Jumatano, 4 Machi 2026

KWA NINI KUPANDA MAKANISA?

 









    Jambo kwa wote, naitwa Dean Davis, na tazama ''ongezeka'' ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa katika vijiji.

Wamoja walisema : "hakuna amri ndani ya Biblia inayo tu amuru kupanda makanisa. Sababu gani kupoteza nguvu na wakati katika upandaji wa makanisa ?"

Hakikisha ambayo inasema kwa wazi hakuna amri ya Biblia : "Enendeni mukapande makanisa !" Ni kweli. Lakini hakikisho hiyo inadanganya. Wakati Mitume waliposikia amri ya Yesu inayosemwa katika Mathayo 28:19-20, iliyotolewa wakati alipopaa, mbele kidogo ya Pentekoste, waliweka neno lake katika vitendo kwa kupanda makanisa. Walipanda kanisa lao la kwanza pa Yerusalemu. Baadaye, kuanza hapo, waliendelea na upandaji wa makanisa katika Uyahudi, Samaria na mwisho wa dunia, vile vile kama alivyo amuri.

Wakati tunapopanda makanisa, tunafuata mfano wa Mitume wa Yesu.

Amri kubwa inapata msingi wake katika Agizo kuu : mpende Mungu na umpende jirani yako. Wito wa Yesu wa kumpenda jirani yako kama nafsi yako mwenyewe ni msingi wa mafundisho ya wanafunzi kupitiya upandaji wa makanisa. Roho ya wapandaji wengi wa makanisa inajaa upendo kwa wale wasio bado kumjuwa Kristo. Mfano wako uko je?

Tunapanda makanisa sababu upendo wa Mungu unatushurutisha. Tunapendelea wengi, siyo wachache, wapatane na Mungu. Wawe na uzoefu wa maisha tele ndani ya Kristo, wajuwe Mchungaji Mwema, waishi na uhakikisho na tumaini tele. Ndiyo sababu tunapanda makanisa.

Tunatarajia pia kwa mabadiliko, kwa ukombozi, kwa amani na maelewano. Tunajuwa kama Mungu pekee anaweza leta ukombozi.

Tunajuwa kama Yesu peke yake anaweza kujibu maitaji makubwa ya jirani zetu. Lakini tunajuwa pia kwamba jamii ni wazo kutoka kwa Mungu na iko miongoni mwa mpango wake mkubwa wa kubariki dunia. Alimuongoza Adamu kwenye baraka wakati aliposema : "si vema huyu mtu awe peke yake." Hiyo inaambatana bila shaka na ndoa, lakini pia kwa mitindo mingine ya jamii, kama kanisa.

Tunapanda makanisa sababu tunapenda baraka, wakati wanafunzi wa Yesu wanajiunga pamoja kwa imani, wakati wanapo kusanyika kwa wazo moja, wakati wanajinyenyekesha pamoja kwa Uungu wa Kristo. Watu wengi katika Bara la Afrika, Esia, Ulaya na Marekani, wanao onja ushirika wa ndugu na itaji la kuwa ndani ya kanisa takatifu, wanasela : "sijawai bado kuona upendo kama huu ndani ya jamaa yangu. Kanisa hili ni baraka za ajabu kwangu!" Kwa hiyo, tunapanda makanisa sababu tunapenda watu wawe na uzoefu wa jamii la kweli, mahali ambako wanatembea nuruni, kama Yesu alivyo nuruni, na mahali wanapoishi ushirika uletao uzima.

Sababu gani tunapanda makanisa ? Haya yote ni swali la upendo. Tunafuata mfano wa Yesu, aliyetupenda na kujitowa mwenyewe kwa ajili yetu. Unapoanza kupanda makanisa, usiache. Hata kama ulisha panda makanisa mingi, usiache. Upandaji wa makanisa, ni upendo katika vitendo.

Ilikuwa "Ongezeka" na mimi Dean Davis, nawauliza ni pamoja na wanani utagawanya nao neno hili la kutiya moyo ?


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

MIVIRINGO TATU AJILI YA KUWAFANYA WANAFUNZI

  Jambo kwa wote, naitwa Dean Davis, na tazama ''ongezeka'', ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa mak...