Alhamisi, 31 Julai 2025

UNAWEZA KUIFANYA


   Jambo kwa wote, naitwa Dean Davis na tazama ''ongezeka'' ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa katika vijiji.

Miongoni mwa maneno ya ajabu zaidi yaliyo tamkwa na Yesu, mamoja yanaelekezwa kwa wanafunzi wake kwa nyakati za kutatanisha. 

Karibu ya miaka tatu ya mafundisho ya kuendelea, hapa duniani, wanafunzi wa Yesu walikuwa bado kuelewa Yesu alikuwa nani.

Yohana 14 inatuambia juu ya kuchanganyikiwa kwa Tomaso kuhusu utu wa Yesu. Vesi ya 8 inazungumzia kuchanganyikiwa kwa Filipo kuhusu mawasiliano ya Yesu na Mungu Baba.

Ni katika hali hii ya kuchanganyikiwa, ya uzaifu na upungufu wa wanafunzi wake, kwa kuelekea mwisho wa maisha ya Mwokozi wao hapa dunuiani, ndipo Yesu alisema: Amin, Amin, nawaambia, yeye aniaminiye mimi atafanya naye pia yote nifanyayo, hata makubwa kuliko haya, sababu naenda kwa Baba. Na yote mutakayoomba kwa Jina langu, nitalifanya ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana.''

Ajabu! Yesu aliwaambia wanafunzi wake, wakiwa wakichanganyikiwa, wangetekeleza mambo makubwa zaidi kuliko yake kama tu wangeamini.

Tunajuwa kazi za Kristo : Aliponya wagonjwa, alifufuwa wafu, kuwafunguwa walioonewa na shetani, kupambana na viongozi wa kidini wanafiki, na kutangaza Ufalme wa Mungu kwa maelfu ya watu katika Palestine. Hayo ndiyo matendo makubwa. Ijapokuwa Yesu anasema kwamba wanafunzi wake watafanya makubwa zaidi kuliko yake, Ila kwa shurti tu ya kuamini.

Maneno ya Bwana wao yalisikilika kuwa hayawezekani machoni pa wanafunzi wake.

Walijuwa kwamba ni namna gani walivyo: wafuasi wakuchanganyikiwa wenye woga wa Rabbi ambaye hawakumuelewa vizuri. Ni kwa namna gani wangeweza kufanya matendo makubwa zaidi yake?

Ijapokuwa, Yesu aliwapa moyo. Kwa kila tukio lolote lile aliwapa moyo.

Kwa mda ambao kila kitu kingekuwa giza, aliwaamini. Kwa Imani, Yesu aliona kile wangeweza kutimiza. Aliwahimiza kwa kusema:

''amini, amin, nawaambia , yeye aniaminiye mimi, atafanya naye pia yote nifanyayo hata makubwa kuliko haya, sababu naenda kwa Baba.''

Nina uhakika kwamba ninyi ndugu na dada zangu, kwa kuangalia wanafunzi wenu, mutaona pia uko kuchanganyikiwa na huo woga ambao Yesu aliusikia kwa Tomaso na Filipo.

Inakufikia pengine kujiuliza: ''ni nini kabisa watatekeleza?''

Fanya anagalisho kwa mda huo. Usivunjike moyo kwa vitisho. Badala yake, tamka neno la imani na la kutiya moyo. Ambia wanafunzi wako, kwa wakati wao wa mashaka : ''unaweza kuifanya. Mungu yu pamoja nawe. Usiache. Endelea kuwa na tumaini kwa Yesu. Utatimiza mambo makubwa''.

Nakumbuka, nilikuwa karibu na miaka 23. Nilikuwa mwanafunzi kwenye chuo cha Biblia. Sikuwa kabisa mwenye ujuzi zaidi wala mwenye busara zaidi.

Nilikuwa nikijiuliza namna gani nitakavyokuwa Siku za usoni.

Lakini wanaume wamoja waaminifu katika kanisa langu, waliniambia kama waliamini kuwa nitafanya mambo makubwa. Sikuamini maneno yao, lakini yalinitiya moyo. Na leo, ni zaidi ya miaka 50 iliyopita, wakati ninapofikiria maneno yao, ninakubali kwamba Mungu alifanya mambo makubwa ya ajabu ndani ya maisha yangu kupitiya hayo.

Si sababu niko mkubwa, lakini sababu yeye ni mkubwa, na ni mwema.

Sasa, watiye moyo wanafunzi wako. Waambie kama wakiamini, watatenda mambo makubwa ambayo hawangefikiria.

Ilikuwa neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa katika vijiji. Na mimi Dean Davis nawauliza ni pamoja na wanani utagawanya nao leo neno hili la kutiya moyo ?

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

MIVIRINGO TATU AJILI YA KUWAFANYA WANAFUNZI

  Jambo kwa wote, naitwa Dean Davis, na tazama ''ongezeka'', ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa mak...