Jumanne, 9 Desemba 2025

UONGOZI WA MUWAKILI - Kuhamakia kwa mamlaka kama ikiitajika


 

  Mimi ni Chuck Rapp na ongezeka, ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji na kwa viongozi wa makanisa.

Tunaendelea na mfululizo wetu juu ya uongozi. Leo, napendelea kugawanya nanyi maelekezo ya ziada kuhusu kitu nilicho shiriki imepita sasa wiki mbili.


''Muwakili'' anatafsiriwa kama ''mtu anayesimamia rasilimali alizopewa na mtu mwengine, ili kufikia malengo ya mwenye mali''. Katika muelekeo wetu, tunasimamia rasilimali na tunatumikisha mamlaka tuliyopewa na Bwana kwa ajili ya kazi yetu ya upandaji wa makanisa katika vijiji.


Tazama mara ingine ombi ya hapa karibu ya moja kati ya rafiki zangu makasisi wa OMS :

''Bwana, tusaidie kuongoza madaraka tuliyopewa.''


Katika vipindi vyangu vilivyopita. Niligawanya haya mafundisho kuhusu uongozi yaliyotolewa katika Tito 2:15 : ''Fanya mambo hayo, onya na kukaripia kwa mamlaka. Mtu yeyote asikuzarau. 


Kwa kutafakari juu ya mafundisho ya Mtume Paulo, nilijiuliza maswali mengi :


Ni kwa matokeo gani viongozi wanastahili ''kukaripia kwa mamlaka ?


Ni kwa hatuwa gani viongozi wanastahili kujizuwia kuhamakia mtu?


Kama ni muhimu kukaripia, ni kwa namna gani tunastahili kuitenda?


Kwa mwisho, Paulo anapendelea kusema nini wakati anasema kwamba tunastahili kukaripia kwa mamlaka?


Mbele ya yote, kukaripia ni sahisho linalo elekea kwa mtu anayejidanganya katika mafundisho wala katika mwenendo wake. Shabaa ya kukaripia kwa haki ni kumrudisha kwa ukweli ; siyo kumfezehesha. Viongozi wazuri wachaMungu wanastahili kuwa tayari kuhamakia wengine ili kuwafanya upya ao kuwakingia na yale ambayo yangeleta shida kutokana na tukio.


Baadaye, ningependekeza kama kungekuwa mda ambao tungeweza kujizuwia kuhamakia.

Kwa jumla, ninafikiria matokeo mawili. Ya kwanza ni wakati kaka wala dada mkosaji haiko kwenye mamlaka yetu : yeye ni Msimamizi mbele ya wengine. Hiyo inajumlisha pia matokeo ambayo sisi hatuna mawasiliano na yule anayepotea kwa mafundisho ao kwa mwenendo. (Angalia Mithali 27:6)


Hii inanielekeza kwa hatuwa zimoja juu ya namna, viongozi wa kiroho wanastahili kukaripia. Waefeso 4:15 inatusii ''kusema ukweli kwa upendo '' kwa hatuwa hii, ningependekeza kwamba wakati tunachaguwa kuachilia mwenendo wa dhambi wala mafundisho potevu, hatutendi kwa upendo zidi ya mtu mwovu ; kinyume chake ni kwamba, tunajihuzuru kwa majukumu ya kiongozi.


Kwa mwisho, Paulo anafundisha viongozi wa kiroho kukaripia kwa ''mamlaka yote'' inamaanisha nini ? Mamlaka yote'' yanatolewa na Mungu, na wamoja wetu wanatumia madaraka ni wasimamizi mbele ya Mungu.


Kwa kuhitimisha, Yakobo 5:20 anasema : 

''Jueni ya kuwa yeye amrejezaye mwenye dhambi hata atoke katika njia ya upotevu, ataokoa roho na mauti, na kufunika wingi wa dhambi.''


Mara ingine, tutaendelea na somo letu kuhusu uongozi wa Muwakili.

Ilikuwa neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa na viongozi wa makanisa katika vijiji.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

MIVIRINGO TATU AJILI YA KUWAFANYA WANAFUNZI

  Jambo kwa wote, naitwa Dean Davis, na tazama ''ongezeka'', ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa mak...