Tazama Chuck Rapp na ongezeka, ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa na kwa viongozi wakikristo katika vijiji.
Mada yetu katika mwaka wa 2026 ni maendeleo ya Uongozi. Leo natarajia kuanza kwa kuzungumzia mafundisho mamoja ya msingi kuhusu uongozi... Ambayo nawaza ni ya muhimu zaidi wala isiwe ya muhimu.
Kwa miaka 33 iliyopita, nilichaguwa tafsiri ya Uongozi ifuatayo, ambayo nilichangiya na Mwalimu wa shule la juma pili ambaye nilikutana naye kwa miaka yetu iliyopita katika inchi ya Ubeljiji. Alikuwa akionyesha mtazamo wa kijeshi na wa Biblia ya Kikristo wakati alipokuwa akitufundisha juu ya Uongozi.
Uongozi ni uwezo wa kushawishi watu juu ya uaminifu usiogeuka kuhusu amri za Mungu.
_ Jemadari Kanali Gene Klann, OTAN, wa 1993 nafurahia uwazi na upole wa tafsiri hii.
_ uongozi unahusu zaidi ushawishi zidi ya nguvu ao mamlaka.
_ Viongozi wachaMungu hawapashwi kugeuka katika uaminifu wao kwa Mungu. Watu watachaguwa kutokufuata wale walio wanafiki.
_ Msingi wa uongozi wetu unastahili kuwa uwaminifu kwa Neno la Mungu na kwa mafundisho ya Roho - Mtakatifu.
Angalia mtazamo mwengine unaoshikamana vizuri kwa viongozi wanao muheshimu Kristo. Unatokana na Daktari Robert Clinton.
Kiongozi ni mtu aliye na :
Majukumu aliyopewa na Mungu ya kushawishi kundi fulani la watu wa Mungu kwa kusudi ya kutekeleza mipango ya Mungu kwa lile kundi.
Nafurahia uwazi wake.
- uwezo wa kiongozi unatoka kwa Mungu (tutairudilia baadaye kidogo)
- Uongozi ni majukumu tuliyopewa na Bwana Mungu (tutairudilia pia baadaye)
- Uongozi unahusu ushawishi bali siyo woga
- Viongozi wanaongoza makundi za watu kwa lengo ya kufikia mipango ya Mungu , hii inaambatana na mtazamo wetu wa mwaka jana kuhusu kiongozi muwakili kama ''mtu anayeongoza raslimali zilizo za mtu mwengine kwa kusudi ya kufikia malengo ya mwenye mali ''.
Bado ningali na maoni ya kugawanya nanyi leo.
Uongozi ni karama ya kiroho. Katika warumi 12 :8, Paulo anaandika kuhusu karama za kiroho na anadai ya kwamba :''mwenye kuonya, katika kuonya kwake; mwenye kukirimu, kwa moyo mweupe; mwenye kusimamia kwa bidii mwenye kurehemu, kwa furaha.''
Uongozi pia ni wito. Matendo ya Mitime 13:2 inaonyesha uzoefu wa Sauli kwa Barnaba :
''Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile niliyowaitia.''
Watu hawa wawili waliitwa kuwa viongozi ndani ya kanisa la kwanza, na Mungu anaendelea hata leo kuita na kuomba viongozi.
Je! Tunaweza kuwa wazi na kupokea wito kwa karama za Mungu ndani ya maisha yetu.
Je! Tunaweza kuwa waangalifu kwa wale wanaotuzunguka, kwa kuwa waangalifu ili kuchunguza na kufundisha viongozi wapya.
Hii ilikuwa neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa na kwa viongozi wakristo katika vijiji.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni