Jumamosi, 12 Aprili 2025

Hakikisho la wokovu



      Jambo kwa wote, naitwa Dean Davis na tazama ''ongezeka'' ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa katika vijiji.

Niliongea leo na ndugu moja anaye mtumikia Kristo katika inchi ya Afrika ya Mangaribi. Aliniambia kama aliwauliza zaidi ya watu 1000 ya kwamba wanajuwa sehemu ambayo watakaa milele baada ya kifo chao.

Katika hao watu 1000 aliowauliza, ambao baadhi yao wanashiriki kanisa kila jumapili, ni watu Saba tu ndio walio hakikisha kwamba wataishi milele pamoja na Kristo kufuatana na vile alivyofanya

Wengine walisema kama wanajuwa kama wataishi milele jahanamu. Ndugu yangu alijihusisha sana kwa vile wengi wa wale wanaoshiriki ibada hawakuwa na uhakika wa wokovu wao ndani ya Kristo.

Neno langu la kutiya moyo leo ni kwamba tunaweza kuishi ndani ya dunia hii inayovunjika tukiwa na uhakika kwamba tu wana wa Mungu, warithi pamoja na Kristo, walio samehewa dhambi, wakiwa na uhakika kwamba wako na maisha mapya na ya milele ndani ya Kristo. Hatuna cha kuogopa kifo ao jehanamu.

Nilipata uhakikisho wa wokovu nikiwa na umri wa miaka 13. Nimeishi katika uhakikisho huo tokea sasa miaka 55. Tazama namna gani nilivyo upata.

Niliambia ndugu moja katika Kristo kama sikuwa na uhakika wakuwa mukristo. Alifunguwa Biblia yake kwa kitabu cha 1Yohana 5:10 na akanisomea maneno haya: 1 Yohana 5:10

[10]Yeye amwaminiye Mwana wa Mungu anao huo ushuhuda ndani yake. Asiyemwamini Mungu amemfanya kuwa mwongo, kwa kuwa hakuuamini huo ushuhuda ambao Mungu amemshuhudia Mwanawe. Na tazama ushuhuda huo, ni kwamba Mungu alitupa uzima wa milele, na uzima huo uko ndani ya Mwana wake. Yeye aliye na Mwana yuko na uzima; yeye asiye na Mwana wa Mungu hana uzima.

Ndugu akaniuliza sasa : ''Dean, uko na Mwana wa Mungu ndani ya maisha Yako?''

Nilifikiri kiasi kidogo, kisha nikajibu : ''ndiyo, nilitumainia Yesu kama Mwokozi wangu. Anaishi ndani yangu.''

Kisha ndugu akasoma tena 1Yohana 5:11,12 : ''Na huu ndio ushuhuda, ya kwamba Mungu alitupa uzima wa milele; na uzima huu umo katika Mwanawe. 

Yeye aliye naye Mwana, anao huo uzima; asiye naye Mwana wa Mungu hana huo uzima.'' baadaye akauliza, Dean, watu walio na Mwana wa Mungu ndani ya maisha yao wako na uzima wa milele? Nilikubali, ''ndiyo.'' kisha akaniuliza : ''uko na uzima wa milele ?'' nilijibu : ''ndiyo'' niko na Yesu; niko na uzima wa milele ''. Ndugu huyo ananiambia akiwa na uhakikisho : ''Dean, unaweza kwenda na usiwe na shaka ya kwamba wewe ni Mwana wa Mungu, mkristo aliye na uzima wa milele ''. Je! Munajuwa ? Nilitoka mahali hapo nikijaa uhakika kwamba niko Mwana wa Mungu na kwamba niko na uzima wa milele.

Tokea hapo, nilikwisha kuona woga mara nyingi. Lakini sijawai kupata woga wa kuingia jehanamu ao kutengwa na Yesu. Niko naye.

Uko na uhakika wa kuokolewa ndani ya Kristo ? Unaweza kuokolewa. Wanafunzi wako wanao uhakika wa kuokolewa ndani ya Yesu-Kristo ?

Wanaweza kuokolewa pia. Tafazali, bila kukawia, gawanya nao ukweli wa ajabu wa wokovu, uliotolewa ndani ya Neno la Mungu 1Yohana 5:10-12.

Mimi ni Dean Davis na ninaomba ili kuwe kanisa katika kila Kijiji cha Afika, na kila mtu ndani ya kanisa hizi aishi kila siku akiwa na uhakika ya uwepo wa wokovu wa Kristo ndani yao, na tumaini ya utukufu na upendo wa Mungu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

MIVIRINGO TATU AJILI YA KUWAFANYA WANAFUNZI

  Jambo kwa wote, naitwa Dean Davis, na tazama ''ongezeka'', ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa mak...