Jambo kwa wote, mimi ni Dean Davis na hii ni "Ongezeka", podikasti inayoleta neno la kutia moyo kwa wapandaji wa makanisa katika vijiji.
Yesu aliamini katika kuongezeka kwa wanafunzi na watenda kazi. Alitoa mfano wa jinsi ya kuhudumu. Yesu alipowachagua mitume wake, “aliweka kumi na wawili wawe pamoja naye, na kuwatuma kuhubiri” ( Marko 3:14 ). Yesu alituchukuwa mda pamoja na wale ambao alikuwa anaenda kuwatuma. Alitumika kama kielelezo chao cha huduma. Waliona jinsi Yesu alivyowakaribia watu, jinsi alivyoponya wagonjwa na kutoa pepo. Walizingatia maisha yake ya maombi na uhusiano wake na wanaume na wanawake, wavulana na wasichana. Kwa hiyo mitume 12 walipotoka kwenda kuhudumu na baadaye wale 72 wakatoka wawili-wawili, walijua la kufanya kwa sababu walikuwa wamemwona Yesu akitenda. Mpandaji wa kanisa, je wanafunzi wako wanajua kuhudumu? Je, wamezingatia maisha yako ya maombi? Je, wanajua jinsi unavyowaendea watu na jinsi unavyoelekeza mazungumzo kuelekea kwa Yesu? Je, wanajua ni lini na jinsi gani unashiriki ushuhuda wako wa sekunde 15 na jinsi unavyowasilisha Injili kwa kutumia miviringo tatu? Je, wamekuona ukifundisha zile amri saba za msingi za Kristo? Wanafunzi wako labda wameona baadhi ya mambo haya. Lakini ukiwauliza, wanaweza kusema wangependa kuona zaidi.
Kama mpandaji wa kanisa, daima una macho yako wazi kutafuta na kutafuta mashamba yasiyopandwa ambapo unaweza kupanda mbegu nzuri ya Injili. Kama mpandaji wa kanisa, unajua vijiji ambavyo hakuna kanisa. Kwa nini usichukue moja au wawili miongoni mwa wanafunzi wako waoga pamoja nawe katika mojawapo ya vijiji hivi visivyo na kanisa? Waonyeshe jinsi unavyotembea katika maombi. Zungumza nao kuhusu kuomba hapo hapo kwa ufahamu. Lakini usitumie mda mwingi kufundisha kwa maneno. Acha matendo yako yafundishe. Wajulishe wafuasi wako kwamba unataka kuwasaidia kuchukua hatua za kwanza katika upandaji wa kanisa. Mojawapo ya njia bora za kumsaidia mfuasi anayeanza kuanzisha kanisa ni kuwasindikiza na kuhudumu pamoja nao. Bila shaka, una uzoefu zaidi katika huduma kuliko wanafunzi wako. Kwa hivyo mara nyingi watakuacha na kujaribu kukufanya ufanye kazi ngumu zaidi. Mara ya kwanza hii sio shida. Lakini hivi karibuni utawaambia kwamba wataomba, kwamba watafundisha, kwamba wataongoza ibada. Utamjulisha mwanafunzi wako kwamba uko ili kumsaidia, lakini yuko tayari kuongoza huduma. Mara ya kwanza hii inaonekana wazimu. Watapinga. Lakini lazima uwe na nguvu.
Usipoondoka ili kumruhusu mwanafunzi wako aongoze huduma mbele yako, atajitahidi bila sababu. Lakini ukirudi nyuma na kusema “Niko hapa kukusaidia, ni juu yako kuongoza njia,” mfuasi wako atakuwa na nguvu katika Bwana na kukuza ujuzi mkuu katika huduma. Njiani unaweza labda kupata pamoja mwanamume au mwanamke wa amani. Katika hatua hii, sukuma kwa upole mwanafunzi wako mbele. Mwambie mtu wa amani kwamba mwanafunzi wako atarudi kuomba pamoja naye na kumfundisha Neno la Mungu. Kwa kufanya hivi, utatoa mfanyakazi mpya ambaye anaweza kufanya wanafunzi na kuanzisha kanisa jipya.
Hii ilikuwa ongezeka na mimi Dean Davis na ninauliza, "Je, ni pamoja na wanani utagawanya nao leo neno hili la kutiya moyo ?

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni