Jambo wapendwa Kaka na dada, wapandaji wa makanisa.
Mimi ni Mchungaji Douti Claude , Kasisi wa VCP. Hii ongezeka ni podikasti inayoleta maneno ya kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa.
Ninapenda kuwa Kaka na dada wawatiye moyo kuhusu hizi siku zetu 90 za kifungo, maombi na upandaji wa makanisa.
Ninawatiya moyo kwamba musichukuwe siku hizi kwa zarau, bali kuwa na bidii na kujinyenyekeza mbele za Mungu.
Napendelea kuwaambia juu ya unyenyekevu ndani ya upandaji wa makanisa.
Unyenyekevu ni wa muhimu ndani ya upandaji wa makanisa.
Unyenyekevu mbele za Mungu na unyenyekevu mbele za watu unaowahudumia.
Unyenyekevu katikati ya watumishi wa Mungu.
Unyenyekevu ni nini?
Unyenyekevu, ni kujishusha binafsi ; unyenyekevu, ni kujishusha mbele ya Mungu na mbele ya wanadamu.
Ni mda ambao tunashikamana ndani ya kifungo na maombi. Ni mda ambao tunajitenga na dunia hii, na kushikamana kwa uaminifu na unyenyekevu kwa Mungu.
Yakobo anasema katika Yakobo 4:4 urafiki wa dunia hii ni uadui na Mungu, lakini Mungu anapenda wanyenyekevu.
Mungu anatoa neema zaidi kwa wanyenyekevu. Mungu anapingana na wenye kiburi lakini anawapa wanyenyekevu neema, kwa vesi ya 6 ya Yakobo sura 4.
Nyenyekeeni mbele za Mungu kwa mda wa siku 90, hivo mutapata neema zaidi ndani ya maisha yenu, vijiji vitafikiwa, utapokea zaidi ndani ya huduma yenu, mutaono ubora katika huduma.
Petro anarudilia haya kwa wazee ndani ya 1Petro 5:5 anasema kuhusu neema ambayo Mungu anatowa kwa wanyenyekevu na kupingana na wenye kiburi.
Ndugu, uwe mnyenyekevu kwa mda huu wa siku 90 za kifungo na za maombi mbele ya Mungu.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni