Jumatano, 18 Juni 2025

SIKILIZA RIPOTI ZA WANAFUNZI WAKO


       Hamjambo nyote, naitwa Dean Davis, na  tazama ''ongezeka'' ni podikasti inayoleta neno la kutia moyo kwa wapandaji wa makanisa katika vijiji. Ikiwa umekuwa ukipanda na kuzidisha makanisa kwa zaidi ya miaka mitatu au minne, umechukua majukumu muhimu. Kwa mwanzo, unaweza kuwa ulilenga katika kuomba mitaani, kutafuta watu wa amani, na kushiriki Habari Njema katika nyumba na vikundi vya nyumbani. Lakini sasa, majukumu yako yamekua. Unatumia muda mwingi kutoa maono, kufunza wengine, kuandaa matukio, na kusimamia upandaji wa makanisa mengi katika maeneo mbalimbali. Pengine unahisi kuondolewa kidogo kutoka kwa furaha na msisimko wa uinjilisti wa moja kwa moja na ufuasi wa waumini wapya. Umechukua madaraka makubwa zaidi, na wale walio karibu yako wanashukuru kwa kazi unayofanya, lakini ukweli ni kwamba, umeondolewa kidogo kutoka kwenye eneo la kukomaa kwa Ufalme. 

Katika nyakati kama hizi, lazima uwe macho. Linda moyo wako. Hakikisha huruma yako kwa waliopotea haipungui. Linda moyo wako. Hakikisha unamwamini Mungu kila siku kwa ajili ya riziki, hekima, nguvu, kibali, na neema. Linda moyo wako, uwe macho msijisifu kwa nguvu zenu wenyewe; mtukuzeni Bwana, rehema zake, na wema wake. Unapopanda makanisa zaidi na zaidi na kugawa majukumu zaidi na zaidi kwa wanafunzi wako, njia moja ya kulinda moyo wako ni kusikiliza kwa makini ripoti za wanafunzi wako. Yesu alifanya hivi. Alipowatuma mitume katika huduma yao, alisikiliza ripoti zao waliporudi.

 Mathayo 9:10 inatuambia, “Wale mitume waliporudi walimweleza Yesu yote waliyoyafanya. Kama unavyojua, kusikiliza sio kusikia tu. Kusikiliza ni kuwa makini. Kusikiliza ni kutafuta kuelewa. Yesu alisikiliza ripoti za wanafunzi wake, nasi ni lazima tufanye vivyo hivyo. Lazima tuwaache waseme hadithi zao kwa maneno yao wenyewe. Lazima tuulize maswali ya wazi ili kuongeza kuelewa kwetu na wao. Ni lazima tuwe na subira wanapozungumza. Kwa kufanya hivyo, tunaonyesha heshima kwa wanaume na wanawake hawa wenye bidii ambao wanajaribiwa katika huduma yao ya kufanya wanafunzi na kupanda makanisa. Tunapata maarifa na kuelewa katika hali halisi ambazo hatujapata.

Tunapata hekima ya muhimu ili kuwashindikiza wanafunzi wetu vizuri. Na wanafunzi wetu wenyewe wanafaidika kwa hekima na kufikiria kwa uzoefu wao wa huduma.


Sasa, mufanye kama vile Yesu. Mchukuwe mda wa kusikia ripoti za wanafunzi wenu, mkifanya hivo, pande zote mbili mtapokea nguvu. Mukisikiliza kwa makini, roho zenu zitaunganishwa. Mungu atatukuzwa na mtakuwa timu iliyo nguvu. Kwa kusikia, Bwana atawaongoza pamoja mbali zaidi, na kuwa na imani zaidi, ya hekima na maoni.


Ilikuwa Ongezeka na mimi Dean Davis nawauliza, ni pamoja na wanani utagawanya nao leo neno hili la kutiya moyo ?

UONGOZI WA MUWAKILI - UONGOZI WA MUWAKILI


    Tazama Chuck Rapp na ongezeka, ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa na kwa viongozi wakikristo.

Leo, tunaendelea na mfululizo wetu juu ya uongozi wa Muwakili, na tunamaliza somo letu la mfano wa Muwakili dhalimu.

Muwakali anatafsiriwa kama ''mtu anayesimamia rasilimali alizopewa na mtu mwengine ili kufikia malengo ya mwenye mali''. Katika mazingira yetu, tunaongoza rasilimali tulizopewa na Bwana kwa ajili ya kazi yetu ya upandaji wa makanisa katika vijiji.

Katika podikasti zangu za nyuma. Nilionyesha Mada tatu za msingi za mfano huu:

Mawakili wanastahili kutowa ripoti.

Ujanja wa Muwakili na sifa alizopokea kwa bwana wake.

Umuhimu mkubwa wa uaminifu katika mambo madogo kama vile ndani ya rasilimali.

Shurti muhimu ambayo Yesu anajaribu kututolea hapa ni kwamba inafaa kuwa Muwakili mwaminifu. Usizoofike na sifa anazozipokea Muwakili dhalimu - tulijadili swali hili katika kipindi cha nyuma. Muwakili dhalimu alichukuwa rasilimali za bwana wake kama njia ya kujibia maitaji yake na kujiendelesha mwenyewe. Yesu, kwake yeye, anapendelea wafuasi wake wawe waaminifu na wenye haki katika usimamizi wao wa rasilimali.

Yesu anaeleza katika vesi 10 na 11 :

''Aliye mwaminifu katika lililo dogo sana, huwa mwaminifu katika lililo kubwa pia; na aliye dhalimu katika lililo dogo, huwa dhalimu katika lililo kubwa pia.

Basi, kama ninyi hamkuwa waaminifu katika mali ya udhalimu, ni nani atakayewapa amana mali ya kweli?''

Hii inanikumbusha somo letu la mfano wa Talanta katika Mathayo 25.

Tukiwa waaminifu katika mambo madogo, kwa hiyo tunaweza kukabiziwa mengi. Na kama hatuwezi kuwa waaminifu katika mambo ya dunia - yasiyo yetu hata kwa mwanzo, namna gani Mungu anaweza tukabizi ''utajiri wa kweli'' wa Ufalme wake?

Neno kubwa ya utashi wa Yesu uko kwenye vesi ya 13 :

''Hakuna mtumishi awezaye kutumikia mabwana wawili; kwa maana, ama atamchukia huyu na kumpenda huyu, ama atashikamana na huyu na kumdharau huyu. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali.''

(Angalia pia Mathayo 6:24)

Kama Mungu ndiye Bwana wetu, kwa hiyo sasa, rasilimali zetu, mda wetu, vipaji vyetu na pesa zetu vitakuwa kwa ajili yake.

Muwakali mwaminifu na mwenye haki, ambaye Bwana wake ni Mungu, ataweka vyote alivyo, na vyote anavyofanya kwa kazi ya kujenga Ufalme wa Mungu.

Kwa mwisho, wanaopenda pesa kuliko Mungu, ambao wanatafuta tu kulipwa ao kutajirika, hawaweki Ufalme wa Mungu katikati ya vipaumbele vyao.

Katika podikasti yetu ijayo, tutaendelea na somo letu kuhusu uongozi wa Muwakili.

Ilikuwa neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa na kwa viongozi wakikristo.

UONGOZI WA MUWAKILI - Mfano wa Muwakili dhalimu. Sehemu 2



     Mimi niChuck Rapp na ''Ongezeka'' ni podikasti iliyoundwa ili kuleta neno la kutia moyo kwa wapandaji wa makanisa na kwa viongozi. 

Leo, tunaendelea na mfululizo wetu kuhusu uongozi wa uwakili (au uongozi wa usimamizi). Mwandishi mmoja anafafanua muwakili kuwa "mtu anayesimamia rasilimali za mtu mwingine ili kufikia malengo ya mwenye mali''. 

Katika mazingira yetu, tunasimamia rasilimali zinazotolewa na Bwana kwa ajili ya kazi yetu ya upandaji wa makanisa  katika vijiji.

 Katika podikasti yangu ya mbele niliwasilisha mada tatu ninazoziona katika mfano huu: Wasimamizi lazima wawajibike. Ujanja wa msimamizi wa nyumba na sifa alizopokea kutoka kwa bwana wake. Umuhimu wa uaminifu, katika mambo madogo na katika usimamizi wetu wa kipesa. Katika kipindi hiki, tunajadili ujanja wa msimamizi na sifa alizopokea kutoka kwa bwana wake. Tunasoma katika mstari wa 8: “Yule bwana alimsifu yule msimamizi asiye mwaminifu kwa sababu alikuwa ametenda kwa busara. Hii ina maana gani? Mfano huu unaonekana, kwa njia nyingi, kuwa mgumu kuelewa. Kwa nini mtu tajiri, bwana wake, amsifu mtumishi aliyefuja mali yake kisha akampunguzia madeni ya wengine?

Ufunguo wa kuelewa hadithi ya Yesu ni kwamba haihusu mahusiano ya bwana na mtumishi. Badala yake, ni kuhusu njia sahihi ya kusimamia pesa. Kando ya haraka: Inatokea kwangu kwamba matendo ya msimamizi asiye mwaminifu yaliwafanya wengine wajiunge naye katika ukosefu wake wa uaminifu. Usimamizi wetu mwaminifu, au kushindwa kufanya hivyo, kunaathiri wengine. Katika kuzingatia kwa nini bwana alimsifu msimamizi asiye mwaminifu, lazima kwanza tuelewe kwamba hakuwa akisifu ukosefu wake wa uaminifu. Alimsifu kwa sababu alitambua jinsi msimamizi huyu alikuwa ametumia (au kutumia vibaya) ufikiaji wake wa rasilimali ili kujiandaa kwa uamuzi wake unaokuja na kulinda maisha yake ya baadaye. Mistari ya 8 na 9 inapanua wazo hii: "Kwani watu wa dunia hii ni werevu zaidi katika kushughulika na aina zao kuliko watu wa nuru." Lakini mimi nawaambia, tumieni mali za ulimwengu huu usio wa haki ili kujifanyia marafiki, ili, zitakapowapungukia, wapate kuwakaribisha katika makao ya milele." Kanuni moja tunayoweza kupata kutoka kwa maneno haya ni kwamba Yesu anatuhimiza tuwe wakarimu kwa mali zetu za kidunia, ili kuendeleza Injili na kufanya marafiki kwa umilele. Hii inapatana na mafundisho juu ya utajiri kwa mahubiri yake kwenye mlima, pale ambako Yesu aliwasihi wanafunzi wake kuwekea utajiri wao mbinguni (Mathayo 6:19-21).


Tukielewa kwamba kila kitu tulichonacho ni zawadi kutoka kwa Mungu, hapo ndipo tutakapokubali  kama Mungu ndiye mwenye vyote  halisi na Sisi ni waangalizi. Ikiwa hivo, tunastahili kutumikisha rasilimali za Bwana ili kuendelesha malengo na shabaa za Bwana.


Katika kipindi chetu cha kufuata,  tutaendelea na somo letu kuhusu uongozi wa usimamizi na mfano wa Muwakili dhalimu.

Ilikuwa neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa na kwa viongozi wakikristo katika vijiji.

Wape Wanafunzi wako Majukumu Makubwa


       Jambo kwa naitwa Dean Davis, na tazama ''ongezeka'' ni podikasti inayoleta neno la kutia moyo kwa wapandaji wa makanisa katika vijiji. Kukabidhi majukumu ya huduma ni sehemu muhimu ya uongozi wa kanisa. Na pia ni muhimu katika mchakato wa kufanya wanafunzi. Chukua muda sasa kujibu maswali haya mawili rahisi: Ninapofanya kazi na wanafunzi wangu, je, mara nyingi mimi huwapa majukumu ambayo ni makubwa sana kwao? Au, je, ninawapa majukumu rahisi sana, yanayoweza kudhibitiwa? Unaweza kusitisha podikasti hii ili kufikiria hili ukipenda. 

Maswali haya mawili ni muhimu sana. Ikiwa tunawapa wanafunzi wetu majukumu ambayo ni makubwa sana kubeba, wanaweza kuvunjika moyo. Ikiwa hawajui la kufanya au jinsi ya kufanya, mambo yataenda vibaya. Hata kama wanajua la kufanya na jinsi ya kulifanya, lakini hawana wakati wa kukamilisha kile ambacho umewauliza, hii inaweza kusababisha matatizo makubwa. Kwa upande mwingine, wakati mwingine wafuasi wako, wako tayari kufanya mambo makubwa na kuchukua majukumu mazito. Lakini ikiwa hutambui uwezo na nia yao, mambo yanaweza pia kwenda vibaya. Watafadhaika, na wanaweza kuanza kujitilia shaka, na pengine hata kukuacha utafute mahali ambapo karama zao na ujuzi wao vitatumika vyema katika Ufalme wa Mungu.

 Kwa hiyo, tunapaswa kufuata miongozo gani tunapowakabidhi wanafunzi wetu madaraka?

 Hapa kuna kanuni tano zinazonisaidia sana: 1. Onyesha maono makubwa. 
2. Kuwa mwangalifu kwa uwezo, vipawa na ujuzi wa wanafunzi wako.
3. Wape majukumu yanayowasogeza mbele kidogo. 
4. Thibitisha mara kwa mara kile wanachofanya vizuri. 
5. Wasaidie kwa subira kujifunza kutokana na makosa yao ili wawe na nguvu zaidi wakati ujao.


Maono ya VCP: kanisa katika kila kijiji cha Kiafrika ifikapo 2050, ni maono makubwa na yenye matarajio makubwa. Ndivyo ilivyo Agizo Kuu: kufanya wanafunzi wa mataifa yote. Shiriki maono haya mara kwa mara na kwa uwazi. Kisha, ukikumbuka karama na uwezo wa wanafunzi wako, wape majukumu ya maana ambayo yanawapa changamoto ya kuomba, kujinyoosha, na kutafuta masuluhisho ya busara. 

Daima thibitisha kile ambacho kimefanywa vizuri. Warekebishe kwa upole na uwaelekeze ili wawe na ujuzi zaidi wakati ujao. Ndugu yangu, dada yangu, fuata mfano wa Yesu: wape wanafunzi wako majukumu ya maana. Ukifanya hivyo, utabarikiwa, watabarikiwa, na neema ya Mungu itaonekana kwa namna ya kushangaza !

Ilikuwa ''Ongezeka'', na mimi ni Dean Davis, nawauliza ni pamoja na wanani utagawanya nao leo neno hili la kutiya moyo ?

Jumanne, 10 Juni 2025

UONGOZI WA MUWAKILI - Mfano wa Muwakili dhalimu. Sehemu 1


      Tazama Chuck Rapp na ongezeka, ni podikasti inayoleta neno la kutia moyo kwa wapandaji wa makanisa na viongozi wa Kikristo katika vijiji.

 Leo, tunaendelea na mfululizo wetu wa uongozi wa uwakili. Mwandishi mmoja anafafanua muwakili kuwa "mtu anayesimamia rasilimali za mtu mwingine ili kufikia malengo ya menye mali." 

Katika mazi'gira yetu, tunasimamia rasilimali zinazotolewa na Bwana kwa kazi yetu ya upandaji makanisa katika vijiji.

 Mfano wa msimamizi dhalimu unapatikana katika Luka 16:1-13. Ninakuhimiza utulie na uisome. Kwa mtazamo wa kwanza, hadithi hii inaweza kuonekana kuwa ya kutatanisha. Kwa nini bwana wa nyumba angemsifu msimamizi-nyumba asiye mwadilifu kwa kutenda kwa busara? (Tutashugulikia swali hili katika sehemu yangu inayofuata. Katika podikasti hii na mbili zifuatazo, tutachunguza mada tatu ninazoona katika hadithi hii:

 - Wasimamizi lazima wawajibike. 

- Utambuzi wa msimamizi na sifa kutoka kwa bwana wake. 

- Umuhimu wa uaminifu katika mambo madogo na katika kusimamia fedha. Kwa kuanzia, nazani ni muhimu kwamba mfano huu unafuata mara moja ule wa mwana mpotevu aliyetapanya mali ya babake. 

Ni lazima pia tufikirie mazi'gira ya fundisho hili: 

Yesu anazungumza na wanafunzi wake na Mafarisayo, viongozi wa kidini wa wakati huo. (Tunaona hili mwanzoni mwa sura ya 15.Tunasoma yafuatayo katika sura ya 16, mstari wa 1 na 2 : “Palikuwa na mtu mmoja tajiri ambaye msimamizi wake alishitakiwa kwa kutapanya mali yake. Anamtolea hesabu msimamizi wa nyumba asiye mwadilifu ambaye aliona mali za bwana wake kuwa njia ya kujifurahisha na kujiletea maendeleo. Mstari wa 1 unasema "alipoteza" rasilimali za tajiri. Baadhi ya tafsiri zinasema "alizitapanya". Msingi ni kwamba Baba yetu anatuomba tuwe mawakili waaminifu. 

Yesu anataka wafuasi wake wawe wasimamizi wa nyumba wenye haki na waadilifu. Hebu tuangalie tena wasikilizaji wa Yesu. Anawakemea kwa kutosimamia ipasavyo baraka na majukumu yanayowapata wakiwa wateule wa Mungu. Wasikilizaji wengine walikuwa wanafunzi wake (ona mstari wa 1), ambao sisi ni sehemu yao leo. Ikiwa tunaelewa kanuni kwamba kila kitu tulicho nacho ni zawadi kutoka kwa Mungu, tunatambua kwamba Mungu ndiye mmiliki wa vyote tulivyo tulivyo navyo, na kwamba sisi ni mawakili wake. Kwa hivyo, lazima tutumie rasilimali za Mwalimu kufikia malengo ya Mwalimu''.

Katika kipindi chetu cha kufuata, tutaendelea na somo letu kuhusu uongozi wa Muwakili, kwa kutafakari utambizi wake.

Ilikuwa neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa na kwa viongozi wa kikristo katika vijiji.

UONGOZI WA MUWAKILI - Mfano wa Mtini usiozaa matunda






 







Tazama Chuck Rapp na ongezeka, ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa na kwa viongozi wakikristo katika vijiji.

Katika mwaka huu mpya, nilianzisha mtiririko mpya kuhusu Mada ya uongozi wa Mawakili. Mwandishi moja anatafsiri Mwakili ''kama ni mtu anayeongoza rasilimali alizopewa na mtu mwengine ili kufikia malengo ya mwenye mali'' katika mazingira yetu, tunaongoza rasilimali tulizopewa na Bwana kwa ajili ya kazi yetu ya upandaji wa makanisa katika vijiji.

Kifungu chetu katika podikasti ya leo ni Luka 13:6-9.

Yesu akahadisia hadisi hii: ''Akanena mfano huu; Mtu mmoja alikuwa na mtini umepandwa katika shamba lake la mizabibu; akaenda akitafuta matunda juu yake, asipate. 

Akamwambia mtunzaji wa shamba la mizabibu, Tazama, miaka mitatu hii naja nikitafuta matunda juu ya mtini huu, nisipate kitu; uukate, mbona hata nchi unaiharibu? 

Akajibu akamwambia, Bwana, uuache mwaka huu nao, hata niupalilie, niutilie samadi; 

 nao ukizaa matunda baadaye, vema! La, usipozaa, ndipo uukate''. 

Kwa kuanza kujifunza mfano huu, kitu cha kwanza nilicho jiuliza, ni '' ni myaka ngapi inayo chukuwa Mtini ili kuzaa matunda?''. Hii inaonekana kuwa swali lenye busara, kwa sasa, nimefanya utafiti wa haraka kwenye mtandao na nilipata mitandao mingi iliyoonyesha kwamba Mtini unazaa matunda baada ya myaka 3 ao 4.

Ni kweli! Muumba wa ulimwengu haijui hayo? (Tuone wakolosai 1:16)

Ninachotaka kusema hapa ni kwamba, ''mtu'' wa mfano wetu - anaye wakilisha Mungu - anangojea kwetu sisi kuzaa matunda kwa mda uliyopangwa. Na kwetu pia ni hivo ; anasubiri kwetu pamoja na huduma yetu - tuzae matunda wakati tunapofikia kiwango cha kukomaa wakati matunda yanasubiriwa.

Tulinganishe mazingira ambayo Mtini uliishi. Ulikuwa umepandwa kwenye udongo mzuri wa mzabibu. Jua na mvua vilikueko. Baada ya mwaka wa tatu, mtengenezaji wa divai alichimba Shimo kandokando ya mti na kuweka mbolea. Mti ulifaidika na mazingira yote yanayostahili kwa kuzaa matunda. Tazama mafundisho maalm ya huu mfano.

- Mungu anangojea matunda kwa mda unaotakika ; alitowa yote yafaayo ili kwamba matunda yazaliwe.

- uvumilivu na neema yake vinatoa mda zaidi kwa kuzaa, na anatutendea sote kwa namna moja

- kwa mwisho, kuko kuwajibika kwa ukosefu wa matunda.

Namaliza kwa ukumbusho wa 2Petro 1:3. ''Kwa kuwa uweza wake wa Uungu umetukirimia vitu vyote vipasavyo uzima na utauwa, kwa kumjua yeye aliyetuita kwa utukufu wake na wema wake mwenyewe''.

Katika kipindi chetu cha kufuata, tutaendelea na somo letu juu ya uongozi wa Mawakili.

Ilikuwa neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa na viongozi wakikristo katika vijiji.

Kufundisha kwa utuwema na huruma


    Jambo kwa wote, Naitwa Dean Davis na tazama ''ongezeka'' ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa katika vijiji.

Kwa siku hizi za mwisho, ndani ya vipindi hivi, tulichambuwa mada zinazo ambatana na Mada ya ongezeka. Tulikumbusha kwamba njia moja tu ya kutekeleza maoni ya VCP - kanisa moja katika kila Kijiji cha Afika ifikapo mwaka wa 2050 - ni kwa njia ya ongezeka. 

Sababu tunapenda Mungu na tunataka kutekeleza Agizo kubwa ya kuwafanya mataifa yote kuwa wanafunzi na kwa mahali pote. Tunayo imani katika ongezeka. Roho ya upandaji wa makanisa katika vijiji, VCP ni ongezeko la wanafunzi, waviongozi na makanisa.

Kama tunapendelea kuongeza wanafunzi na viongozi, tunastahili kufanya vizuri zaidi tu ya kuwafundisha mawazo mapya. Tunastahili kuwapa fursa ya kutenda. Kutowa namna, ni kupana nguvu, uwezo na mamlaka. Viongozi wa kikristo wenye busara wanajuwa kama kuko namna nyingi ya kufikia hapo.

Tunatowa uwezo kwa wengine kwa kuwashauri (kuwafundisha) kupitiya mashauri na kwa kuwakilisha majukumu na mamlaka.

Namna ingine ya muhimu ya kuwaacha wengine huru ni mafundisho. Yesu alitowa uwezo kwa wanafunzi wake kwa kuwafundisha : aliwafundisha Ufalme wa Mungu, na kufanya huduma kwa wengine.

Lakini, kwa bahati mbaya, mafundisho yote hayana ndani yake uwezo. Watu wamoja wanafundisha tu sababu wanapendelea kusikilizwa wakisema mawazo ya muhimu.

Wengine wanafundisha sababu wanapenda kupata heshima inayopewa Mwalimu. Wengine wanafundisha sababu wanafurahia vile watu wanakaa kimya wakiwasikiliza. Alafu, waalimu wanaofundisha kwa lengo la kusifiwa ao kuheshimika mara nyingi hawatowe sana uwezo kwa wanafunzi wao.

Sasa, ni hatuwa ao tabia gani za waalimu wanaotowa uwezo kwa wengine?

Namna Mwalimu anastahili kufundisha wakati anatarajia kudumisha na kuwafanya wanafunzi wake wawe na ujuzi wa kuongoza? Huduma ya Yesu inatupatiya jibu nzuri kwa swali hili. Mafundisho ya Yesu yalijaa huruma. Mafundisho yake hayakuwa rahisi kuyaelewa, sababu yalijaa utuwema.

Mathayo 4:23 inatuambia:

''Naye alikuwa akizunguka katika Galilaya yote, akifundisha katika masinagogi yao, na kuihubiri Habari Njema ya ufalme, na kuponya ugonjwa na udhaifu wa kila namna katika watu''

Yesu alionyesha huruma yake kwa kuchukuwa miaka tatu kwa kutayarisha wanafunzi wake kwa majukumu yaliyo makubwa zaidi. Aliwatuma wanafunzi wake kazini na kusikiliza ripoti zao wanaporudi. Yesu alionyesha tendo la uvumilivu kwa wanafunzi wake. Kamwe hakuwaacha wenyewe, hata wakati walikuwa na uzaifu wa kujifunza na kuelewa.

Je! Na weye? Wanafunzi wako wangekuonyesha wewe kama mtu aliye na uvumilivu na utuwema?

Wakati unapofundisha, unachukuwa mda wa kusikia? Wanafunzi wako wangesema kama unawapa mda na unatafuta kuwaelewa? Wanajuwa kama unawaaminia na unasubiri kuwaona wakitekeleza mambo makubwa? Mwalimu wako anajaa utuwema na huruma ?

Kama ni hivo, msifu Bwana na uendelee na kazi yako nzuri. Lakini ukijisikia kwamba ndani mwako unakosa huruma, chukuwa wakati leo hii kumwambia Bwana. Umwambiye kama unasikitika kwa ukosefu wako wa uvumilivu mbele ya wanafunzi wako na ukosefu wako wa utuwema.

Uwe mwangalifu. Omba kwa unyenyekevu kwa Bwana akujaze na huruma kwa wale unaowafundisha. Umwambiye kama unapendelea sana kuwapa namna ya kuishi kama wanafunzi.

Bwana atajibu kwa ombi lako, kama anavyosema Yakobo 4:6:

''Lakini hutujalia sisi neema iliyozidi; kwa hiyo husema, Mungu huwapinga wajikuzao, bali huwapa neema wanyenyekevu.''

Mimi ni Dean Davis, nawauliza ni pamoja na wanani utagawanya nao leo neno hili la kutiya moyo ?

UONGOZI WA MUWAKILI - Mfano wa Talanta - Sehemu ya 3



Tazama Chuck Rapp na ongezeka, ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa na kwa viongozi wakikristo katika vijiji.

Kwa mwanzo huu wa mwaka, nilianzisha mtiririko mpya kuhusu Mada ya uongozi wa Mawakili.

Mwandishi moja anatafsiri Mwakili kama ''mtu anaye ongoza rasilimali alizopewa na mtu mwengine ili kufikia malengo za mwenye mali''.

Leo, tunaendelea mafunzo yetu ya mfano wa Talanta, unaopatikana katika Mathayo 25 :14-30.

Katika vipindi viwili vilivyopita, tulijifunza kanuni saba ambazo zilitolewa katika hadisi hiyo.

Ningependelea kufafanuwa mambo mamoja ambayo hatuoni katika mfano huo wa Yesu.

Kwa kuanza, napendelea kuwapasha alama moja ya muhimu saana.

Wasimamizi Mawakili wanaongoza kwa unyenyekevu.

Tazama baadhi ya maoni ambayo hatuyaoini kwa Mwakili aliye tangulia na Talanta 5 na akamaliza na Talanta 11.

- hakumuamakia wala kumutukana Mtumishi aliye tumika vibaya na Talanta yake moja. Mwakili ''mwaminifu'' alimwachia mwenye mali hatua ya kumtangaza ''mbaya, mvivu na asiye na maana''. Kama wanadamu, mara nyingi tunajaribiwa kwa kuhukumu wengine, na tunastahili kuwa waangalifu kwa jambo hilo. Tunastahili kumwachia Mungu na wale wenye madaraka kujihusisha na Wale wasiojibu kwa ukamilifu kwa yanayotarajiwa.

- jambo la pili, hatukuona Mtumishi aliye na Talanta 11 kufurahia yule aliye na 4. Pengine utakumbuka kama nilivyosema katika podikasti yangu ya nyuma, Mtumishi aliye pokea mifuko tano na ule aliyepokea mifuko mbili walisifiwa sawasawa na bwana wao. Ni vema, Mtumishi mwema na mwaminifu kwa mambo madogo ; nitakupa vitu vingi. Njoo tuchangia mema ya bwana wako. Nakazia tena unastahili kuepuka mtego wa kujilinganisha na wengine.

- kwa mwisho, nafurahia Mtumishi aliye na Talanta 10. Siyo mda wa kujisifia (tunayaona mara nyingi kwa wajezaji) kwa kujihusisha na umimi. Chukulia hii mifano ya Yesu katika Luka 17:10. ''Vivyo hivyo nanyi, mtakapokwisha kuyafanya yote mliyoagizwa, semeni, Sisi tu watumwa wasio na faida; tumefanya tu yaliyotupasa kufanya''. 

Hakuna nafasi ya kujiinuwa ndani ya mifano hii ya Yesu.

Hata kama Mtumishi aliye maliza na Talanta 11 alisifiwa na mwenye mali, alibaki tu Mtumishi.

Sisi kama wasimamizi Mawakili, tunapashwa kuonyesha mwenendo wa upole, kwa kutekeleza kila siku kwamba yote tuliyo nayo, na vyote tulivyo, ni vya mwenye mali, Bwana Yesu-Kristo.

Katika toleo letu la kufuata, tutaendelea na mafunzo yetu kuhusu uongozi wa Mawakili.

Ilikuwa neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa na kwa viongozi wakikristo katika vijiji.

MIVIRINGO TATU AJILI YA KUWAFANYA WANAFUNZI

  Jambo kwa wote, naitwa Dean Davis, na tazama ''ongezeka'', ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa mak...