Jumatatu, 31 Agosti 2026

Saidia watu kujibu kwa hadisi kubwa ya Mungu

 








        Jambo kwa wote, naitwa Dean Davis, na munasikiliza ''ongezeka'', ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa katika vijiji.

Moja ya majukumu ya muhimu zaidi tuliyo nayo sisi kama wapandaji wa makanisa ni kuwa musimuliaji wa hadisi. Kila mutu hapendelei kabisa kujilinganisha kuwa musimuliaji wa hadisi. Ijapokuwa, mbele ya kuwa mwinjilisti, mbele ya kuweza kupanda kanisa, tunapashwa kuwa wasimuliaji wa hadisi.

Wakati Yesu alipoanza huduma ya kuhubiri, kufundisha na kuandaa wanafunzi, alisema : ''tubuni na kuamini Habari Njema.'' Habari Njema ni hadisi ya mpango wa Mungu wa wokovu, uliotekelezwa na Yesu kupitiya mfano wa maisha yake, kifo chake cha msalaba na ufufuko wa ushindi.

Kuko haina nzuri nyingi za kugawanya hadisi hii kubwa ya Mungu inayotendeka duniani. Tunaweza kusimulia mtiririko wa hadisi za kibiblia juu ya uumbaji wa Mungu wa kushangaza kuhusu uhasi wa binadamu zidi ya Mungu, juu ya namna Mungu alivyo chaguwa binadamu, Ibrahimu, ili kurejesha baraka duniani, juu ya uhasi wa binadamu unaoendelea, juu ya itaji lake la kujitowa sadaka na kuungama.

Tunaweza kusimulia hadisi kubwa ya Mungu kwa kuonyesha filamu ya YESU, inayoanza na uumbaji na inamalizika na ahadi ya Mungu kwamba Yesu atarudi. Tunaweza kugawanya Habari Njema kwa kuchora miviringo tatu na kwa kueleza uhasi wetu pia na kushindwa kwetu kuepuka kwa nguvu zetu wenyewe kanuni iliyovunjika ya dunia yetu. Tunaweza kusema juu ya maisha, ya kifo na ufufuko wa Yesu.

Mitindo yote hii ni namna bora ya kugawanya Habari njema, lakini kusimulia tu hadisi hii haitoshe. Tunaweza kusaidia watu kuishi hadisi hii ndani ya maisha yao binafsi ili waweze kugeuzwa kupitiya neema iletayo wokovu ya Mungu.

Munaona, watu wengi wanafikiri kwamba hadisi kubwa ya Mungu inahusu watu wengine. Wanazania kama ni hadisi inayohusu Mungu, Adamu na Hawa, Nuhu na watoto wake, Abrahamu, Isaka na Yakobo. Na wana haki : watu hawa wote wamefanya kazi muhimu ndani ya hadisi ya Mungu.

Lakini kama ukisikia hadisi kubwa ya Mungu kama muhuzuriaji tu wa inje, ukijihusisha tu na watu mashuhuri walio onyeshwa ndani ya hadisi hii, utakuwa umepita kando ya ujumbe muhimu.

Jambo la muhimu katika hadisi ya Mungu ni vile alivyotuma Mwana wake wa pekee aje kufa ajili ya kukuokowa aje kufa ajili ya kuniokowa. Ndiyo, kuko watu wengine wengi ndani ya hadisi hii. Lakini kama bado weye mwenyewe hautajihisi kuwa kama mutu muhimu wa hadisi hii kubwa ya Mungu, hauwezi bubadilishwa.

Siyo tu kujuwa kama Mungu anapenda ulimwengu. Siyo tu kujuwa kama Yesu alikuja kuokowa watenda dhambi. Kile tunastahili kusaidia watu kuelewa, ni kuwa Yesu alikuja kwa ajili yao na kwamba Yesu alikuja kukutana nao.

Kama tunaweza saidia watu kuona nafasi yao ndani ya hadisi hii kubwa ya Mungu, vitu vingi vitatokea.

Wakati watu wanasikia kwa mara yao ya kwanza hadisi kubwa ya Mungu, mwangaza unaanza kujitokeza. Wakati watatambuwa kwambi dhambi yao iliyosababisha Yesu kuja duniani, siku inageuka kuwa na mwangaza zaidi. Wakati wataelewa kwamba Yesu alikufa na kufufuka kwa ajili ya kuwaokowa, mwangaza wa injili unawaka zaidi.

Lakini wakati watu wataelewa ni kwa kutubu na kuamini Habari Njema, wanaweza kusamehewa, kununuliwa na kubadilishwa, hapo sasa mwangaza wa injili unakuwa na utukufu.

Sasa, simulia hadisi kubwa ya Mungu. Uisimuliye vizuri. Isimulie mara nyingi. Isimulie na hadisi, pamoja na filamu, pamoja na taswira.

Isimulie kwa mtu  moja kama vile kwa watu wengi.

Lakini ukumbuke kila siku kitu kimoja : wakati unapo simulia hadisi hii kubwa, wasaidie watu kuelewa kwamba jibu lao kwa upendo wa Mungu ni kama wakifanya hadisi hii iwe yenye kuenea.

Ukifanya hivo, utaona maisha ya watu wengi yakibadilishwa.

Ilikuwa ''ongezeka'', na mimi Dean Davis, nawauliza swali hii : ni kwa nani utagawanya nao neno hili la kutiya moyo ?

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Usikawize ubatizo

  Karibu kwenye ongezeka, ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa, kwa wachungaji na viongozi wa Kikristo. Mimi...