Habari za asubuhi, ndugu wapendwa wapandaji wa makanisa, nawasalimu nyote katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo asubuhi ya leo. Mimi ni Mchungaji Douti Claude, Kasisi wa VCP Afrika. Ninajivunia weye. Asubuhi ya leo, ningependa kushiriki nawe ujumbe huu muhimu sana kama sehemu ya "ongezeka", podikasti yetu inayoleta maneno ya kutia moyo. Wakati wa siku 90 za maombi, kufunga na upandaji wa makanisa, umefanya kazi ya ajabu kote katika Bara la Afrika. Unaendelea kufanya kazi hii kwa kushinda roho, bila shaka. Tunafurahi kupokea shuhuda zako na kila kitu kinachofanyika. Mungu akubariki na kukutia nguvu. Ningependa kuwaomba ninyi wapandaji wa makanisa wapendwa, watumishi wapendwa, kuomba kwamba Roho Mtakatifu aseme na wale wanaosikia Habari Njema.
Tunahubiri Habari Njema. Watu wanasikia, watu wanakuja kwa Yesu, lakini inatubidi kuwaombea, ili Roho Mtakatifu aseme nao na Roho Mtakatifu akae ndani yao. Kwa nini? Sikiliza kifungu hiki kutoka Warumi sura ya 8, mstari wa 13 hadi mstari wa 16. Inasema, "Kama mkiishi kwa kuufuata mwili, mtakufa, lakini mkiyafisha matendo ya mwili kwa Roho, mtaishi. Kwa maana wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu ni wana wa Mungu, nanyi hamkupokea roho ya utumwa, ambayo itawafanya ninyi tena kuwa na woga ya kufanywa wana, ambayo kwa hiyo twalia, "Aba, Baba." Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu.” Oh, Haleluya! Roho wa Mungu hushuhudia pamoja na roho zetu kwamba sisi ni watoto wa Mungu. Ni uhakikisho wa wokovu wetu.
Roho wa Mungu anatuhakikishia kwamba sisi ni watoto wa Mungu. Unaona, ni muhimu kuomba ili Roho Mtakatifu aseme nasi, ili Roho Mtakatifu akae ndani yetu. Lakini hii itatokeaje? Ni kwa kujitenga na mambo ya maisha, kutoka kwa mwili, kutoka kwa tamaa za mwili, na kwa kuishi katika roho, kujitoa zaidi kwa mambo ya kiroho, kwa mambo ya Mungu. Maana mstari wa 13 unasema, “Kama mkiishi kwa kufuata mambo ya mwili, mtakufa lakini mkiyafisha matendo ya mwili katika Roho, mtaishi. Ndugu wapendwa, akina dada wapendwa, wapandaji wa makanisa, lazima tuombee waamini wapya, wale wote wanaomkubali Yesu. Roho Mtakatifu aseme nao, Roho Mtakatifu awaongoze. Waache kufisha tamaa za mwili na kushikamana na mambo ya Mungu, na kumpenda Mungu na kumwabudu Mungu katika roho na kweli. Na Roho Mtakatifu ataendelea kuwatia hatiani na kuwahakikishia kwamba wao ni watoto wa Mungu. Inafurahisha sana kujua kwamba wewe ni mtoto wa Mungu. Anasema Roho anatusaidia. Ni lazima tuelewe kwamba tumepokea roho ya kufanywa wana. Tumefanyika wana wa Mungu na sisi ni watoto wa Mungu. Na kwa roho hii tuna haki ya kulia “Abba, Baba,” kumwita Mungu “Baba Yetu.” Inapendeza kusikia hivyo. Lakini bila Roho wa Mungu hatuwezi kuelewa mambo haya. Bila Roho wa Mungu, hatuwezi kuacha tamaa za mwili na kupendezwa na mambo ya Mungu. Asubuhi ya leo, wapandaji wa makanisa wapendwa, nataka kuwatia moyo muombe kwa bidii Roho wa Mungu aseme na akili za wote wanaosikia habari njema.
Wakae ndani ya Kristo na wawe na uhakikisho wakuwa watoto wa Mungu.
Nawashukuru. Nawatakia Siku Njema.
Amani kwenu.
Ilikuwa ongezeka.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni