Jumatano, 11 Desemba 2024

KUTEMBEA KWA ROHO


 





Karibu kwenye ''ongezeka'', podikasti ya kuwahimiza wapandaji wa makanisa katika vijijini, wachungaji na viongozi wa Kikristo. Mimi ni mwenyeji wako leo, Daneille Snowden. 

Katika Yohana 16:7 tunasoma - YESU ALISEMA, NI KWA FAIDA YETU NIENDE. Anasema nini? Faida katika Kigiriki ina maana ya kufaidika na kupata ambayo ni faida. Aina hii ya faida ni juu na zaidi ya kawaida yoyote. Moja ya faida zinazotolewa na Roho Mtakatifu kuja juu na ndani yetu ni: Tutafika kwenye UTIMILIFU wa…: Ufahamu na Hekima.


Huu ni ufahamu wa kina wa Neno la Mungu na kusudi lake. Akiwa na Nguvu Zake na karama Zake zisizo na mwisho ili kutuandaa maishani. Kuna msemwa inayosema: “Kazi ya Mungu ndani yetu (ukamilifu) ni kazi ya Roho Mtakatifu. Kazi ya Mungu kupitia sisi (utimilifu) pia ni kazi ya Roho Mtakatifu.” (F. Hartly) Tutafika kwenye UKAMILIFU: (HUO NDIO UTIMILIFU). Utimilifu huu wa Roho Mtakatifu akitujaza na nguvu na karama zake utatuweka huru kutokana na mapungufu yetu (ndani ya mawazo yetu wenyewe). Hivyo ndivyo Paulo alivyoweza kusema: “Nina pigano lililo njema, nami nimeIimaliza mwendo wangu na kuilinda imani.”

 2 Timotheo 4:7 Nimejifunza haya ndani ya mume wangu Brad na maisha yangu katika huduma na maisha ya kila siku kumebadilisha kweli tunaona sisi ni nani katika Ufalme wa Mungu. Tumetumikia katika huduma kwa jumla ya miaka 35, na 26 tukiwa wachungaji. Miaka 6 iliyopita ya uchungaji, Brad alikuwa kwenye kiti cha magurudumu, na hakupewa muda mrefu wa kuishi. Kisha Mungu akamponya na sasa tunatembea katika maisha kama wamisionari. Mada yetu ambayo Mungu alitupa ilitoka katika Wafilipi 1:6 “Nikiliamini sana neno hili, ya kwamba yeye aliyeanza kazi njema ndani yenu mtaifanya hata siku ya Kristo Yesu; UKAMILIFU huo ni UTIMILIFU! Utimilifu huu hutokea wakati Kristo anatiririka kupitia kwetu hadi kwa wengine. Na ni endelevu KWA ROHO! Kama ilivyoandikwa katika Zakaria 4:6: Ndipo akaniambia, Hili ndilo neno la Bwana kwa Zerubabeli, si kwa uwezo, wala si kwa nguvu, bali ni kwa Roho yangu, asema Bwana wa majeshi. Asante kwa kusikiliza, je, utashiriki podikasti hii na wengine?

ALAMA MAHUSUSI KWA VIONGOZI WA MUNGU. Nehemia - Mwaminifu kwa Bwana.

 








Mimi ni Chuck Rapp na ongezeka, ni podikasti ya kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa na viongozi wa makanisa.

Leo tunaendelea na mfululizo wetu juu ya sifa za uongozi za Nehemia. Kuna mengi tunaweza kujifunza - na kutafuta kufuata - kutoka kwa mtu huyu. Wiki chache zilizopita, tulijifunza katika sura ya 2 jinsi Nehemia alivyokuwa kiongozi mwenye mpango na jinsi, alipowasili Yerusalemu, alifikiria hali ya kuta. Muda mfupi baada ya ukaguzi wake wa usiku wa kuta alianza kupata upinzani. Katika hatua hii ya hadithi ya Sanbalati na Tobia wanaanza kuingilia kati na majaribio yao ya kuvuruga kazi na kuwakatisha tamaa wafanyakazi. Katika mstari wa 19 na 20, tunasoma “Lakini Sanbalati, Mhoroni, na Tobia, Mwamoni, na Geshemu, Mwarabu, waliposikia habari hiyo, walitusumbuwa na kutudhihaki. "Ni nini hiki unachofanya?" waliuliza. "Je, unaasi dhidi ya mfalme?" Nikawajibu kwa kusema, Mungu wa mbinguni atatufanikisha. Ninaona masomo mawili muhimu sana ya uongozi katika mistari hii. • Kwanza, karibu kila wakati tunapofanya kazi kutoka kwa Bwana kutakuwa na upinzani. Wakati mwingine upinzani huo utakuwa kutoka kwa watu walio nje ya kundi letu kama vile katika swala hili. Lakini wakati mwingine upinzani utatoka kwa wale ambao tunafikiri wako upande wetu. Binafsi, hiyo ndiyo hali yenye changamoto zaidi kwangu. Ninaita hii "moto wa kirafiki." Nakumbuka mgawo wetu wa kwanza wa misheni karibu miaka 30 iliyopita. Wengi wa wafanyakazi wenzangu walitafuta kutusaidia (mimi na mke wangu) kupata mahali petu, lakini wachache walionekana kutaka kutuweka mahali petu. Hilo lilituumiza sana lakini tulijua kwamba Mungu alikuwa ametuita. Tatizo ni kwamba, viongozi lazima wawe tayari kwa upinzani; ikiwa Bwana ana wito

