Alhamisi, 31 Julai 2025

Hakikisho la wokovu


    Jambo kwa wote naitwa Dean Davis na tazama ''ongezeka'' ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa katika vijiji.

Leo, niliongea na ndugu moja anaye mtumikia Kristo katika inchi ya Afriki ya Mangaribi. Aliniambia kama aliuliza zaidi ya watu 1000 kama wanajuwa ni wapi watakaa milele baada ya kifo chao.

Juu ya watu 1000 walioulizwa, ambao wengi miongoni mwao walikuwa wafuasi na wanashiriki kanisa kila siku ya Mungu, ni watu Saba tu miongoni mwao ambao walitambuwa kama wataishi milele pamoja na Kristo sababu ya kile Yesu aliwatendea. Wengine walijibia kwamba hawana uwakika na mahali ambapo wataishi milele, wala wanajuwa kama wataishi milele katika jehanamu. Ndugu yangu aliguswa sana na vile wengi wanaoingia kanisa hawakuwa na uhakika wa wokovu ndani ya Kristo.

Neno langu la kutiya moyo ni hili hapa : tunaweza kuishi ndani ya dunia hii iliyovunjika na kuwa na uhakika kwamba tuko wana wa Mungu, warithi pamoja na Kristo, waliosamehewa, walio okolewa, waaminifu wenye maisha mapya na ya milele ndani ya Kristo.

Hatuna cha kuogopa kifo wala jehanamu.

Nilipata hakikisho la wokovu wakati nilikuwa na umri wa miaka 13. Na ninahishi na uhakika huo tokea sasa miaka 55. Ona namna hayo yalitendeka.

Niliambia ndugu moja katika Kristo kama sikuwa na uhakika wa kuwa Mkristo. Alifunguwa Biblia yake katika kitabu cha 1Yohana 5:10 na akanisomea haya maneno :

''Yeye amwaminiye Mwana wa Mungu anao huo ushuhuda ndani yake. Asiyemwamini Mungu amemfanya kuwa mwongo, kwa kuwa hakuuamini huo ushuhuda ambao Mungu amemshuhudia Mwanawe.''

Kisha ndugu akaniuliza : ''Dean, je! Uko na Mwana wa Mungu ndani ya maisha yako ?''

Nilijiwaza kwa mda mchache, baadaye nilisema : ''ndiyo. Niliweka tumaini langu ndani ya Yesu kuwa Mwokozi wangu. Anaishi ndani yangu.''

Kisha ndugu alisoma tena 1Yohana 5:11-12 :

''Na huu ndio ushuhuda, ya kwamba Mungu alitupa uzima wa milele; na uzima huu umo katika Mwanawe. 

Yeye aliye naye Mwana, anao huo uzima; asiye naye Mwana wa Mungu hana huo uzima.''

Kisha akaniuliza : ''uko na uzima wa milele? Nilijibu : ''ndiyo, niko na Yesu : niko na uzima wa milele.''

Sasa, ndugu akaniahakikishia : ''Dean, unaweza kuondoka hapa bila kuwa na mashaka ya kwamba uko Mwana wa Mungu, Mkristo aliye na uzima wa milele.''

Je! Unajuwa nini? Niliondoka mahali pale nikiwa na uhakikisho kama mimi ni Mwana wa Mungu na kwamba Niko na uzima wa milele.

Tokea hapo, niliona woga wa kila namna. Lakini sijasikia woga wa kwenda jehanamu wala wa kutengwa na Yesu.

Ninao.

Je! Uko na uhakikisho wa wokovu ndani ya Yesu-Kristo ? Unaweza kuwa nao. Wafuasi wako wanao  huo uhakikisho ? Wanaweza kuwa nao. Tafazali, bila kungoja, wagawia huo uhakika wa ajabu kuhusu uhakikisho wa wokovu kutokana na Neno la Mungu, ndani ya 1Yohana 5:10-12

Mimi ni Dean Davis, naomba ili kuwe kanisa katika kila kijiji cha Afrika, na kila mtu katika hizi kanisa aishi kila siku na uhakikisho mukubwa wa wokovu wa Kristo ndani yake, tumaini la utukufu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

MIVIRINGO TATU AJILI YA KUWAFANYA WANAFUNZI

  Jambo kwa wote, naitwa Dean Davis, na tazama ''ongezeka'', ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa mak...