Mimi ni Chuck Rapp na ongezeka, ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji na wasimamizi wa makanisa katika vijiji
Mada yetu kwa mwaka huu wa 2025 ni Uongozi wa Muwakili.
Kwa ukumbusho, Muwakili anatafsiriwa kama ''mtu anayesimamia rasilimali alizopewa na mtu mwengine ili kufikia malengo ya mwenye mali'' kwa mtazamo wetu, tunaongoza rasilimali tulizopewa na Bwana kwa ajili ya kazi yetu ya upandaji wa makanisa katika vijiji.
Katika vipindi vilivyopita, nilionyesha Mada tano kubwa za uwakili:
1. Tabia inahusika.
2. Mawakili wanaombwa kutowa ripoti ya uwakili wao
3. Muwakili anapashwa kujuwa kujenga mawasiliano
4. Muwakili anastahili kugawanya malengo ya ukuaji ya bwana wake.
5. Mawakili waaminifu wanaendelea katika hatuwa zao za usimamizi.
Leo, tutajadili Mada hii ya mwisho, iliyo ya muhimu sana, na tunarudilia mfano wa talanta katika kitabu cha Mathayo 25:14-30
Kumbukeni : watumishi waliyo pokea mifuko tano na mbili za zahabu walikuwa mawakili waaminifu na walizidisha rasilimali zao.
Napenda tuangalie kwenye vesi za 28 na 29.
Wakati Mtumishi mvivu hakuleta chochote kwa bwana wake, bwana wake alisema hivi:
Ondoeni kwake ule mfuko wa zahabu, na mumupe yule aliye na mifuko kumi.
Sababu kwake aliye na vingi, atapewa mengine, na atakuwa na mali mingi...''
Nataka kurudilia huyu msemwa, sababu ni wa muhimu sana;
''kwake aliye na vingi, atapewa mengine, na atakuwa na mali mingi.''
Kanuni iko wazi;
✓ mawakili waaminifu watapewa zaidi.
Kanuni hii inafanyika sana ndani ya kazi yetu ya upandaji wa makanisa katika vijiji.
Tunaona vuguvugu ya ajabu na upendeleo wa Mungu unaonekana kupitiya Afrika kwa mpango wa shirika la VCP (village church planting) angalia matokeo fulani:
Kwa miaka tano, tulizidisha mara mbili hesabu ya inchi ambamo tunatumikia ndani.
Kwa miaka tano, tumezidisha mara mbili hesabu ya vituo vya mafunzo vya VCP.
Kwa miaka tano, bajeti yetu (tukiongeza pesa za miradi muhimu) ilizidishwa mara mbili
Kwa mwaka wa 2024, zaidi ya waamini wapya 250 000 walimpokea Kristo, ripoti ikitolewa ndani ya makanisa yaliyopandwa na mpango wa VCP.
Tuna moyo wa shukurani kwa upendeleo na mpangilio wa Mungu, na tunastahili kuongoza vizuri yote hayo.
Pamoja na kuongezeka huku kwa VCP, inatupasha kuwa na watendakazi na wasimamizi. Hii inamaanisha kwamba kuwa na waalimu wapya, waratibu wapya, na makasisi watakao ongezwa kwenye timu _ na watachaguliwa miongoni mwa wale walio onyesha uwakili wa uaminifu.
Mawakili waaminifu wanaendelea katika hatuwa zao za usimamizi.
Ilikuwa neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa na viongozi wa makanisa katika vijiji.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni