Miviringo tatu zinamtawaza Yesu kama Mfalme. Jambo kwa wote, naitwa Dean Davis, na tazama ''ongezeka'' ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa katika vijiji.
Wakati nilijaribu kwa mara ya kwanza kuelewa Habari Njema ya Yesu, nilisikia kila mara wahubiri na waalimu wakisema kama ''tunastahili kumwamini Yesu''. Nilikuwa nikiona kupitiya shauku yao na marudilio ya msemwa huo, ya kwamba ni muhimu sana ''kumwamini Yesu''. Lakini sikuelewa kabisa nini walimaanisha hapo.
Walitaka kusema kwamba tunastahili kuamini mtu aliyeitwa Yesu aliyeishi imepita sasa miaka 2000? Niliamini hivo, na nilipenda sana yale aliyoyatenda na mafundisho yake.
Walipenda hakika kusema kama Yesu alifufuka kutoka wafu ?
Sikuamini kabisa hayo.
Walipenda, wakati wakihakikisha kama tunastahili kumwamini Yesu, kama tunapashwa kufuata mafundisho yake ? Nilipenda mafundisho yake, lakini sikuwa tayari kuyafuata yote.
Hapo nilikosa msimamo. Waalimu wangu waliniambia kuwa ningestahili kuamini Yesu. Waliniambia pia ningemfanya awe Bwana wa maisha yangu.
Nilijuwa kama yale walioniambia yalikuwa ya muhimu, lakini sikujuwa nifanye nini.
Baadaye siku moja, kupitiya maombi na usomi wa Agano Jipya, niliielewa kwamba hakika Yesu alifufuka kutoka wafu. Nilikubali kwamba ningestahili kumwamini.
Nilistahili kuamini Yesu na kumtii sababu ni mwema, amejaa upendo, na yuko hai.
Na kisha nikaomba hivi :
''Bwana Yesu, ninasikitika kwa namna nimeishi. Tafazali, unisamehe. Nifanye kuwa kiumbe kipya. Nakupokea kama Bwana na Mwokozi wangu. Amen''.
Ombi langu lilikuwa rahisi, lakini lilibadilisha kila kitu. Sasa, nilijuwa kama nilimwamini Yesu. Sio tu niliamini kwamba aliishi, na akafa na akafufuka, lakini nilimwamini. Nilezaliwa upya !
Wakati tunapotangaza injili ya miviringo tatu, tunawaalika watu, ''kugeuka kutoka uasi wao na kumtawaza Yesu kama Mfalme wa maisha yao ''.
Ni kweli, tayari Yesu ni Mfalme. Siku ya Pentekoste, Petro alisema :
''Yesu huyo Mungu alimfufua, na sisi sote tu mashahidi wake.
Basi yeye, akiisha kupandishwa hata mkono wa kuume wa Mungu, na kupokea kwa Baba ile ahadi ya Roho Mtakatifu, amekimwaga kitu hiki mnachokiona sasa na kukisikia.
Maana Daudi hakupanda mbinguni; bali yeye mwenyewe anasema,
Bwana alimwambia Bwana wangu,
Keti upande wa mkono wangu wa kuume.
Hata nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.
Basi nyumba yote ya Israeli na wajue yakini ya kwamba Mungu amemfanya Yesu huyo mliyemsulibisha kuwa Bwana na Kristo.''
Yesu ni Bwana ; Yesu ni Mfalme ! Lakini taifa lake linaasi. Wakati tunapo waomba watu kumtawaza Yesu kama Mfalme wa maisha yao, tunawaomba kuacha uasi zidi ya Mungu na kisha kuweka tumaini lao kwake na kumtii.
Je ! Utachukuwa mda mchache ili kumwambia Yesu kama ni Mfalme wako ?
Kumwambia pia kama unampenda, na kumwamini na unapenda kumufuata ? Acha Roho Mtakatifu aseme nawe wakati unapofanya hivo.
Baadaye, kwa upendo mkubwa na furaha kubwa, alika watu wengine kumtawaza Yesu kama Mfalme wa maisha yao.
Ilikuwa ''ongezeka'' na mimi Dean Davis, nawauliza : ni pamoja na wanani utagawanya nao leo neno hili la kutiya moyo ?

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni