Alhamisi, 31 Julai 2025

UONGOZI WA MUWAKILI - Tabia inahusika


    Jambo nyote, tazama Chuck Rapp na ongezeka, ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa na viongozi katika vijiji.

Tunaendelea na mfululizo wetu juu ya uongozi wa Muwakili. Leo na katika vipindi vinavyokuja, nitajihusisha kuhusu baadhi ya mada kubwa zinazoshikamana na kuongoza. Tunaanza na ukweli huu: tabia inahusika.

Kwa ukumbusho, muongozi wa rasilimali (ao Muwakili) anatafsiriwa kama ''mtu anayesimamia rasilimali alizopewa na mtu mwengine ili kufikia malengo ya mwenye mali''. Katika mazingira yetu, tunaongoza rasilimali tulizopewa na Bwana kwa ajili ya kazi ya upandaji wa makanisa katika vijiji.

Mutakumbuka pengine kwamba tabia ilikuwa Mada yangu maalm mnamo mwaka wa 2024, wakati tulikuwa tukijifunza tabia za uongozi wa Nehemia. Katika kipindi changu kinachoitwa ''kuwa mwaminifu juu ya mda, niliongea kama Danieli alitumika yapata miaka 66 chini ya uongozi wa wafalme watatu wa Babiloni! Tunagunduwa namna alivyotekeleza hayo katika sura ya 6, vesi ya 4.

[4]Basi mawaziri na maamiri wakatafuta sana kupata sababu za kumshitaki Danieli kwa habari za mambo ya ufalme; lakini hawakuweza kuona sababu wala kosa; kwa maana alikuwa mwaminifu, wala halikuonekana kosa wala hatia ndani yake''.

Ni ushuhuda wa namna gani ! Ni urizi wa namna gani ! Hakuna yeyote yule, hata wapinzani wake hawakupata hata kidogo ya rushwa ndani yake.Alikuwa mwaminifu akiwa Muwakili chini ya uongozi wa wafalme watatu wa Babiloni, na hakuwa na zarau katika utendaji kazi wake. Tujikaze, pamoja na nguvu, upako na kuvikwa Roho Mtakatifu, kuwa kama Danieli.

Kwa mwanzo wa mwaka, tumeanza mtiririko huu kwa mfano wa Talanta katika Mathayo 25.

Mtumishi ambaye alipewa mifuko tano ya feza ''alienda kuchuuza pesa hizo'' (vesi 16).

Mawakili waaminifu wanaonyesha utayari na wanatumika kwa uaminifu kwa kusudi ya kutekeleza kurudi bora kwa Bwana. Mwenendo huu wa unyenyekevu na uaminifu kwa Bwana ni mfano wa kufuatwa.

Tukumbushe pia kwamba mfano wa Mtumishi mwaminifu na hodari, katika Mathayo 24. Kwenye vesi za 46 na 47,

Yesu anafundisha :

[46]Heri mtumwa yule, ambaye bwana wake ajapo atamkuta akifanya hivyo.''

[47]Amin, nawaambieni, atamweka juu ya vitu vyake vyote''.Yesu anafundisha ndani ya mfano wa Talanta kuwa wale wanaomtii Mungu watalipwa. Utii wetu, ambao uko na mizizi ndani ya tabia yetu, ni vya muhimu sana.

Ninamaliza na baadhi ya vesi na maneno juu ya tabia:

Mithali 10.9 :

[9]Aendaye kwa unyofu huenda salama; 

Bali apotoshaye njia zake atajulikana''.

Billy Graham : ''uaminifu inamaanisha kwamba tuko waaminifu, wakuigwa, na usio laumika.''

Mithali. 11.3 : ''Ukamilifu wao wenye haki utawaongoza 

Bali ukaidi wao wenye fitina utawaangamiza.''

Ndiyo, tabia inahusika!

Wakati mwengine, tutaendelea somo letu kuhusu uongozi wa Muwakili.

Ilikuwa neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa katika vijiji na viongozi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

MIVIRINGO TATU AJILI YA KUWAFANYA WANAFUNZI

  Jambo kwa wote, naitwa Dean Davis, na tazama ''ongezeka'', ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa mak...