ikiwa Bwana ametuita, ni lazima tuwe watiifu na kuendelea. • Pili, Nehemia alikuwa kiongozi mwenye kujiamini. Hata hivyo, imani yake haikujitegemea yeye mwenyewe au wale walio karibu naye. Badala yake, alijibu, “Mungu wa mbinguni atatufanikisha.” Ona kwamba Nehemia hakujibu ili kujitetea alipodhihakiwa na wapinzani. Hakuwaonyesha sifa zake. Hakushiriki katika vita vya maneno; aliepuka jibu la hasira kwa wale waliompinga. Naomba tuige mfano huu! Daudi, katika Zaburi 20:7-8, alikuwa na haya ya kusema, “Hawa wanatumainia magari na wengine farasi, bali sisi tunalitumainia jina la BWANA, Mungu wetu. Wanapigwa magoti na kuanguka, lakini sisi huinuka na kusimama imara.” Na tusimame imara, tusimame kwa ujasiri, kwa sababu ya tumaini letu kwa Bwana! 

Ilikuwa neno la kutia moyo kwa Wapandaji wa makanisa na viongozi wa Kijiji.

ALAMA MAHUSUSI KWA VIONGOZI WA MUNGU. Nehemia - Hekima ya kusawazisha kazi na usalama

 








Tazama Chuck Rapp na Ongezeka, podikasti ya kutoa neno la kutia moyo kwa wapandaji wa makanisa katika vijijini na viongozi. Leo tunaendelea na mfululizo wetu kuhusu sifa za uongozi za Nehemia. Kuna mengi tunaweza kujifunza - na kutafuta kufuata - kutoka kwa mtu huyu. Sura ya 4 inatanguliza upinzani kutoka kwa Sanbalati, Tobia na wengine. Ninashukuru jibu la Nehemia katika 4:9. “Lakini tulisali kwa Mungu wetu na kuweka mlinzi mchana na usiku ili kukabiliana na tishio hilo.” Sisi, kama Nehemia, lazima kwanza tumtumaini Mungu na kisha tufanye sehemu yetu pia. Viongozi wa VCP na wapandaji wa makanisa wanakabiliwa na upinzani kutoka mambo mengi … dini nyingine, viongozi wa mitaa au serikali, wakati mwingine hata viongozi wa kanisa. Katika kukabiliana na changamoto hizo, ni lazima tuombe, tumtumainie Mungu, na kisha kutambua na kutii kile ambacho Roho Mtakatifu anatuagiza kufanya. Ninathamini maagizo ambayo Nehemia alitoa katika 4:16-17. "Kuanzia siku hiyo na kuendelea, nusu walikuwa na mikuki, ngao, pinde na silaha ... Wale waliobeba vifaa walifanya kazi yao kwa mkono mmoja na kushikilia silaha kwa mwingine." 

Ni picha nzuri kama nini ya mfanyakazi wa kiroho! Tunafanya kazi kwa mkono mmoja huku tukiwa na silaha za vita vya kiroho kwa mkono mwingine. Andiko la Waefeso 6:10-18 linatupatia maagizo mazuri sana tunapojitayarisha kushiriki katika vita vya kiroho. Ninaona katika kifungu hiki kwamba Nehemia alikuwa na hekima ya uongozi kusawazisha uharaka wa kukamilisha kazi na usalama wa wafanyakazi. VCP inakabiliwa na changamoto hii katika maeneo kadhaa ambapo tunafanya kazi. Kwa hakika, baadhi ya makanisa yaliyoanzishwa na VCP yameshambuliwa na kuharibiwa, na viongozi wachache wa kanisa wamepoteza maisha yao kwa mashambulizi ya kimwili. Tafadhali ungana nami katika kumuombea Mkurugenzi Claude na wengine ambao lazima wapate hekima ya Mungu ili kuepuka kuwaweka wafanyakazi wetu kwenye hatari isivyo lazima huku pia tukijitahidi kukamilisha maono ya kuanzisha kanisa katika kila kijiji cha Kiafrika kufikia 2050. Ninavutiwa na ujasiri wa wanaume na wanawake hawa wa kawaida waliofanya kazi ya kujenga upya kuta za Yerusalemu.

 Mungu awape ujasiri kama huo wafanyakazi wetu wa VCP. Mwisho, ningependa kutaja sifa moja ya ziada ya kiongozi ambayo ninaiona katika sura hii ya ine. 4:18b inatuambia kwamba “Yule mtu aliyepiga tarumbeta alikaa pamoja nami.” 4:20a, “Popote mtakaposikia sauti ya tarumbeta, jiunge nasi huko.” Viongozi wanawajibika kwa maonyo na mawasiliano. Ezekieli 33:6-7 na Hosea 8:1 ni maandiko mawili kati ya mengi yanayoelezea wajibu wa viongozi kupiga kengele au kutoa onyo kwa watu. Wakati mwingine ujumbe huu ni mgumu na haupokelewi vizuri. Hata hivyo, tunapaswa ‘kusema kweli kwa upendo. ( Waefeso 4:15 ) Tunatozwa hesabu ikiwa tutakosa kufanya hivyo. 

Ilikuwa neno la kutia moyo kwa Wapandaji wa makanisa na viongozi wa vijiji.

MIVIRINGO TATU AJILI YA KUWAFANYA WANAFUNZI

  Jambo kwa wote, naitwa Dean Davis, na tazama ''ongezeka'', ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa mak...