Jambo kwa wote, naitwa Dean Davis na tazama ''ongezeka'' ni podikasti inayoleta neno la kutiya moyo kwa wapandaji wa makanisa katika vijiji.
Upandaji wa makanisa ni huduma inayotokana na mafundisho ya nguvu kwa mda mrefu.
Kwa mda wa miaka ine, wapandaji wa makanisa wa kizazi cha kwanza wanafuata masomo ndani ya kituo cha mafunzo cha VCP. Ndani ya kituo hicho, wanasoma na kujifunza Biblia, wanazingatia na kuweka katika vitendo ujuzi mpya za kihuduma na wanaweka kipao mbele kutangaza Habari Njema, kufanya wanafunzi na kupanda makanisa mapya. Lakini hata iwe bora mafundisho kwenye kituo cha mafunzo kwa ajili ya upandaji wa makanisa katika vijiji, haitoshi. Usinielewe vibaya.
Napenda wakufunzi wa VCP na majifunzo yanayo fanyika kwenye vituo vya majifunzo. Lakini haitosheleze kabisa. Kwa kujifunza kupanda makanisa, unastahili kuchunguza wapandaji wa makanisa wakiwa kazini. Acha nirudilie kwamba : ''kwa kujifunza kupanda makanisa, unastahili kuchunguza wapandaji wa makanisa wakiwa kazini.'' kwa hiyo, wakati unapokwenda kufanya kazi ya upandaji wa makanisa, kamata mwanafunzi moja pamoja nawe. Wakati unapofanya huduma ya maombi, chukuwa mwanafunzi moja pamoja nawe. Wakati unaongea na kiongozi wa mji, kamata mwanafunzi moja pamoja nawe. Wakati unapo hadisia hadisi za Biblia, chukuwa mwanafunzi moja pamoja nawe.
Wakati unapo ombea wagonjwa, kamata mwanafunzi moja pamoja nawe. Wakati unapofundisha moja ya agizo Saba za msingi za Yesu-Kristo, chukuwa mwanafunzi moja pamoja nawe.
Yesu alifundisha kwa wamitume kutoka kwenda wawili wawili (Marko 6:7).
Aliwaambia wanafunzi 72 kwenda wawili wawili (Luka 10:1).
Lakini ni sababu gani Yesu alisisitiza kuhusu huduma kwa kikundi ?
Sababu gani alifundisha kila Siku wanafunzi wake kutoka wawili wawili wakati wanapokwenda kwenye huduma na kutangaza Habari Njema ? Nawaza kwamba kuko sababu nyingi. Ilikuwa hatuwa ya usalama. Watu wawili wanao safiri pamoja wako Salama zaidi ya mmoja. Wako Salama zaidi zidi ya mashambulizi na wanaepuka ajali nyingi na magonjwa. Watu wawili wanaofanya huduma yao pamoja, tunakuwa na imani zaidi ya mtu moja anayefanya huduma yake binafsi.
Kwa pamoja wanapatana kwa maombi, na makubaliano haya yanaleta baraka. Yesu alisema; Mathayo 18:19):''Tena nawaambia, ya kwamba wawili wenu watakapopatana duniani kuomba neno lo lote duniani, watafanyiwa na Baba yangu aliye mbinguni.''
Kwa hiyo, kwa kukamata mwanafunzi moja pamoja nawe, usalama wako unaongezeka na nguvu zako za kiroho kwa imani ndani ya Kristo zinaongezeka. Hizo ni sababu zakutosha ili kuchukuwa kila Siku mwanafunzi moja pamoja nawe wakati unapofanya huduma.
Lakini ziko nyingi ! Wakati unapokamata mwanafunzi moja pamoja nawe unapofanya huduma, unatekeleza shabaha mbili kwa wakati moja. Unasaidia wengine na kufundisha mwanafunzi wako.
Yeye atakuchunguza wakati unapojitayarisha kwa huduma. Mwanafunzi wako anakuchunguza, anakusikiliza na kuona namna unavyofanya kazi yako. Anaweza pengine kukuuliza maswali ili kugunduwa sababu gani unafanya yale unayofanya katika huduma.
Uchunguzi huo na mazungumuzo yanaleta faida kwa mwanafunzi na kwako.
Ni hapo majifunzo ya kweli yanafanyika.
Wakati mwanafunzi wako anakuchunguza unapofanya huduma ya Roho Mtakatifu, mawazo, masomo na habari zilizo jadiliwa ndani ya kituo cha mafunzo yanakuwa ya kweli ndani ya roho na mioyo yao. Kwa hiyo, kuchukuwa mwanafunzi moja pamoja nawe wakati unapofanya huduma.
Wafanyishe wanafunzi wako mazoezi ili nawao pia wachukuwe wanafunzi wao pamoja nao wakati wanapofanya huduma.
Kwa kufanya hivo, huduma yako itaimarika na kizazi kipya cha watumishi wakristo kitaendelea.
Ilikuwa ''ongezeka'' na mimi Dean Davis, nawauliza ni pamoja na wanani utagawanya nao leo neno hili la kutiya moyo ?

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni