Mimi ni Chuck Rapp na ongezeka, ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa katika vijiji na kwa viongozi.
Mada yetu leo ni Uongozi kama vile Muwakili. Kwa kukumbusha haraka, Muwakili anatafsiriwa kama ''mtu anayesimamia rasilimali alizopewa na mtu mwengine ili kufikia malengo ya mwenye mali''. Kwa mwelekeo wetu tunaongoza rasilimali tulizopewa na Bwana kwa ajili ya kazi yetu ya upandaji wa makanisa katika vijiji.
Kwa mwanzo wa mwaka, katika kiingilio changu kuhusu swala hili, nilisema kama tutachunguza Mada tano kubwa za uongozi ;
1. Tabia inahusika
2. Mawakili wanashurutishwa kutowa ripoti ya uwakili wao
3. Muwakili anastahili kujenga mawasiliano
4. Muwakili anastahili kugawanya malengo ya maendeleo ya bwana wake
5. Mawakili waaminifu wanaendelea katika hatuwa zao za usimamizi
Katika podikasti ya mwanzo wa mwezi wa juni, nilijadili Mada ya kwanza : Tabia inahusika.
Leo tutajadili Mada ya pili : Usimamizi. Tuliiona katika mifano ine tuliyojifunza, na zaidi kwa upekee ndani ya mfano wa talanta katika Mathayo 25:14-30
Kwa mwanzo, kuko zawadi kwa uwakili bora. Angalia katika vesi za 21 na 23, kuhusu wale waliopata talanta tano na talanta mbili, kwa mara moja, maneno ya bwana yanafanana : ni vema, Mtumishi mwema na mwaminifu !
Ulikuwa mwaminifu kwa mambo madogo, nitakupa mengi.''
Mara nyingi, ''usimamizi'' unatumikishwa tu kwa mwelekeo mbaya, lakini siamini kuwa hii inastahili kuwa vile.
Kama kiongozi, utumishi bora wa usimamizi ni kukamilisha mwenendo, tendo ao matokeo binafsi. Inafanishwa na kiongozi wa michezo (kocha) anayewapa moyo na kuimarisha vizuri mchezaji wakati anapofaulu.
Kwa hiyo, anapashwa pia kuonekane usimamizi hata wakati wa kushindwa.
Katika mfano wetu, Muwakili mbaya alihamakiwa na kuhazibiwa. Tunayaona hayo kwa vesi za 24-30.
Mtumishi ambaye hakufanya chochote na talanta yake moja, alionekana kuwa ''mbaya '' na ''mvivu'', na talanta aliyokuwa nayo ilinyanganywa.
Viongozi bora wachaMungu wanastahili kuwa na hekima na utambuzi muhimu ili kujuwa ni kwa wakati gani na kwa namna gani kuwafanya wengine kuwa wasimamizi wa mwenendo wao mbaya, matendo mabaya Wala matokeo mabaya. Napendekeza kwamba sababu maalm ni wakati mtu anajuwa anacho stahili kufanya lakini haifanye. ( Angalia Yakobo 4:17.) Ndani ya mfano wa talanta, Mtumishi ''mbaya'' alijuwa kama bwana alitarajia matokeo kwa yale aliyompa.
Kwa namna ingine, ningesema kwamba wakati makosa yanapotendeka sababu mtu moja hakujuwa kilicho tarajiwa ao kile angestahili kufanya, hiyo ingestahili kutumikishwa kama fursa ya mafundisho kwa kiongozi.
Mawakili wanaombwa kutowa ripoti ya uwakili wao, na viongozi wanatumikisha usimamizi moja kwa moja kwa washirika wao.
Ilikuwa neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa katika vijiji na kwa viongozi wao.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni