Jambo kwa wote, naitwa Dean Davis, na tazama ''ongezeka'' ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa katika vijiji.
Kupitiya Afrika, watalii, wanasema kuhusu ''Big Five''. Ni haina 5 ya mbuga za wanayama. Wanapendelea kuona : ndovu, vifaru, simba, chui na nyati.
Wakati ninapofikiria kuhusu jumla ya ujumbe wa Biblia na mafundisho yake, ninasema ''Big Three''. Ni amri tatu ambazo ninastahili kutii. Kwangu mimi, ni tatu za muhimu:
Mika 6:8 inajulikana kama mamlaka ya Mika : ''Ee mwanadamu, yeye amekuonyesha yaliyo mema; na BWANA anataka nini kwako, ila kutenda haki, na kupenda rehema, na kwenda kwa unyenyekevu na Mungu wako!''.
Mathayo 22:36-39 ni amri kubwa : ''
[36]Mwalimu, katika torati ni amri ipi iliyo kuu?
[37]Akamwambia, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote.
[38]Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza.
[39]Na ya pili yafanana nayo, nayo ni hii, Mpende jirani yako kama nafsi yako.''
Mathayo 28:18-20 ni misheni kubwa : ''Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.
[19]Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;
[20]na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.''
Nastahili kutii amri hizi kuzidi zingine zote. Je! Wewe vipi?
Wakati tunapo tii amri hizi tatu za Biblia, tunaishi maisha bora ambayo Yesu ali ahidi. Maisha yetu yanajaa na haja pamoja na malengo. Tunakaribia Mungu. Tabia yetu inageuka Ku ambatana na tabia yake. Upendo wetu unakomaa. Tunabariki wengine na sisi tunabarikiwa.
Huduma ya upandaji wa makanisa katika vijiji imetengenezwa kusudi ya kutekeleza amri kubwa. Tumejitolea kufanya wanafunzi wa Yesu Kristo. Tunafundisha wanafunzi kwa kusudi wa tii kwa yote Yesu aliyo tu agiza. Wakati tunapo sema kwamba tunatumika ili kuwe kanisa kwa kila Kijiji cha Afrika ifikapo mwaka wa 2050, tunajitolea kutekeleza amri kubwa.
Tunajuwa kwamba makanisa zenye afya njema ni jamii maalum ambazo Mungu anatumikisha kufanya wanafunzi. Wakati tusemapo "kanisa katika kila Kijiji cha Afrika, ifikapo mwaka wa 2050", tunahakikisha kama tunapenda kila Kijiji kijae wanafunzi wanaojuwa, wanaopenda na kumtii Yesu.
Kwa hiyo, tunaomba : ''mimi hapa Bwana, nitume''. Tunapokea mafundisho ili tuelewe injili. Tunakuza vipawa ili kutangaza Habari Njema na kufundisha watu kumtii Yesu. Tunajitolea kwa watu na kuwaita kuishi kama wanafunzi wa Yesu ndani ya ushirika wa kanisa la mahali.
VCP imetengenezwa tu kwa kutekeleza amri kubwa. Nafurahi sana kwa vile mumechaguwa kwenda, kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, kufanya wanafunzi katika mataifa yote. Muko kwenye njia nzuri; musiache !
Ilikuwa ''ongezeka'' na mimi Dean Davis, nawauliza : ni pamoja na wanani utagawanya nao leo ujumbe huu wa kutiya moyo ?

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni