anajuwa hesabu ya vyumba atakuwa navyo na nyumba itakuwa na urefu gani.

Mbele ya kuweka jiwe la kwanza la msingi, iko tayari rohoni mwake na picha ya namna itakavyokuwa nyumba ikimalizika kujengwa.

Wajengaji wenye hekima wanaanza na mwisho kichwani mwao. Yote wanayojenga, kuanza msingi hadi dari, yanawekwa tayari ili kufikia lengo lao la mwisho : "nyumba nzuri."

Ninyi kama wapandaji wa makanisa, nanyi pia mungestahili kuanza na mwisho kichwani.

Mungeuliza Bwana : "kanisa hili litakuwa la namna gani? Bwana, namna gani tutakuabudu? Tutatumikisha lugha gani?

Namna gani tutatowa injili? Tutafanya namna gani ili kufundisha wanafunzi ? Bwana, ni kwa namna gani kanisa hili litaonyesha upendo wako kwa jirani zetu?"

Kama wajengaji wa nyumba, wapandaji wa makanisa wanapashwa kuwa na picha ya wazi ya namna kanisa litakuwa. Na mpango huo utatoka kwa Mungu.

Lakini haitoshi kuwa tu na mpango mzuri kwa hiyo, ni kwa neema ya Mungu, ndivyo kanisa letu litakuwa.

Tunamtumikia Mungu aliye hai. Na iko na mpango kuhusu dunia yetu. Anajuwa anachokipenda, na alituambia kile anachokipenda kuhusu ulimwengu:

Hapendi hata moja apotee, bali wote waifikie toba (2Petro 3:9).

Anasema kwamba ujuzi wa utukufu wa Bwana utaijaza inchi, kama maji iijazavyo Bahari (Habakuki 2:14)

Anatayarisha siku ambayo mkutano mkubwa sana ambao hapana mtu awezaye kuuhesabu, watu wa kila taifa, na kabila, na jamaa, na lugha, wamesimama mbele ya kile kiti cha enzi, na mbele za Mwana-Kondoo, wata muabudu (Ufunuo 7:9).

Ndivyo Mungu anavyopenda, na tungestahili kupenda hivo pia.

Herufi ya mwisho ya Alfabeti ya kirumi ni Z, inayoitwa Zed _ ao, kama inavyoitwa katika inchi yangu, Zii. Wakati tunapoanza na mwisho kichwani, tunatumia wazo Z. Wazo Z inamaanisha kwamba tunatarajia mda ujao ambao Mungu anatarajia sisi tujiunge kwake ili kutumika ili kwamba malengo yake yageuke kwa matendo.

Katika upandaji wa makanisa katika vijiji, maono yetu ni kuwa na kanisa katika kila Kijiji cha Afrika ifikapo mwaka wa 2050.

Waundaji wa VCP walikubali maono hayo sababu walipendelea kukubaliana na mpango wa Mungu kwa ajili ya uumbaji wake.

Walijuwa kama Mungu anapenda inchi ijae ujuzi wa utukufu wa Bwana, kama vile maji iijazavyo Bahari.

Walijuwa kama Mungu hapendi hata moja apotee, bali wote waifikie toba. Walijuwa kama ni mapenzi ya Mungu, ambaye sisi tunamhubiri habari zake tukimwonya kila mtu, na kumfundisha kila mtu katika hekima yote, tupate kumleta kila mtu mtimilifu katika Kristo. (Wakolosai 1:28).

Ndiyo maana walichaguwa kumjulisha Kristo kwa kupanda makanisa katika vijiji ambavyo hakuna makanisa. Walitumikisha wazo Z. Mbele ya yote, walielewa mapenzi ya Mungu kwa uumbaji wake. Baadaye, walichaguwa kujiunga kwake ili kutekeleza maono yake ya mwisho.

Wewe pia, uko miongoni mwa VCP. Nategemea kwamba utaambatana na maono haya ya kuwa na kanisa katika kila Kijiji cha Afrika ifikapo mwaka wa 2050. Funga macho yako kwa mda mchache na ufikirie kanisa katika kila Kijiji. Fikiria hivo kwa uwazi, ili maono yageuke kuwa matendo. Kisha usimame na ufanye yanayokuhusu ili kuiweka katika vitendo!

Ilikuwa "ongezeka", na mimi ni Dean Davis, nawauliza : " ni pamoja na wanani utagawanya nao leo neno hili la kutiya moyo ?

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

MIVIRINGO TATU AJILI YA KUWAFANYA WANAFUNZI

  Jambo kwa wote, naitwa Dean Davis, na tazama ''ongezeka'', ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa mak...