Ijumaa, 24 Julai 2026

MIVIRINGO TATU NA TOBA

 










        Jambo kwa wote, naitwa Dean Davis, na tazama ''ongezeka'', ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa katika vijiji.

Wakati nilipoanza kuelewa Habari Njema ya Yesu, nilipenda kusikia ujumbe kuhusu ''maisha tele''. Moja ya vesi za Biblia za kwanza nilizo kariri,  ilikuwa Yohana 10:10;

Biblia

''Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele.''

Nilipendelea maisha tele, maisha inayojaa isia za matumaini.

Lakini ilikuwa kama watu wote walio tangaza injili pamoja nami walikuwa wakinieleza kuwa ningestahili kuachana na dhambi zangu na kuweka tumaini langu kwa Kristo. Basi ningejaribu kuishi maisha tele.

Shida, nilipendelea kuishi maisha tele bila toba.

Nakumbuka kwamba turu nyingi, Muhubiri alisema kuhusu baraka ya kuwa mwana wa Mungu. Ujumbe hizi zilileta matumaini ndani yangu, lakini baadaye alitamka neno hili :"tubuni.'' nilisikia woga moyoni mwangu.

Kwa mwisho, nilitubu. Nilimwambia Mungu kama nasikitikia namna ya maisha yangu mabaya ya kuishi. Nilimwambia kama napenda kuachana na dhambi zangu. Nilimuomba Yesu kunisamee. Ndipo wakati huo maisha tele ndani yangu yalianza.

Nilikua na amani pamoja na Mungu. Nilijuwa kama nilikuwa mtoto wake. Wakati nilikuwa nikisoma Biblia, niliielewa. Maneno yaliyokuwa yakitoka kinywani mwangu yalibadilika, hata pia na namna nilivyokuwa nikiwatenda marafiki zangu. Nilizaliwa upya.

Moja ya sehemu nzuri ya kutangaza injili ya miviringo tatu ni mkuki unaoelekea kwenye dunia iliyovunjika kuelekea mviringo wa chini, hiyo inayosimulia hadisi ya maisha, ya kifo na kufufuka kwa Yesu.

Mkuki huu unamaanisha toba.

Wakati tunapo tangaza miviringo tatu, tunasema :"ukitubu dhambi zako na kumtawaza Yesu kama Mfalme wa maisha yako, na atakupatanisha na Mungu.''

Hii inamaanisha kama ukiachana na uasi wako zidi ya Mungu na kuweka tumaini lako kwa Kristo, Mungu atakusamehe na atakupa maisha tele.

Watu wengi wanashangaa kama Mungu anakubali kutupokea mara tena baada ya sisi kumuasi. Na ni ajabu kweli. Lakini kilicho cha ajabu zaidi, ni kwamba Mungu anatupa neema na nguvu yakutosha kwa sisi kutubu.

Kwa ajili ya upendo wa Mungu, tunaweza kubadilika. Hatushurutishwi kuendelea kuishi maisha hayo hayo mabaya tuliyoyaishi wakati tulipokuwa waasi zidi ya Mungu. Tunaweza kuachana na ubaya, uzalimu na dhambi.

Tunaweza kuanza kuishi maisha ya haki, yenye kujaa upendo kama tukiweka tumaini letu kwa Yesu.

Sasa, wakati unapotangaza injili ya miviringo tatu, chora mkuki huu kwa kuonyesha mwisho wa uasi na kumrudilia Mungu. Ambia watu kama wanaweza kutubu, wanaweza kubadilika, wanaweza kuachana na mabaya na kumuelekea Mungu. Wajulishe kama anafurahi kutupatia nguvu inayotustahili ili tumtumainie na kumtii.

Maisha ya Kikristo ya toba na imani ni kitu kizuri.

Nashukuru sana vile nilivyo tubu ; na ninaomba ili kwamba mamia, hata maelfu ya watu watubu na kuweka tumaini lao kwa Kristo. Wakati unapo tangaza Habari Njema kwa kuchora miviringo tatu na kusimulia hadisi kubwa ya Mungu.

Ilikuwa ''ongezeka'' na mimi Dean Davis, nawauliza ni pamoja na wanani utagawanya nao leo neno hili la kutiya moyo ?

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Kutumika kwa mda wa sasa. Kuomba kwa ajili ya wakati ujao

      Jambo kwa wote. Naitwa Dean Davis, na munasikiliza ''ongezeka'', ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapand...