Jambo kwa wote! Karibu kwenye Ongezeka, ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa, wachungaji na wasimamizi wa kikristo.
Mimi ni mwenyeji wenu leo, Daneille Snowden.
Leo nitajiunga na kifungu cha Waefeso 4:11-15. Fuatana nami :
''Naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu;
[12]kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe;
[13]hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo;
[14]ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwa huku na huku, na kuchukuliwa na kila upepo wa elimu, kwa hila ya watu, kwa ujanja, tukizifuata njia za udanganyifu.
[15]Lakini tuishike kweli katika upendo na kukua hata tumfikie yeye katika yote, yeye aliye kichwa, Kristo''.
Wakati tunapo fundisha wapandaji wetu wa makanisa, na kuongeza idadi ya wasimamizi wa mikutano yetu, karama ambazo Bwana alitowa kwa kanisa ni za muhimu na zinastahili kuwa sehemu ya mafunzo yetu.
Vesi 14 ya Waefeso inafasiriya wazi sababu gani ni ya muhimu. Hii inaonyesha kwamba Sisi - nitaongeza : kwamba kanisa - tusipelekwe kwa urahisi kuingizwa ndani ya elimu potevu.
Imesemekana : ''...ujanja, tukizifuata njia za udanganyifu''.
Sisi kama viongozi, ni muhimu tufundishe na kuandaa waamini juu ya karama ambazo Mungu alitowa kwa kujenga kanisa.
Nilisikia pia ikisemwa kama ni karama ya binafsi ambayo Mungu anaeneza kwa neema juu ya kanisa na juu ya dunia.
Soma : vesi 12 - ''kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma, hata mwili wa Kristo ujengwe;''.
Moja ya karama ni ile ya Uchungaji (Mlinzi wa Kondoo). Karama hii ya Uchungaji inajionyesha kupitiya huruma na kulinda, kwa kulinda Kondoo, inamaanisha kulinda watu ambao Mungu amempa mtu. Mchungaji anafundisha, akijuwa kwamba mafundisho yake yanalisha kanisa na kuiandaa, kwa mwisho, juu ya kutekeleza mpango ambao Mungu aliandaa kwa kila mmoja. Mchungaji ni Mlinzi mkubwa zidi ya kusanyiko lake. Anakesha juu ya usalama, kwa upekee juu ya mpango wa kiroho. Wachungaji wanapenda tu taifa lao na kutamani kuwa pamoja nao.
Anapenda kujiusisha na maisha ya kanisa lake na kuonyesha msaada wake kwa maombi, mafundisho hata kwa kusaidia kwa namna mbali mbali kulingana na maitaji.
Mchungaji yuko tayari wakati taifa lake linafuraha, hata wakati wanapitiya kipindi cha mateso.
Nilikomaa ndani ya familia ya kiuchungaji, na baadaye, mimi na mume wangu tulifanya kazi ya Uchungaji kwa mda wa miaka 27. Niliona baba na mama yangu wakiwatunza washiriki wa kanisa letu kwa upendo.
Nilisikia joto ya upendo wa Mungu ukitawanyika kutoka kwa wazazi wangu hadi kwa kila mtu.
Nilijifunza, kupitiya mfano wao, ni kwa namna gani jamaa la Mungu liko bora. Niliona wazazi wangu wakilia pamoja na washiriki wao, wakiwatiya moyo kupitiya Neno la Mungu, na kuwaombea. Mimi na mume wangu tulifanya pia hivo, kwa kuwaletea chakula ao kuwasaidia nyumbani kwao kama ikiitajika.
Uchungaji ni kujitolea saa 24 juu ya 24, Siku 7 juu ya 7, kwa wale ambao Mungu alitupatiya. Hii ikiongezwa na ulinzi juu ya mashambulizi ya adui anayetafuta kunyanganya moja ya Kondoo, na kuwa tayari na haraka kumzuiya. Tumeshukuru Mungu kwa karama za wachungaji, karama itokayo rohoni hata pia kwa Mungu. Tuwe waangalifu kwetu wenyewe na kwa wengine kama tukiwa na karama hii, na tujuwe kwamba ni kupitiya Roho wake Mtakatifu ndipo tunaweza kuendelea kupenda na kutumikia taifa ambalo Mungu alitupatiya.
Ilikuwa Ongezeka, asante kwa kugawanya podikasti hii kwa wengine.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni