Jumanne, 9 Desemba 2025

UONGOZI WA MUWAKILI - Kuongoza madaraka tuliyopewa



 

Mimi ni Chuck Rapp na ongezeka, ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa na kwa viongozi katika vijiji.

Tunaendelea na mfululizo wetu juu ya uongozi wa Muwakili kwa kutafakari sehemu ya mada kubwa zinazoshikamana na hatuwa hili. Leo, napendelea kugawanya nanyi maombi ambayo niliyasikia hapa karibuni kutoka kwa mmoja wa watumishi wenzangu makasisi wa O.M.S.


Kwa ukumbusho wa haraka, Muwakili anatafsiriwa kama ''mtu anayesimamia rasilimali alizopewa na mtu mwengine ili kufikia malengo ya mwenye mali''.

Kwa mwelekeo wetu, tunaongoza rasilimali na madaraka ambayo Bwana alitupatiya kwa ajili yetu ya upandaji wa makanisa katika vijiji.


Tazama maombi yake: ''Bwana, tafazali,  tusaidie kuongoza madaraka yetu vizuri tuliyopewa.''

Ombi hili liligusa moyo wangu, sababu kwa mda wote wa majifunzo ya mfululizo juu ya uongozi, nilijihusisha sana juu ya uongozi wa rasilimali za kiuchumi wala za binadamu. Mungu anatupatia watu wazuri ili tutumike pamoja nao, wanasaidia kwa pesa za kutosha kwa ajili ya huduma.


Lakini anatupatiya pia madaraka yake.

Tujifunze jambo hili leo. Tazama vesi mbili za Biblia zinazozungumzia Mada hii:


''Watiini wenye kuwaongoza, na kuwanyenyekea; maana wao wanakesha kwa ajili ya roho zenu, kama watu watakaotoa hesabu, ili kwamba wafanye hivyo kwa furaha wala si kwa kuugua; maana isingewafaa ninyi.''

Waebrania 13:17


Sisi kama viongozi, Mungu alituweka katika hatuwa za madaraka.

Lakini, kama watumishi-viongozi, madaraka haya yanapashwa kutumikishwa kwa ajili ya kuwahidumia wengine na kuhudumia Ufalme. Napenda kukazia nukta mbili hapa :


1. Tunastahili kukesha kwa ajili ya wale tunaowaongoza.

2. Mungu anatudai mbele zake kwa namna tunavyokesha kwa ajili yao.


**"Maana neema ya Mungu iwaokoayo wanadamu wote imefunuliwa; 

nayo yatufundisha kukataa ubaya na tamaa za kidunia; tupate kuishi kwa kiasi, na haki, na utauwa, katika ulimwengu huu wa sasa; 

Nena maneno hayo, onya na kukaripia kwa mamlaka yote; asikudharau mtu awaye yote".

 _ Tito 2:11-12,15


Kwa mara ingine tena, napenda kukazia sehemu ya hatuwa ambazo tunapata katika mafundisho ya Mtume Paulo :


1. Ujumbe wa wokovu wa Mungu unawahusu watu wote.

2. Neema ya Mungu haistahili kutumikishwa vibaya. Tunastahili madaraka tuliyopewa kwa kufundisha wanafunzi kuzikataa tamaa za dunia na kuishi maisha matakatifu.

3. Kwa utumishi wa madaraka yetu, tunastahili kutiya moyo pia kuhamakia, kwa usawa. Kuhimarisha kwa zaidi kunaweza kuzuwa kiburi kwa wengine. Kuhamakia kwa zaidi kunaweza kuwavunja moyo. Walio chini ya madaraka yetu wanaitaji hivi vitu viwili, na tunaitaji roho ya utambuzi kwa kujuwa kile nilicho cha muhimu kwa kila nyakati na majira.


Kwa turu nyingine, tutaendelea na somo letu kuhusu uongozi wa Muwakili.

Ilikuwa neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa na kwa viongozi wao

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

MIVIRINGO TATU AJILI YA KUWAFANYA WANAFUNZI

  Jambo kwa wote, naitwa Dean Davis, na tazama ''ongezeka'', ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa mak...