Mimi ni Chuck Rapp na ongezeka, ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa katika vijiji na kwa viongozi.
Mada yetu leo ni Uongozi kama vile Muwakili. Kwa kukumbusha haraka, Muwakili anatafsiriwa kama ''mtu anayesimamia rasilimali alizopewa na mtu mwengine ili kufikia malengo ya mwenye mali''. Kwa mwelekeo wetu tunaongoza rasilimali tulizopewa na Bwana kwa ajili ya kazi yetu ya upandaji wa makanisa katika vijiji.
Kwa mwanzo wa mwaka, katika kiingilio changu kuhusu swala hili, nilisema kama tutachunguza Mada tano kubwa za uongozi ;
1. Tabia inahusika
2. Mawakili wanashurutishwa kutowa ripoti ya uwakili wao
3. Muwakili anastahili kujenga mawasiliano
4. Muwakili anastahili kugawanya malengo ya maendeleo ya bwana wake
5. Mawakili waaminifu wanaendelea katika hatuwa zao za usimamizi
Mada ya leo ni kwamba Muwakili anapashwa kugawanya malengo ya maendeleo ya bwana wake, na tutaijadili katika mwelekeo wetu wa upandaji wa makanisa katika vijiji.
Ya kwanza, tuzingatiye maono yetu ya VCP ambayo ni : ''kanisa katika kila Kijiji cha Afrika ifikapo mwaka wa 2025'' haitawezekana kufikia lengo hili bila ukuaji. Kama tunapenda kuongoza vizuri rasilimali na utoaji kwa Mungu kupitiya VCP, tunastahili kutamani kuwa na ukuaji (Na tumsifu Mungu, sababu VCP imepata maendeleo makubwa ya kushangaza, sababu kwa leo tunatumika sasa katika mataifa 36 za Afrika na kuwa na zaidi ya vituo vya mafunzo 800.)
Ya pili, tuzingatiye Mada hii kwa maoni ya Bwana wetu. Sababu gani Bwana wetu angekuwa na maoni ya ukuaji ?
Tuangalie maandiko.
2Petro 3:9 inatuambiya : ''Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba.'' mapenzi ya Bwana ya kuona ''wote wamefikilie toba'' inafanana kabisa na lengo la ukuaji wa Ufalme.
Tunaona ujumbe mwengine wa kufanana na huu wa Mtume Paulo anaye andika kwa 1Timotheo 2:3b-4 :
''... Mungu Mwokozi wetu;
ambaye hutaka watu wote waokolewe, na kupata kujua yaliyo kweli.'' hapo pia, tunaona lengo la maendeleo la Bwana wetu, sababu matakwa yake ni kwamba watu wote wafikilie ujuzi wa wokovu wa Yesu-Kristo.
Kwa mwisho, katika Ufunuo wa Yohana, tuzingatiye maono haya kwa sura ya 7, vesi 9 : ''Baada ya hayo nikaona, na tazama, mkutano mkubwa sana ambao hapana mtu awezaye kuuhesabu, watu wa kila taifa, na kabila, na jamaa, na lugha, wamesimama mbele ya kile kiti cha enzi, na mbele za Mwana-Kondoo, wamevikwa mavazi meupe, wana matawi ya mitende mikononi mwao ...''
Mkutano mkubwa ambaye hakuna mtu awezaye kuuhesabu wa waabiduo katika mbingu, ''wa kila taifa, wa kila lugha, wa kila jamaa na Kabila '' inaonyesha ukuaji wa Ufalme wa Bwana wetu, na ndiyo shabaha yake kwetu ili tushiriki kwa hilo kusanyiko kubwa.
Ilikuwa neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa katika vijiji na kwa viongozi wao.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni