Alhamisi, 31 Julai 2025

Karama za unabii kwa ajili ya kuongezeka


     Jambo kwa wote, naitwa Dean Davis na tazama ''ongezeka'' ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa katika vijiji.

Katika kipindi changu cha nyuma, nilionyesha kwamba neno ''Mtume'' mara nyingi linaeleweka vibaya, sababu liko na tafsiri nyingi kulingana na makanisa tofauti. Japo hiyo, tunastahili kungojea kwa Kristo atoe Mitume kwa kanisa zetu, kama alivyo ahidia ndani ya kitabu cha Waefeso 4. Tunaitaji watu, waliyotolewa na Mungu, kutumwa ili kufunguwa makanisa mapya pale ambako hayajakuwa bado. Ndivyo ilivyo, kazi ya Mtume !

Waefeso 4 : 11-12 inatuambia : 

''Naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu; 

[12]kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe''.

Oh ! Neno la kwanza katika hii oroza, ''Mtume'', mara nyingi inaeleweka vibaya na la pili : ''Nabii''. Ijapokuwa, Kristo anataka kutowa Manabii kwa kanisa zake ili mwili wa Kristo ujengwe. Lakini kwa kanisa Nabii ni nani ?

Nabii anapokea kwa Mungu uwezo binafsi wa kuwapa moyo kanisa na kuonyesha matukio ndani ya dunia yanayo mchukiza Bwana. Nabii anatangaza ukweli kutoka kwa Mungu na anawaita wakristo kwa utii.

Manabii wanategemea sana maombi na karama za kiroho ili kutimiza huduma yao.

Lakini kama Nabii hatembei kwa Roho, alama mbaya zinaweza kutokea.

Nabii ambaye ambaye hayuko chini ya uongozi wa Roho Mtakatifu anaweza kuchukuwa mwenendo wa hukumu wala kugeuka kuwa mwenye kiburi kwa sababu ya hali yake ya kiroho.

Anaweza kuzania kutowa unabii bila kusikia sauti ya Bwana Mungu wala kuelewa Neno lake ndani ya Biblia. Anaweza ata kuwaziwia wengine kusema ili kutamka maneno yasiyofaa.

Kanisa zenu zinaitaji Manabii, kama vile zilivyo pia na itaji ya Mitume, Wainjilisti, Wachungaji na Waalimu.

Zinaitaji pia kupewa moyo na sahisho. Zinaitaji viongozi wanaochukuwa mda mwingi katika maombi na walio tayari kutowa ujume wa Mungu.

Manabii wanahimiza huduma ya injili na upandaji wa makanisa wakiwaita washiriki kwa vitendo na kuwapa moyo waliyo watiifu.

Lakini uko mwangalifu kwa wale walio na karama ya unabii katikatika yenu? Yesu alisema kwamba atatowa Manabii kwa kanisa zetu. Kama tunapendelea kuwa Mawakili wazuri, tunastahili kuchunguza kuongezeka kwa Manabii, kukubali na kuhimiza huduma yao kuwasahihisha wakati wakienenda pembeni ya Roho Mtakatifu, na kuwapa nafasi ya kutangaza ujumbe wa Bwana. 

Kama vile Mtume Paulo alivyosema katika 1Watesalonike 5:19-22 : ''Msimzimishe Roho; 

msitweze unabii;  jaribuni mambo yote; lishikeni lililo jema;  jitengeni na ubaya wa kila namna''.

Maombi yangu kwa kanisa zenu, Mungu awape wanaume na wanawake wenye nguvu ambao munaitaji ili kutimiza mapenzi yake, ili kukomaa na kuongezeka!

likuwa Ongezeka, na mimi ni Dean Davis nawauliza ni pamoja na wanani utagawanya nao leo neno hili la kutiya moyo ?

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

MIVIRINGO TATU AJILI YA KUWAFANYA WANAFUNZI

  Jambo kwa wote, naitwa Dean Davis, na tazama ''ongezeka'', ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa mak...