Jumamosi, 5 Aprili 2025

Punje ya ngano



 Jambo kwa wote, naitwa Dean Davis na tazama ''ongezeka''ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa katika vijiji.

 Maisha ya Yesu ni mfano mzuri kwetu sote. Petro na wanafunzi wengine walipoelewa Yesu alikuwa nani, mafundisho yake yalianza kubadilika. Alielekeza juhudi zake Yerusalemu, mahali ambapo alijua kwamba angesalitiwa, kuhukumiwa vibaya, kuhukumiwa na kusulubiwa. Kwa makusudi alielekea Yerusalemu na msalabani. Na njiani, aliwafundisha wanafunzi wake gharama ya ufuasi. Yesu hakugeuza maneno yake. Alisema waziwazi. Alituita tuchukue msalaba wetu kila siku na kumfuata.

 Yesu alisema katika Yohana 12:23-28, "Yesu akawajibu, "Saa imefika ambayo Mwana wa Adamu hana budi kutukuzwa. Amin, amin, nawaambia, Chembe ya ngano isipoanguka katika nchi, hukaa hali iyo hiyo peke yake; bali ikifa, hutoa matunda mengi. Yeye aipendaye nafsi yake ataiangamiza; na yeye aichukiaye nafsi yake katika ulimwengu huu, ataiokowa kwa maisha ya milele. Mtu akinitumikia na anifuate; na nilipo, ndipo atakapokuwa na mtumishi wangu, mtu akinitumikia, Baba atamheshimu?... Baba, uniokoe na saa hii? Lakini ni kwa ajili ya hiyo ndiyo maana nilikuja, Baba litukuje jina lako!

Unapopanda mbegu ya ngano au mahindi, au nafaka nyingine yoyote, mambo hubadilika.

Mbegu iliyopandwa haifai tena kuliwa. Chini ya udongo,  inakuwa haina maana kula. Umbo lake hubadilika kadiri inavyovimba na kibaridi. Maganda yake hutengana na mbengu. Hakuna mtu anayeiita "mbegu" tena. Kimsingi imekufa na haiwezi kutumika kwa chakula. Lakini ubora zaidi bado unakuja. Kwa sababu mbegu hii isiyo na maana inakuwa mmea mdogo hai, unaokua na mzuri sana. Haionyeshe sura ya chochote, lakini amejaa uwezo! Inapokua na kukomaa, mmea huu mdogo unakuwa mkubwa na wenye nguvu. Kisha hutoa matunda: matunda mengi sana za mbegu. Na huleta furaha kwa mkulima wakati wa mavuno.

 Hakuna hata moja kati ya haya ambayo yangetukia kama ile punje ndogo ya ngano isingeanguka chini, kufunikwa na udongo, na kufa kama punje. Kama Yesu alivyosema, "Chembe ya ngano isipoanguka katika udongo, ikafa, hubakia mbegu moja tu; lakini ikifa, hutoa mbegu nyingi." 

Maisha yako na yangu ni kama punje hii ya ngano: iliyojaa uwezo usioweza kufikiwa. Hatujui ni maisha ngapi tunaweza kuathiri kwa wema ikiwa tutakufa kwa nafsi na kujitoa kabisa kwa Yesu. Lakini tunajua kwa uhakika kwamba ikiwa hatutakufa kwa malengo yetu ya ubinafsi na maono ya kibinafsi ya kumfanya Yesu kuwa mfalme wa maisha yetu, hatutafanya kitu kikubwa cha wema mwingi kwa ajili yetu au wengine katika ulimwengu huu.

Tunakufa kwa ubinafsi kwa kuacha malengo yetu ya ubinafsi kwenda mahali Yesu anataka twende, kufanya kile ambacho Yesu anataka tufanye. Yesu anatutaka twende, tufanye kile ambacho Yesu anataka tufanye, na kusema kile ambacho Yesu anataka tuseme. Hata kama inatugharimu kila kitu. Hapo ndipo ahadi ya Yesu inaanza kutimia. Akasema, “Mmea ukifa, hutoa mbegu nyingi.” Wakristo wanapokufa kwa ajili ya nafsi zao na kuishi kwa ajili ya Mungu, baraka zinazotiririka hazina mwisho. Hii pia ni nguvu ya kuongezeka. 

Mimi ni Dean Davis, nawauliza ni pamoja na wanani utagawanya nao leo neno hili la kutiya moyo ?

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

MIVIRINGO TATU AJILI YA KUWAFANYA WANAFUNZI

  Jambo kwa wote, naitwa Dean Davis, na tazama ''ongezeka'', ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa mak...