Ijumaa, 24 Julai 2026

UUMBAJI UNATANGAZA WEMA WA MUNGU

 
















     Jambo kwa wote, naitwa Dean Davis, na tazama ''ongezeka'', ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa katika vijiji.
Wakati nilipoanza kupanda makanisa kwa Bara la Marekani ya kusini, nilitumika pamoja na ndugu aliyeitwa Pedro.

Ijapokuwa upole wake na uaminifu wake katika kutowa injili, mara nyingi alipigwa, kutukanwa na kuzarauliwa kwa ajili ya imani yake kwa Kristo. Japo hiyo, alibaki mvumilivu, akijazwa na upendo, na akitafuta kila siku kusaidia wengine kutambuwa mwangaza wa Yesu. Pedro alirudilia mara kwa mara, hata kama watu wanamuasi Mungu, Mungu anabaki mwema : anaagiza mvula na juwa, na kutowa chakula. Alionyesha hivo kuwa Mungu anaendelea kuonyesha upendo wake ijapokuwa kutokuamini kwetu.
Ujumbe huo sio mpya ndani ya 
Matendo ya Mitume 14:17, Paulo na Barnaba wanasema mambo hayo : Mungu anafanya vema kwa kutowa mvula, mavuno na chakula, akijaza kwa namna hiyo mioyo na furaha.
Wakati tunapotangaza injili kupitiya miviringo tatu, tunakumbusha hivo pia kwamba dunia, hata kama imevunjika, ingali na alama za wema wa Mungu: wema kujitokeza kwa juwa, tabasamu la mtoto, mvuwa inayo otesha mavuno.

Kwa kutowa injili, usipite haraka bila kuonyesha ukweli huo. Inafaa kualika watu kutambuwa wema wa Mungu katika uumbaji, kusikiliza uzoefu wao na kuwaleta kufikiria.
Lakini dunia imevunjika sababu ya dhambi. Watu wanajaribu kuikwepa, lakini Yesu pekee ni njia inayoelekeza kwa Mungu. Kupitiya yeye, tunaweza kupata uzoefu wa kweli wa wema wa Mungu.
Wakati tunapo mrudiliya Mungu kwa imani na kwa toba, tunaanza tayari kuonja kwa mpango wake wa asili, kama kionjo cha mbingu mpya na inchi mpya.

Siku moja, tutaishi furaha hii pamoja na Mungu, katika ushirika wa kweli na siku kuu tukiwa naye.
(Ufunuo 19).

Ni hadisi kubwa ya Mungu. Muigawanye kwa uaminifu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Kutumika kwa mda wa sasa. Kuomba kwa ajili ya wakati ujao

      Jambo kwa wote. Naitwa Dean Davis, na munasikiliza ''ongezeka'', ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapand...