Jambo, na karibu kwenye ''ongezeka'', ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa katika vijiji.
Mimi ni Brad Snowden. Wakati ninapo gunduwa kitu kizuri, napenda kuigawanya, na ikiwa najuwa kwamba hiki chombo kiko rahisi kwa matumizi muhimu, siwezi kujizuwia kuigawanya.
Leo, tutagunduwa chombo cha kutamanika ajili ya kutangaza Habari njema ya Yesu-Kristo. Mungu anatupa namna ya kugawanya hii habari njema pamoja na wale bado hawajasikia kuhusu upendo wake. Chombo ambacho tutagunduwa leo ni kile cha miviringo tatu. Ni chombo chenye nguvu kwa kutangaza injili ya Yesu-Kristo kwa watu wote. Miviringo tatu ni taswira rahisi inayoshindikiza ushuhuda wako kuhusu Yesu-Kristo. Kuko vipendele sita rahisi kwa kugawanya hiyo ushuhuda, na miviringo tatu zinaweza kuchorwa kwenye karatasi wala chini kwenye udongo. Nani asiye tamani taswira nzuri? Ndiyo lengo kabisa ya chombo hicho. Tunaweza sasa kuongea kuhusu mpango wa Mungu, kwa namna alivyo umba dunia, na vile tunavyoishi ndani ya dunia iliyovunjika na dhambi. Kwa kutumikisha miviringo tatu, unaweza kugawanya hadisi yote, kuanza uumbaji hadi kwenye msalaba. Hii inatupa chombo rahisi ambacho kinaweza kutumikishwa na watu wote.
Kwa kuchora miviringo na kwakuielewesha, maelezo yanakuwa rahisi. Hii inatupa pia fursa ya kuwauliza moja kwa moja kama wako tayari kupokea Yesu-Kristo. Chombo hiki kina nguvu tena ni cha muhimu, na ubora wake zaidi ni vile hakiitaji kukariri maandiko. Kama ukikariri maandiko inakuwa bora zaidi, na unaweza kuigawanya. Nafurahia uumbaji wa Bwana anaye turuhusu kugawanya upendo wake kwa wote.
Anatupa vyombo vinavyo rahisisha ugawaji.
Wakati tunataka kutayarisha shamba kwa upandaji, hatuwezi kwenda bila vyombo vyetu, na baadaye tunastahili kuvitumikisha kwa kupanda mbegu. Inaenda sambamba na chombo cha miviringo tatu ambacho Mungu ametupatiya. Tunapashwa kujizoweza kwa kuvitumikisha, na zaidi mutakavyo vitumikisha kwa nguvu zenu kwa kutangaza injili, zaidi itakuwa rahisi. Ninajuwa kama Mungu atawatumikisha, na hiyo itakuwa na nguvu kwa Ufalme. Tazama neno la kutiya moyo kwa wasimamizi wa upandaji wa makanisa katika vijiji.
Ni kwa wanani utagawanya nao leo?
Mungu awabariki !

.jpeg)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni