Alhamisi, 31 Julai 2025

WAOMBEE WALE UNAOWAFUNDISHA


Jambo nyote ! Tazama Ongezeka , ni podikasti ya kuwahimiza wapandaji na viongozi wa makanisa. Mimi ni Brad Snowden, na leo ningependa kujadili kipengele cha maisha ya Yesu. Bwana alikuwa na uhusiano maalum na wanafunzi Wake. Aliwafundisha, kuwatia moyo, na kuwawezesha kutumia kile alichowapa kutimiza mipango na malengo ya Baba wa Mbinguni. Kuwa tu mfuasi wa Kristo ni chanzo kikuu cha unyenyekevu, lakini tunaposikia maombi yake kwa ajili yetu katika Yohana 17, inatufanya kuwa wanyenyekevu zaidi. Kristo alituonyesha njia ya kufuata, mfano sio tu kwa maisha yetu wenyewe, bali pia jinsi tunapaswa kuwatendea na kuwaheshimu ndugu na dada zetu katika Kristo. Katika Yohana 17, katika dakika za mwisho kabisa za maisha ya Yesu duniani, tunagundua mtazamo wa maombi, uliojaa hamu kwamba Baba wa Mbinguni angeweka ndani yetu yote ambayo Yesu alikuwa nayo. Yesu alichotaka kwa wanafunzi wake kumi na wawili—na anachotaka kwetu leo—ni kwamba tujazwe na Roho wake Mtakatifu, ili tuwe mashahidi wake. Tupo hapa duniani ili kutiana moyo na kuombeana. Tena na tena, katika Yohana 17, tunamwona Yesu akiwaombea wanafunzi wake,  wakijua jinsi ambavyo wangetumiwa kwa ajili ya Ufalme wa Mungu baada ya kuondoka kwake. Hakuwaombea tu wanafunzi wake, bali pia wale ambao wangeguswa na Habari Njema wangehubiri na kuishi mbele yao. 

Oh, kama tungeweza kufahamu uwezo wa kuwaombea wanafunzi wetu na kwa vizazi ambavyo maombi hayo yanaweza kufikia! Ninashangaa, hata katika maisha yangu mwenyewe, ni mara ngapi ninafikiria juu ya faidi hii ya kizazi. Wanafunzi ambao Bwana amenipa neema ya kusaidia, kutia moyo, na kuandamana… ni wangapi wataguswa nao kupitia nguvu za Roho Mtakatifu? Ni ajabu kufikiria juu ya suala la vizazi. Kadiri tunavyozeeka, ndivyo vizazi vingi tunavyoweza kugusa, au angalau, ambavyo vinaweza kuwa sala yetu. Yesu aliwaombea wanafunzi wake. Ushindi wa namna gani! Ombi lake lilikuwa kwamba sote tuunganishwe katika moyo mmoja na akili moja na Kristo. Kuunganishwa na wanafunzi wetu, tunaposhiriki, kuwatia moyo, kugusa maisha yao, na kumruhusu Mungu awaumbe wao wenyewe wawe wafanya-wanafunzi… na kuzidisha kunaendelea na kuendelea. Katika Yohana 17, moyo wa Kristo uliwekwa katika kuwaombea wanafunzi wake. Kuna nguvu iliyoje katika maombi!Tusijiepushe na fursa hii ya kuwaombea wanafunzi wetu. Tuombeane, tuombe Mungu atimize mapenzi yake, hata baada ya muda mrefu tutakapo toweka. 

Na mfano huu uendelee kubeba ujumbe wa Habari Njema ya Yesu Kristo. Oh, kama tungeweza kuwa na moyo huu! Ikiwa tungeweza kubarikiwa kujua kwamba Bwana husikia maombi yetu na kwamba wanafunzi wetu wanabadilishwa kwa hiyo. Ni baraka ya namna gani, ni fursa ya namna gani, kwamba Kristo alitupa mfano huu katika Yohana 17 kwa huduma yenye matunda: kuwekeza kwa wanafunzi wetu, na huanza na maombi. 

Ilikuwa neno la kutia moyo kwa wapandaji wa makanisa. 

Bwana akubariki unapowaombea wanafunzi wako. Je, ni pamoja na wanani, utagawanya nao leo neno hili la kutiya moyo ?

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

MIVIRINGO TATU AJILI YA KUWAFANYA WANAFUNZI

  Jambo kwa wote, naitwa Dean Davis, na tazama ''ongezeka'', ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa mak...