Jumanne, 9 Desemba 2025

Uongozi Wa Muwankili - Kuzaa matunda



 

     Tazama Chuck Rapp na ongezeka, ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa katika vijiji na kwa viongozi


Tunaendelea na mfululizo wetu juu ya uongozi wa Muwakili kwa kutafakari sehemu ya mada kubwa kuhusu uwakili.

Leo, napendelea kugawanya nanyi maombi ambayo hapa karibuni niliyasikia kutokea kwa Mchungaji moja kutoka Nigeria.


Kwa kukumbusha, Muwakili anatafsiriwa  kama : ''mtu anayesimamia rasilimali alizopewa na mtu mwengine ili kufikia malengo ya mwenye mali''. Kwa mtazamo wetu, tunaongoza rasilimali tulizopewa na Bwana kwa ajili ya kazi ya upandaji wa makanisa katika vijiji.


Tazama maombi ya Mchungaji Isaac, niliyoyasikia imepita sasa wiki chache:

"Kuwa juu ya kila kitu, tunaomba ili tuwe wenye kuzaa matunda mengi zaidi kwa Ufalme wako.''


Kwa kugawanya maneno ya maombi haya, ninaona alama tatu za muhimu alizotaja.


Anaanza na ''kwa kuwa juu ya kila kitu''. Hii inamaanisha kwamba ni kipaumbele cha kwanza katika uongozi wetu. Kiongozi Muwakili aliye mfano atakazia sana juu kuzaa matunda. Nitaongea mengi katika podikasti yangu ya kufuata juu ya hatuwa hii, kwa kipekee juu ya umuhimu wa  uwajibikaji.

''kipaumbele'' chetu, Mungu, kama ndani ya mfano wa Talanta (Angalia Mathayo 25:14-30), anatarajia kupokea marudilio ya kile alichotupatiya.


Kwa sehemu ya pili, katika maombi yake, Mchungaji Isaac aliomba ili tuwe ''wenye kuzaa matunda mengi zaidi''. Kuzaa matunda ni itaji kubwa ya kiongozi Muwakili. Moja ya vesi inayonigusa sana ni kwa kipekee ile ya Luka 12:48b :

''... Na kila aliyepewa vingi, kwake huyo vitatakwa vingi; naye waliyemwekea amana vitu vingi, kwake huyo watataka na zaidi.''

Neno ''kuomba'' katika toleo la New international Version liko nguvu. Tafsiri zingine, kama vile New English Version, inatumia maneno '' hitaji'', ''kungoja'' ao ''kuwajibisha''. Ujumbe uko wazi : Bwana ataomba kwa  viongozi yale waliyatenda, namna walivyotumikisha rasilimali walizopewa.


Kwa mwisho, alimalizia maombi yake ''kwa ajili ya Ufalme wako''. Nafurahia hiyo zaidi sana. Munaona, ni Ufalme wa Kristo ambao utafaidika na kazi yetu. Hatutumiki ilikujijengea umaarufu wetu ao kuangalia ajili ya huduma yetu binafsi.

Viongozi mawakili hawatumiki sababu ya kupandishwa vyeo. Yesu alifundisha hivo katika hotuba yake juu ya mlima : ''utafuteni kwanza Ufalme wa Mungu na haki yake, na mengine mtazidishwa baadaye.'' (Mathayo 6:33)

Mara nyingi, ujuzi wala kupandishwa cheo vinaweza kutokea baada ya kazi yetu, lakini ni matokeo tu, wala siyo malengo za uongozi wa Muwakili.


Wakati ujao, tutaendelea na somo letu kuhusu uongozi wa Muwakili.

Ilikuwa neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa na kwa viongozi katika vijiji.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

MIVIRINGO TATU AJILI YA KUWAFANYA WANAFUNZI

  Jambo kwa wote, naitwa Dean Davis, na tazama ''ongezeka'', ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa mak...