Kwa ukumbusho, Muwakili anatafsiriwa kama ''mtu anayesimamia rasilimali alizopewa na mtu mwengine ili kufikia malengo ya mwenye mali''. Kwa mtazamo wetu tunaongoza rasilimali tulizopewa na Bwana kwa ajili ya kazi yetu ya upandaji wa makanisa katika vijiji.
Kwa kipindi kilichopita, nilionyesha Mada tano kubwa za uwakili :
1. Tabia inahusika
2. Mawakili wanaombwa kutowa ripoti ya uwakili wao
3. Muwakili anastahili kujenga mawasiliano.
4. Muwakili anapashwa kugawanya malengo ya ukuaji ya bwana wake.
5. Mawakili waaminifu wanaendelea katika hatuwa zao za usimamizi.
Hadi sasa, tulijadili Mada mbili za mwanzo.
Leo, tutaangalia kwa makini kuhusu ukweli ulio muhimu :
👉 Uongozi wa Muwakili unahitaji kujenga mawasiliano pamoja na Bwana, wanafunzi wetu pamoja na rasilimali tunazo ongoza.
1. Kujenga mawasiliano na Bwana.
Kama tukiwa viongozi -mawakili, tunastahili kutekeleza malengo ya Bwana, ni muhimu sana kujenga mawasiliano binafsi naye.
Katika muelekeo wetu, Bwana wetu ni Yesu-Kristo.
Tunastahili kumjuwa vizuri, kuelewa Roho yake kwa ajili ya mioyo na shabaha yake, ambayo inaonyeshwa waziwazi katika Mathayo 28:19-20a:
Mathayo 28:19-20
[19]Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;
[20]na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi''
Kwa hiyo, tunapashwa kumjuwa kwa undani Bwana na mipango yake kwa maisha yetu na kwa huduma zetu.
2. Kujenga mawasiliano pamoja na wanafunzi wetu
Tukiwa kama viongozi-mawakili, tunastahili pia kuendelesha mawasiliano yenye nguvu pamoja na wale wanaotufuata.
Mtaalamu wa uongozi, Mchungaji na Mwandishi John Maxwell, siku moja aliandika :
''anayefikiriya kuongoza na kama hana wanafunzi ni kama mtu anaye jitembeza.''
Kwa namna nyingine, kwa kuwa Muwakili wa kweli, unapashwa kuwa na wanafunzi
_ na hiyo inawezekana tu kama tunajenga mawasiliano na wao.
Ningesema kwamba kuendelesha mawasiliano inaomba kwa pamoja kuwa na ukaribu na mda.
Kiongozi VCP, nakuhimiza kufuata mashauri ya Mithali 27:23:
''Fanya bidii kuijua hali ya makundi yako;
Na kuwaangalia sana ng’ombe zako.''
3. Jenga mawasiliano na rasilimali
Kwa mwisho, kiongozi Muwakili anapashwa pia kujenga mawasiliano mazuri na rasilimali.
Ninajuwa kwamba nilistahili kufanya utafiti kuhusu Mada hii, na tazama niliyogunduwa :
''kujenga mawasiliano na rasilimali inahusisha siyo tu kujenga urafiki, bali pia kuyaweka kwa faida ili kwa mwisho yalete mafanikio na mapato.
Hiyo inahusu pia ugawaji wa ujuzi, wa uzoefu, pamoja pia na kutowa mashauri na msaada kwa wengine. Inatokana na kujenga njia ya uaminifu ambayo kwa hiyo tunaweza tegemea ili kupata mwelekeo na majadiliano, zaidi kwa wakati rasilimali ni ndogo.''
Viongozi mawakili wako na nguvu zaidi na uhodari sana wakati wanatumika kwa pamoja.
Ilikuwa neno la kutiya moyo kwa wapandaji na kwa viongozi wa makanisa katika vijiji

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni