Alhamisi, 31 Julai 2025

Kufundisha kwa ajili ya mavuno mengi


 Jambo, munasikiliza, Ongezeka, ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa na kwa viongozi wakikristo katika vijiji. Mimi ni Brad Snowden.

Yohana 4:35-38

: ''Hamsemi ninyi, Bado miezi minne, ndipo yaja mavuno? Tazama, mimi nawaambieni, Inueni macho yenu myatazame mashamba, ya kuwa yamekwisha kuwa meupe, tayari kwa mavuno. 

Naye avunaye hupokea mshahara, na kukusanya matunda kwa uzima wa milele, ili yeye apandaye na yeye avunaye wapate kufurahi pamoja.   Kwa maana hapo neno hilo huwa kweli, Mmoja hupanda akavuna mwingine. 

 Mimi naliwatuma myavune yale msiyoyataabikia; wengine walitaabika, nanyi mmeingia katika taabu yao.''

Yesu, katika huduma pamoja na wamitume wake, alikuwa akiwafundisha kwa namna ya kuzuwa maswali mengi ndani ya roho zao. Katika kifungu hiki, swali nyingi zingeumiza mioyo yao : ni nani ninastahili kutafuta? Nani anaendelea kuvuna, na anavuna nini? Namna gani walipata tunda hili ? Mawazo na swali hizi zinaweza kuongezeka.

Yesu alitupatiya mifano mingi ya Mitume waliofunzwa kwa maswali yaliyo wazi, yanayoleta mabishano ya nguvu na kwa maelezo bora.

Huduma yake ilivizia kuongezeka kwa mitume na faida yake katika dunia hii. Umaarufu ambao kila mmoja wao angekuwa nao, na maisha mengi ambayo yangebadilishwa.

Siyo tofauti kwetu Sisi pia. Bwana anapenda kujionyesha kwetu ili tukomae katika ujuzi wa vile alivyo na hata zaidi tena. Anapenda pia kututumikisha ili kuongoza watu wengine na kuwasaidia kukomaa katika huduma yao yakipekee.

Namna gani tunaweza kuwa chanzo cha kuwatiya moyo ndani ya maisha yao?

Namna gani tunaweza kuwahimiza wengine kuamini kwamba Mungu anataka kutumika zaidi pamoja nao ?

Namna gani ya kugawanya maneno ya haki yanayozuwa maono mapya ?

Ni nani Bwana anaweka rohoni mwako ili kumwendea, kutembea karibu yake na kumusaidia kugeuka kuwa mvunaji mukubwa ?

Ni maongezi gani yaliyo ya muhimu ili wachukuwe maamuzi mazuri na kuwakilisha mpango wa Mungu kwa ajili ya maisha yao na kwa wale wanaoitaji tumaini ?

Wapandaji wa makanisa, viongozi, ni furaha gani kuona wanafunzi wenu kugeuka kuwa wenye hekima !

Mithali 11:30 :"Mazao ya mwenye haki ni mti wa uzima; 

Na mwenye hekima huvuta roho za watu.''

Yote tunaweza kufanya ili kutiya moyo, kufundisha, kutowa mfano, kutembea karibu na wengine na kuwatolea yale Mungu alitupatiya ili wageuke kuwa na hekima kwa yale yanayofurahisha roho ya Mungu na kazi bora.

Endelea, sababu kwa mda uliyopangwa, utavuna matunda ya kazi yako yote.

Ilikuwa neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa katika vijiji.

Ni pamoja na wanani utagawanya nao leo hayo ?

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

MIVIRINGO TATU AJILI YA KUWAFANYA WANAFUNZI

  Jambo kwa wote, naitwa Dean Davis, na tazama ''ongezeka'', ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa mak...