Jambo na karibu kwenye ''ongezeka'', ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji na viongozi wa makanisa katika vijiji, wachungaji na viongozi wakikristo.
Mimi ni muhamasishaji wenu Daneille Snowden. Nafurahia kugawanaya nanyi leo, ao kukazia maono ambayo Mungu ametowa kwa One Mission Society kwa ajili ya upandaji wa makanisa katika vijiji ; kupanda kanisa katika kila Kijiji cha Afrika ifikapo mwaka wa 2050. Ni maono makubwa sana ambayo tumepewa na Bwana wetu Yesu mwenyewe, wakati aliposema :"Enendeni, mkawafanye mataifa kuwa wanafunzi wangu... '' (Mathayo 28.19-20). Mimi na mume wangu tuligunduwa upandaji wa makanisa katika vijiji pa Mozambique.
Usomi na shuhuda tulizo zisikia zilitugusa sana. Zaidi ya mwaka moja baadaye, Mungu alituita kutumika kama wamisheni ndani ya huduma ya CMF kwenye vuguvugu hili kubwa.
Tukiwa wanafunzi wa Yesu-Kristo, tunafuata mfana wake, kama inavyosemwa katika Mathayo 9:35 :"Naye Yesu alikuwa akizunguka katika miji yote na vijiji, akifundisha katika masinagogi yao, na kuihubiri habari njema ya ufalme, na kuponya magonjwa yote na udhaifu wa kila aina.''
Yesu alikuwa akizunguka katika miji na vijiji ! Wengine watajiuliza pengine wapi wataanzia kulingana na kazi hii iliyo kubwa mno. Jibu ni rahisi : kufuata Yesu, kutafuta uwepo wake, kungojea ukiwa ndani, na zaidi, kufuata mfano wake. Kwa hiyo, tunapashwa kuwa waangalifu sana na kuelewa vizuri Agizo kubwa. Pamoja na maono, Mungu anatupa mpango ! VCP inatuonyesha mfano wa Shamba ine, mpango uliyo ndondolewa ukieleza namna gani kuingia kwenye maono haya.
Shamba la 1 ni sehemu zabiti ya mpango ; inahusisha maombi mengi, hata na maombi ukiwa ukitembea ukiwa na ramani na Biblia ; vyombo viwili kwa ajili ya kuendelesha maono.
William Carey, Mmisheni wa karne ya XVIIIe, aliandika :"kwa kujuwa mapenzi ya Mungu, tunaitaji Biblia na ramani vilivyo funguliwa ''. Ninawaalika leo kuchunga sana maono haya iliyo rohoni mwako, na moyoni mwako na nafsini mwako.
Habakuki 2:2 inatuambia : ''BWANA akanijibu, akasema, Iandike njozi ukaifanye iwe wazi sana katika vibao, ili aisomaye apate kuisoma kama maji.''
Tujulishe mapenzi ya kweli ya Mungu ya kwamba watu wote waokolewe!
Ilikuwa ''ongezeka''.
Usisahau kugawanya podikasti hii pamoja na kaka na dada ndani ya Kristo na viongozi wenu wakikristo !
Enendeni, mkawafanye wanafunzi !

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni