Alhamisi, 2 Aprili 2026

NAMNA GANI UTATAMBUWA WATU WA AMANI

 










    Jambo kwa wote, naitwa Dean Davis na tazama ''ongezeka'', ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa katika vijiji.

Moja ya uzoefu wa mafanikio ambayo Mtumishi Mkristo anastahili kuishi ni kutafuta na kupata watu wa amani. Munajuwa kama mtu wa amani ni mwanaume ao mwanamuke, aliyetayarishwa na Mungu kwa kupokea injili na kujibu kwa wajumbe wa injili wakati wanaleta Habari njema. Munajuwa watu wa amani wanaoonyeshwa ndani ya Biblia : Mwanamuke Msamaria kwenye kisima, Kornelio, Lidia, Mlinzi wa gereza kwa Filipo na wengine zaidi. Munajuwa namna gani Mungu alivyotayarisha watu hawa kupokea Habari njema na kuweka mawasiliano kati ya wajumbe wa Habari njema na watu wengine ndani ya miji na vijiji. Mfano wao unafuata mtindo ambao Yesu aliwafundisha wamisionari 72. Mtindo huo wa huduma ulioonyeshwa na Yesu, unapatikana katika Luka 10.1-10.

Sifa kwa Bwana, mtindo huu wa huduma ulioanzishwa na Mwokozi bado ungali nguvu hata leo.

Ninakumbuka wakati nilipokuwa nikisaidia kupanda kanisa pa Quito, inchini Équateur. Nilikuwa nikishiriki katika kusanyiko la maombi, ndipo nilipo pokea wito wa kasisi wa Hospital. Alisema : "kuko bwana moja hapa ambaye ameonekana na ugonjwa wa uvimbe kwenye kifuko cha mkojo. Iko na woga sana. Anapashwa sasa kutoka kwenye Hospital yetu nakujielekeza kwenye hospital ingine.

Unaweza kutuma mtu moja wa kanisa lenu kuongea naye haraka?''

Nilijielekeza mara moja kwenye hospital na nikaojiana na yule bwana pamoja na mke wake.

Alikuwa hakika mwenye woga sana. Alijuwa ugonjwa wake. Nilimwambia kama ni mapenzi ya Mungu kuponya watoto wake, iwe hapa chini wala katika ulimwengu ujao.

Niligunduwa kwamba hakuwa nauhakika wowote wa kuwa mtoto wa Mungu.

Niliwaalika, yeye na mke wake, kuomba ili wampokee Kristo, ndivyo walivyofanya. Baadaye, niliomba kwa ajili ya uponyaji wake. Maisha yake yalibadilishwa na kwa mda mchache, aligawanya Habari njema pamoja na jamaa lake.

Wakati waganga walipomfanyia vipimo, walishangaa kuona uvimbe wake ulipona ! Rafiki yangu huyo alikuwa mtu wa amani.

Alionyesha kuwa hivo kupitiya namna alivyo kubali, wakati nilipompendekeza kuomba. Alihakikisha kama alikuwa mtu wa amani kwa kiu chake cha kujuwa mambo ya Mungu na utashi wake wa kugawanya Habari njema pamoja na wengine.

Tunapata watu wa amani kupitiya maombi. Niliitwa kwa ajili yake wakati nikishiriki kusanyiko la maombi pamoja na wengine wapandaji wa makanisa. Jibu lao kwa ombi la kufanya maombi mara nyingi ni alama ya kiu cha kiroho. Tunapata watu wa amani kwa kugawa injili. Watu wa amani walitayarishwa na Mungu kuwa na kiu ya Habari njema ; wanaonyesha kiu hicho kwa namna wanavyoitikia.

Watu wa amani wanatangaza Habari njema waliyosikia kwa jamaa na rafiki zao.

Wanaonyesha wajumbe wa injili kwa ndugu zao. Wanaunganisha wajumbe wa injili pamoja na rafiki zao, jirani zao na wanamemba wa jamaa zao. Watu wa amani ni chombo ambacho Mungu anatumikisha ili kueneza Habari njema kwa watu wengi. Anafanya hivo sababu hapendi hata moja apotee, bali wote waifikie toba.

Wakati tunapata watu wa amani, tunafurahi sababu tunaona na kuamini kwamba injili inaweza kutawanyishwa haraka!

Naweye Je! Uko na hadisi ao umekutana na kijana, mwanaume ao mwanamuke aliye na kiu ya Mungu ? Uko na hadisi wala umekutana na mtu wa amani aliye kubali uwepo, kwa maombi yako na kwa kutangaza kwako injili ? Kama jibu ni ndiyo, endelea kutafuta na kupata watu wengine wa amani. Kama sivyo, omba Mungu akuongoze kuelekea kwenye watu aliyowatarisha kuwa watu wa amani. Wakati wataweka tumaini lao kwa Kristo, uwafundishe kutii kwa kila agizo la Yesu.

Uwasaidiye kuwaleta watu walio kandokando yao kwa Yesu.

Ilikuwa ''ongezeka'', na mimi Dean Davis. ''nawauliza ni kwa wanani mutagawanya nao leo neno hili la kutiya moyo ?''

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

MIVIRINGO TATU AJILI YA KUWAFANYA WANAFUNZI

  Jambo kwa wote, naitwa Dean Davis, na tazama ''ongezeka'', ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa mak...