Jumanne, 24 Machi 2026

MTU WA AMANI NI NANI ?


 











Karibu kwenye ''ongezeka'', ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji na wasimamizi wa makanisa. 

Mimi ni Brad Snowden, na leo, napendelea kuzungumzia kifungu cha maandiki cha muhimu.

Luka 10:5-6 "[5]Na nyumba yo yote mtakayoingia, semeni kwanza, Amani iwemo nyumbani humu; 

[6]na akiwamo mwana wa amani, amani yenu itamkalia; la, hayumo, amani yenu itarudi kwenu. 

Kifungu hiki kinaonyesha vizuri sana , maana ya kukutana na ''mtu wa amani'' kwa kufika kwa Kijiji kipya. Ni muhimu kukutana na watu wenye moyo mwema na walio wazi, sababu ukarimu wao unakuza  mahusiano ya kina. Wakati mtu anakupokea, ana mwelekeo zaidi wa kuwa msikivu na tayari kwa kusikia ushuhuda wako. Ufunguzi huu unaruhusu Mungu kuanza kazi yake ndani ya maisha yao, kisha ndani ya jamaa zao, na kwa mwisho kutoa fursa kwa Kijiji chote kusikia Habari njema ya Yesu -Kristo.

Baba yangu mukwe alipenda kuhadisia hadisi moja ya wakati 

Kampuni za kukata miti zilielea miti juu ya mito. Mara nyingi, gogo lilikwama kwenye mwamba au kisiki, na kuzuwia bingine byote. Alizowea kuiita ''gogo fungulo '', alikuwa akisema kwamba wachungaji, maana yake wapandaji wa makanisa, ni wale ambao wangestahili kutafuta hili ''gogo fungulo '' na kulifanyia kazi ili kulifunguwa, na kuruhusu hivo wengine wote kushuka juu ya mto bila msongamano. Kwa namna hii, mtu wa amani anaweza kuwa kama hili gogo fungulo : 

mtu ambaye ushawishi wake unaweza kubadilisha mazingira ya kijiji kizima.

Mara nyingi katika utafutaji wetu wa matokeo ya kuvutia, tunasahau mtu huyo wa muhimu anayefanya kila kitu kiwezekane. Mtu wa amani ni muhimu zaidi ili kazi ya Mungu ifanyike ;  tuombe ili Bwana atayarishe roho hizo ziweze kupokea wapandaji wa makanisa. Ni Roho Mtakatifu peke yake tu, anaweza tayarisha roho na mioyo ya wale waliochaguliwa kwa kazi hiyo, kwa nafasi nzuri na kwa mda mzuri. Mtu wa amani ni yule anayefungula mlango wa kiroho kwa Kijiji na kandokando.

Tuombe Bwana wa mavuno atufunulie ni akina nani hao ''watu wa amani'' katika kila jamii na namna gani anatarajia kuwatumikisha.

Ujumbe huu ulikuwa chimbuko la kutiya moyo wasimamizi wa upandaji wa makanisa katika vijiji 

Ni pamoja na wanani utagawanya nao leo ?

Mungu awabariki sana.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

MIVIRINGO TATU AJILI YA KUWAFANYA WANAFUNZI

  Jambo kwa wote, naitwa Dean Davis, na tazama ''ongezeka'', ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa mak...