Ijumaa, 24 Julai 2026

MIVIRINGO TATU MUNGU HUINGILIA KATI

 









     Jambo kaka na dada. Naitwa Dean Davis, na tazama ''ongezeka'' ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa katika vijiji.

Inatendeka namna gani kwenu, wakati munapo tangaza injili ya miviringo tatu ? Nafikiria kwamba munapo tangaza injili ya miviringo tatu, munaona kama watu wengi wanakubaliana nanyi wakati munapo waeleza kwamba dunia ambamo tunaishi ndani imevunjika. Inanisikitisha kusema kama mateso ya dunia yetu yanakuwa kweli kila siku. Wakati nilipokuwa nikitayatisha podikasti hii, inchi yangu imepitiya katika kipindi cha machafuko magumu ya kisiasa tena yakusikitisha. Utajiri na elimu yote ya inchi yetu hazikutusaidia kuziwiya mgawanyiko mkubwa ambao tumo ndani.

Ndiyo, dunia ambamo tunaishi ndani imevunjika. Lakini wakati tunapo tazama uumbaji, tunaelewa japo hiyo kwa machache kama Mungu ni mwema. Wema wake unaonekana ndani ya uumbaji.

Kwa hiyo, ukweli unaotangazwa katika miviringo mbili ya mwanzo ni wa ukweli kwa watu wote : dunia imevunjika, lakini mateso na uharibifu havikuwa na sehemu kwa mpango wa asili wa Mungu kwa dunia. Ukweli unaotangazwa katika mviringo wa tatu unaeleweka kidogo, lakini miongoni mwa miviringo tatu, ni hiyo inayoleta matumaini zaidi.

Mviringo wote wa tatu unasema juu ya Yesu : namna gani alivyokuja duniani, namna gani alivyoishi maisha ya upendo, namna gani alivyokubali kusulubiwa kwa ajili ya dhambi zetu, na namna gani alivyofufuka ndani ya wafu, akiwa mshindaji juu ya dhambi, zidi ya kifo na mateso.

Mviringo wa tatu unasema juu ya uajibikaji wa Mungu. Inatuambia juu ya mkombozi aliyetokea inje ya dunia yetu iliyo vunjika ili kuleta uponyaji na matumaini. 

Hadisi hii ni ya ajabu sana ambayo Yesu mwenyewe aliita Habari Njema. Japo hiyo, mviringo wa tatu ni sehemu ya hadisi ya Mungu isiyo eleweka vizuri na watu waliovunjika ndani ya dunia hii.

Kama wapandaji wa makanisa, pengine mutajiuliza : ''nifanye nini ili kuwasaidia watu kuelewa mviringo wa tatu ili waweke tumaini lao kwa Kristo na waokolewe na mateso tunayoyaishi ndani ya dunia hii?''

Muniruhusu kugawanya pamoja nanyi kinacho nisaidia zaidi :

Omba. Omba kwa ajili yako ili usimulie hadisi vizuri. Omba kwa ajili ya wasikilizaji wako ili Mungu ajifunue kwao wakati wanaposikia Habari Njema. Omba ili kusiwe mtu atakaye kusumbuwa wakati ukisimulia, na kusiwe chochote kitawapotosha wakati wanaposikiliza. Omba ili ujazwe na upendo mkubwa kwa watu unao ongea nao. Weka tumaini kwa Mungu ili akujaze na Roho wake Mtakatifu.

Sijisikie huru. Pengine unaogopa na kuwaza kama utasimulia hadisi yote vizuri. Usiogope. Ujisikie huru na ufanye tu kila iwezekanayo kwako. Mungu iko pamoja nawe, ni yeye anayetumika ili kuwasaidia wasikilizaji wako kuweka tumaini lao kwake.

Ujue kile unataka kuongea, lakini usiwe haraka. Baki mwangalifu na usimulie hadisi ya Yesu wakati unapochora mviringo wa tatu. Usipotoshwe na chochote ; tangaza Habari Njema. Baadaye, acha matokeo mikononi mwa Mungu. Wamoja watatubu na kuamini hapo hapo. Wengine watakuzarau, wewe pamoja na ujumbe wako. Wengine wataitaji kujuwa zaidi. Weka tumaini kwa Mungu. Anatenda kazi.

Na ukumbuke : wakati unapo gawanya Habari Njema, unaleta utukufu kwa yeye aliyekuja kukuokowa. Na hiyo kila siku ni kitu kizuri. Usiache!

Hii ilikuwa neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa katika vijiji.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Kutumika kwa mda wa sasa. Kuomba kwa ajili ya wakati ujao

      Jambo kwa wote. Naitwa Dean Davis, na munasikiliza ''ongezeka'', ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapand...