Jambo wapenzi wapandaji wa makanisa, Kaka na dada.
Nawasalimu katika Jina la Bwana wetu Yesu-Kristo. Mimi ni Mtumishi wenu, Mchungaji Douti Claude, Kasisi wa VCP. Asubui ya leo, ningependelea kukuambia kuhusu Mada ya ''kuhadisia hadisi za Biblia ''. Kama mujuavyo , Biblia ni kitabu cha hadisi za Mungu kuhusu Mungu na wanadamu. Ili kuelewa vizuri kile ninataka kusema na kuwa na ujuzi wakati wa kuhadisia hadisi za Mungu, unaweza kusoma '' Fundisha na ongezeka '' muhula wa 1 katika ukurasa wa 65-02 hadi ukurasa wa 65-38. Lakini kwa ufupi, napendelea kuwaambia kuwa Yesu-Kristo, ambaye alikuja kama Mwana wa Mungu, yeye mwenyewe alihadisia hadisi za Mungu na alitupa moyo kuifanya, kuhadisia hadisi za Mungu. Katika Mathayo 28, vesi 19 na 20, Marko 16, vesi 15, Yesu alitupa moyo kwenda kuhubiri Habari Njema kwa viumbe vyote.
Katika Mathayo, anasema kwenda kuwafanya mataifa yote kuwa wanafunzi. Na ni wazi kuwa ni hadisi za Biblia ambazo tunastahili kuhadisia watu. Sasa ni nani anastahili kuhadisia hadisi ya Mungu? Ni sisi, kama vile wanafunzi wa Yesu-Kristo. Na kwa wanani tutawahadisia hadisi? Kwa viumbe, kwa wote ambao Mungu aliumba : kwa kila binadamu aliye juu ya inchi, kwa wote ambao wanawaza kusikia Neno la Mungu ambalo Yesu-Kristo aliita Habari Njema, Injili. Sasa, kaka na dada wapenzi, napendelea kuwatiya moyo kusoma zaidi kitabu na kupata maelekezo juu ya namna ya kuhadisia hadisi na sababu gani kuhadisia hadisi za Mungu, hadisi za Biblia.
Namna gani unaijuwa, katika jamaa zetu, watu wanapenda kusikia hadisi. Na unajuwa kama hadisi za Mungu zinafanana kuwa hadisi zisizo na madhara, hazigombane na mtu, haziwatukane wengine. Na mara nyingi, hadisi za Mungu ni za kuchekesha, lakini zinaleta pia tahadhari. Na ziko nzuri kuzisikia.
Inafaa tu kujuwa namna yakuzitangaza kwa wengine. Inastahili kujuwa kuzitangaza kwa ufupi, kwa makini sana, kwa usahihi. Hivo, ili kusimamisha agano lako, inastahili kutayarisha hadisi yako, mara nyingi ukitumikisha picha ndogo, vyombo vya kuleta mifano vinavyoitwa storyboard, kwa kujenga storyboard yako, ao wakati unapo hadisia hadisi, unaweza kumbuka nukta muhimu, sehemu muhimu za hadisi, ili kwamba hadisi iwe hai, ya kweli na ya kufurahisha. Nawapa moyo kwa kujitayarisha vizuri wakati unachaguwa hadisi ndani ya Biblia. Kuko hadisi nyingi katika Biblia, na kama unachaguwa ile ambayo unapendelea kuhadisia, uwe umejitayarisha vizuri sana, uwe na uhakika, na kuwa na uwezo wa kuhamasisha watu kukufuata ili kwamba hadisi izae matunda.
Na kwa Wale wanaokusikiliza, ili kwamba upate watu wanaokusikia na wanapokea Neno la Mungu ndani ya roho zao. Kaka na dada wapenzi, neema ya Mungu iwe juu yenu na iongezeke.
Jifunzeni na kufanya mazoezi kuhadisia hadisi za Mungu.
Mungu awabariki.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni